Mishahara ya Wake Zetu

kiukweli matumizi ya fedha kati ya wanandoa yanategemea mipango yao binafsi.

mimi bnafsi sipendi hela za kuaomba na wala sipend life standard ya familia iwe mbaya. what we do huwa tunapriotise each month kwamba tunakazi gani mbele yetu. iliyopo tunaangalia kipato chetu wawili kinaweza kusustain vipi kazi husika. hii ni ile inayobaki baada ya kushop for groceries, na other costs pamoja na za kuwapa wazazi kila mwezi.

kuhusu kwenda salun kwa mm hiyo ninaifanya alone but siku moja moja hubby ana sponsor ili kuonyesha kujali. kuhusu mavazi ya kids na sisi wenyewe huwa tuna karatiba ambako tunakafwata na inapotokea umekutana na kitu kizuri ukakitamani basi unaweza kununua.

malipo ya watumish wa kazi iwe shamba ama home nayo pia tuna fanya collectively hakunaga pesa za mama wala za baba zote ni za familia na tunahakikisha zinafanya kazi zafamilia.

michango ya harusi, k/party na send offs zikuhizi hatuchangi kabisa wala hatauendi, tunatoa rambi rambi kwenye misiba na kusaidia wakati wa ugonjwa basi. tulifikia hapo baada ya kuona kwamba kwa mwezi unaweza kuwa na kadi hata 15 zote michango so unajikuta zaid ya kuchanga huna kingane unachofanya.

yote ni sawa ila inategemea wewe na mkeo mtapanga vipi jinsi ya kutumia kipato chenu, sio vibaya kadi zenu za benki zikawa eneo ambalo ni accessible kwa nyie wote wawili, na sion kama kuna ubaya hata pasword mkipeana so long as mnatumia hela vizuri.

sipendi daima milele mwanaume mfujaji na nashukuru sana Mungu hakunipa wa aina hiayo manake kiukweli lazima angeniua tu. mimi kwangu cheza na mimi utakavyo but not hivi vitu viwili, watoto na pesa/mali zangu lol! hapo lazima nitawakilisha lile kundi la upalestina sina masihara.
 
Fairly, inatakiwa wote wawili mke na mume mchangie kipato chenu katika maendeleo ya familia zenu. Pesa ya mke ni ya mume na ya mume ni ya mke. Tatizo kubwa linalofanya wanawake wawe wazito kuchangia maendeleo ya familia zao ni TABIA YA WANAUME TENA WALE WENYE KIPATO KIKUBWA/WASTANI KUWA NA NYUMBA NDOGOO!!Mke anahudumia familia mume anahudumia nyumba ndogo, ndio maana wanawake wengi wanakwambia pesa ya mume ni yao wote ila ya mke ni yake yeye tu.
 
mjengo wa nini huko kwenu wa kaka zako sio but kumbuka wana wake zao na watoto wao...yaani unaacha kujengea wanao unamjengea wifi yako na wanae ...teh

aise mi nilijenga kwetu, mr alimind sn......akasema mwanamke akiolewa anajenga kwake na sio kwao...ajabu lakini yeye ndiye aliyeanza kujenga kwao lkn hiyo ikawa sio tatizo, tatizo ni mimi kujenga kwetu....acheni roho mbaya bwn... yaani hata tukiwasaidia wazazi/ndugu hamtaki eti kisa kuolewa!! ujue hao ndio waliotusomesha
 
duuuh yaani mwanamke unajenga nyumba kwenu,tena kijijini? mmmh mimi sijengi hata banda la kuku pale ni kwa ndugu zangu wa kiume nitapaeshimu na kwenda pale kama mgeni tu...nitajenga kwa mume ambako ndo sehemu halali ya watoto wangu

Mmmh kila mtu anaplan zake.... kwakweli naheshimu hilo. Mimi kwakweli kuchanga na mume kwenye mjengo ni kitu ambacho I will do in writing na any case warithi au wamiliki wanakuwa ni watoto wetu tu. Wanawake wengi weshalizwa, at the time of divorce or death, linatoka rundo la watoto na wote wanahaki kurithi ambapo wewe umetia jasho lako.
 
Du, mambo haya! Hili swala mbona si gumu? Unajua siku hizi watu hawautumii vizuri uchumba. Kipindi cha uchumba mambo ambayo unatakiwa kuyaweka bayana mojawapo ni namna gani pato lako na la mkeo litatumika ktk familia! Tatizo vijana wa dot com, kipindi cha uchumba wanachakachuana tu basi wanasahau kwamba kipindi hiki ni cha kuweka msingi wa namna familia yenu itakavyokuwa endapo mungu atawabariki mkafanikisha lengo lenu la kuoana! Mimi namzidi mke wangu mshahara Mara mbili na point kadhaa lkn ninachofanya mwisho wa mwezi ni kuchanganya pesa then matumizi yetu naya misaada kwa ndg tunaweka pembeni na inayobaki inaenda kwenye plan ya kuendeleza familia yetu! Saluni na nguo huwa haombi kwani huwa nautamaduni wa kumpa hata kabla hajaniomba kwani pia mm huwa nimtu wa kusapraizi! Sipendi sana mwanamke asiyetaka mumewe ajue mshahara wake wala anayependa kutumia anavyotaka bila kunishirikisha mimi mme wake! Nahisi inafanya ndoa Kuwa na walakini kwani ushirikiano ni mhimu! Na mm hupenda ajue badiliko lolote la mshahara wangu siku yoyote! Nawashauri wanawake mbadilike kwani vitu hivi vinaweza kusababisha mmoja wenu Kuwa na kinyongo, unapoolewa muwe tayari kupanga namna na kutumia pesa zenu kwa pamoja, siyo mnataka HAKI SAWA huku hamtoi ushirikiano si sawa! we are happy with this life!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 

shule nzuri tu kwa wenye masikio, macho na uwezo wa kusoma na uelewa. ndivyo niishivyo na wife. hajawahi niuliza napata sh. ngapa lkn anajua changu kikubwa zaidi ya mara 2 kwa chake. mimi najua take home yake kwani mimi ndo nimekabidhiwa ATM, nachukua kama ninashida natumia, namjulisha na hawezi/hajawahi kataa hata siku moja. Yeye akiwa na shida ananiambia, na tunasolve fasta kama salio langu linasoma.

watakao kuelewa hapo ni wakristo tu, waislam na wanaooa kimila hawatakuelewa kwani malengo ya ndoa yanatofautiana sana.
 

In writing? Kwamba mnaita wakili ana-draft mkataba kwamba wewe Mrs. X umejenga nyumba kwa kushirikiana na mume wako Mr. Y kwa hiyo lolote litakalotokea nyumba inagawanywa pasu kwa pasu (baada ya kuuza)

Kama ndiyo hivyo......mtarudi kwenye sofa, kitanda mwishowe hata mboga.....Kaazi kweli kweli.
 

Nifanye kazi mimi kadi ushike wewe, naua mtu.....:boxing:
 


Yes please.....
 
acha ukabila kila mtu na mawazo yake mimi mwenyewe mchaga

I'm sorry kama nimekuoffend Smile, lakini nilichokuwa nazungumza ni kuwa mila na desturi za kabila zina mchango pia katika kuathiri mafikirio ya mtu. Wachaga si wote, heshima ya mtu huwa ni kujenga nyumbani. Ni tofauti na makabila mengine ambayo kujenga home si issue, kama nimefanikiwa nikiwa dsm, basi maisha yangu na wanangu yatakuwa ya dsm. Ni wachaga wachache kwa simple research ynagu wanaoignore suala hili. wengi wanalifanya, na kinachosababisha hali hii ni utamaduni wa wachaga kuwa na vikao vya kifamilia kila mwaka kwenda nyumbani. na baadhi ya jamii za kichaga, usipojenga unaweza nyimwa sehem ya kulala. Nimeyaona pande za KIRUA VUNJO haya. Na ngoma huwa nzito wakati wa msiba.

Hata hivyo wachaga wa kimarngu atahari hii haijawachukua sana, wanaweza kubalance wakafanya vitu kote kote, sasa kama uwezo ni chini watajali kwake, yaani kwao na watoto wake.

Lakini nisamehe kama umenikoti vibaya dada Smile.
 
Nifanye kazi mimi kadi ushike wewe, naua mtu.....:boxing:

wanawake wa aina yako wapo tena sana. wapo wanaoamua kuua waume zao ili warith mali, wafuatilie mirathi iwe milk yao na wengine hutaka kuonekana wajanja kwenye familia zao. Ni mila tu na desturi ndizo zilizoathiri hadi kwa kiwango hicho.
 
Duuh!! Hapa atleast nimepata picha na mwanga jinsi wanawake walivyo, na ndio maana ni rahisi sana kwa shetani kuleta uharibifu kupitia wanawake na pesa. Na hii ndo sababu wazi wanaume wengi katika ndoa wana mizigo mizito sana ila huwa hawana muda wa kufanya u-beijing .
Wakati wanaume wakiwa wana jitahidi kupambana na uchumi duni na uboreshaji wa maisha wanawake walio wengi wana endekeza ubinafsi na uchoyo, Waume na mizigo ya mke, watoto, ujenzi, kazi nk nk nk = stress = stroke = early death = mjene = yatima = machangu = majambazi = nk nk nk nk.

Dunia hii Mungu ametupa iwe nyumba yetu kwa muda kidogo wa kuishi hapa lakini wanawake wapumbavu wanaibomoa kwa mikono yao.
Wanawake wenye hekima ombi kwenu, wafunzeni mabinti zenu kama mlivyo funzwa na Roho si kuwa wanaume wanataka muwape pesa zenu ila ushiriki wenu katika kuendeleza ustawi wenu kwa pamoja kama familia vinginevyo mambo hayata enda.
C U soon
 


hapo kwenye red naomba nikujibu upande wa waislamu, kwa waislamu mambo haya ni straight forward, wala hakuna mjadala.. baba ndio provider wa familia kwa kila kitu (ni lazima sio hiari) wife hana obligation yoyote ya kutunza familia... wife anaruhusiwa kufanya kazi/biashara n.k na kipato chake ni cha kwake yeye mwenyewe..mume hana chembe ya mamlaka kwenye kipato/mali ya mwanamke...ni hiari yake kutoa au asitoe..halazimishwi (Allah knows best)
 

suala ni kuwa na program ya familia. hv kama umeolewa, siku ukifa utazikwa wapi? kwenu au kwao na mme? kuasaidia wazazi ndugu ni jambo jema sana lakini kushikilia mshahara na kudai mambo ya familia yanakuhusu wewe (mme) na wewe kudai mshahara wako ni mali ya kwenu si jambo zuri, labda kama mme wako umemfanya kuwa hawara hapo sawa kabisa.
 
wanawake wa aina yako wapo tena sana. wapo wanaoamua kuua waume zao ili warith mali, wafuatilie mirathi iwe milk yao na wengine hutaka kuonekana wajanja kwenye familia zao. Ni mila tu na desturi ndizo zilizoathiri hadi kwa kiwango hicho.

Duuuh wewe hujui hata kuchill, soma kwanza ufahamu usitoke mapovu ya bure.
 

hakika kabisa. ndo maana niometoa maneno hayo. Waislam hawana suala la mwili mmoja, iko toafut kabisa. Na kuna jamaa yangu yeye wife wake hajui hata hela yake anaitumia vipi, nilipomwuliza kasema yuko sahihi na wala siwezi kumwuliza najua wajibu wangu kidini. sikuwa na nyongeza ila kukubali tu.

Na kuongezea kwenye mila na desturi (makabila) zipo jamii huamini mke ndo kila kitu, na watoto wanakuwa ni wa upande wa mwanamke, hivyo huwezi mwambia kujenga kwake hata siku moja, bali atajenga kwao kwa kuwa naamini anawaandalia watoto wake makazi
 
nashauri wanawake msitumie fedha zenu kw matumizi ya familia maana ukimwachia mwanya tu anahonga za kwake ,mpe majukumu mengi ili akose hela yakuhonga full stop!!!!!!!!! cacico njoooooooooo useme unafanyaje weye one day ulisema na hii ilinikaa sana kichwani kuwa nyie mna account moja ya familia mnadonate au nimekosea????????
 

Kuzikwa unazikwa kwenye udongo regardless hakuna ulazima wa kuzikwa ukweni. Mimi nitaenda kidini zaidi, muislam anazikwa kokote, mwanamke wa kiislama habebi jina la ukoo wa mume. Mme kutunza family ni wajibu wake, nitasaidia ikibidi na inapohitajika. Mimi kama mimi mume atakaponionyesha kuwa yeye ndo head wa family kwa kubeba majukumu zaidi, hilo halina mjadala nitasaidia tu

Lakini 2nd day of our marriage mambo ya 50/50 asinianzie....maana hakitaeleweka.
 
da!!!!!umenivunja mbavu mwenzio!!!!!!!

habari ndo hiyo...ukiona wanaume wanalalamika weeeee lakini hawa-divorce hao wanawake wanaowasumbua unafikiri ni kwa nini,..yaani mwanamke akishaenda huko kwa hao wanasheria akaorodhesha mali zenu halafu akaambiwa mgao wake ukoje utashangaa aliondoka asubuhi analia anarudi jioni anacheka..tena kama mwanamke ana roho nzuri kidogo atakuambia...Baba watoto acha bange....
 
Basi Sawa

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…