Mishakaki ya Paka

Mishakaki ya Paka

Khaaa! Hadi nahisi kichefuchefu.
Ashtakiwe aisee kama sheria inaruhusu.
 
Nilisikia hii kitu jamani puuuuh disgusting..mishikaki mie basi.looh!
na anaongea huku akicheka as if anachofanya ni sifa.
Je watu wangapi watakuwa wamedhurika bila kujua sababu ni nini?
Pamoja na kwamba kuna nchi wanakula paka ila wanapitia process mpaka ije kufaa kuliwa sio kama anavyofanya jamaa huyo..
Ila hii yote ni dhiki..kama kungekuwa na ajira za kutosha asingefanya hivi.duh.Mungu atuepushe.
 
hee! haya bwana ingawa anajasiria kupata mali, lakini anshitua kidogo, ila kama wanaokula wanaona ni tamu na haijawadhuru kwa muda wote huo, basi aendelee na biashra cha muhimu awaeleze watu ukweli wa aina ya nyama anyoiuza.
 
Naona kuwa Clouds FM walipaswa kumripoti huyu jamaa kwenye vyombo vya sheria. Haiyumkiniki kumuhoji mvunja sheria na kumuacha aendelee kuvunja sheria tena kwa kumuhifadhi jina lake.

Tuliopita Manzese jana jioni tuliona kuwa watu wamegoma kabisa kula mishikaki wakihofia kula paka. Hii imewaharibia kweli wale wanaofanya biashara halali.
 
Mlio sikiliza power breakfast Leo najua Mmeipata vizuri.
Jamaa mburahati kauza mishkak ya paka for the last four years!
Amekiri kwa siku anauza paka wanne na kuendelea.
Hivi huyu jamaa hawezi chukuliwa hatua zozote za kisheria?
Jamni hii inasikitisha!!

Hawa wanyama wana soko sana kule china, kwa hiyo ni msosi wa kawaida tu ni kama sungura
 
Kwani wanaokula umbwa, unyoka, upanya mbona hamsemi , unyau tu ndo maneenoooooooo acheni hizo wananchi
 
huwezi kufananisha hivyo vitu viwili
yule ni mwongo kwa sababu aliulizwa familia yako inajua kwamba unafanya shuguli hizo ie unachinja na kupika mishkaki ya paka akasema ndio.. nasomesha watoto wanne shule kwa kazi hiyo

akaulizwa; je wewe na familia yako mnakula hiyo nyama... akazunguka mwisho akasema hapana, hata hawajui kwamba nafanya kazi hiyo....
why contradict yourself???

mtu wa wapi eti mpogolo ukimsikiklliza anaonekana mmakonde

Haya ndio yanayonifanya niamini kwamba huyo jamaa anaweza kabisa kuchinja paka na kuuza mishikaki yake, kwa sababu yeye mwenyewe ni kama akili hazimtoshi, nilikuwa nasikiliza kipindi siku hiyo, naamini bonge hakuwa anadanganya, swali la kujiuliza ni labda bonge alipataje habari za huyo mtu mpaka akaenda kumhoji? kama ni taarifa kutoka kwa raia wema ina maana haikuwa siri basi
 
Is this true??????????????????????? Or my lord!!! Ni mburahati ipi maana kuna kipindi nilikuwa naenda kwa mshkaji wangu anakaa mburahati bondeni. Ikawa tunatoka na kwenda kula mishkaki maeneo ya kijiweni.....ni wapi huyu jamaa alikuwa???
Haa haa haaaa!! Mkuu, vipi unataka ujitapishe kabisa au?! Hatari kweli kweli.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom