Mishahara ya wake zetu


Dunia imebadilika kwanza hilo tulijue.
Hapo mwanzo Mungu alipoweka mgawanyiko wa majukumu-Adamu kwa jasho utakula na wewe Hawa kwa uchungu utazaa, mambo yalikuwa kama hivyo . Waume mashambani na wanawake majumbani kuzaa na kulea watoto. Ila ninaposema dunia imebadilika ni kwamba haya nayo yamebadilika.
Leo hii wanawake si lazima wazae kwa uchungu- Tunashuhudia operations nyingi wakati wa kujifungua , wasichana wengi wanazaa kwa visu. Hapo hakuna Uchungu uliosemwa na Muumba.
Hali ya maisha/Uchumi unamlazimisha mwanamke atafute kazi. Wengi wameenda shule na kupata nafasi/ madaraka makubwa.

Kwa maana hiyo basi Mshahara wa mwanamke unapaswa kuingia katika mipango mizima ya kuinua familia kiuchumi.Nasema hivi kwasababu zile roles zilizokuwepo zamani zimebadilishwa na binadamu kubadilishwa (kwa kupenda au kutokupenda) na mabadiliko ya dunia (ya kiuchumi, kijamii kama elimu n.k)

Kwa busara kabisa mshahara wa mwanamke lazima utumike kuijenga familia (kidole kimoja hakivunji chawa) Hii haimaanishi heshima ya baba kama kichwa cha nyumba itaondoka.
Ila cha kuzingatia mchango wa baba uonekane zaidi, siyo akae tu kusubiri mshahara wake na wa mkewe awe na akili ya ziada ya kujishughulisha na kuleta ziada nyumbani.Hii inatokana na ukweli kwamba physical ability alio pewa na Mungu unamfanya afanye zaidi kuliko mkewe.
Let say kama ni fundi ujenzi wa kulipwa anaweza kujishughulisha na ziada ya kubeba zege kama kibarua kingine kuleta ziada atleast na tofauti yake na mkewe.



Ahsante jembe langu. we nijiasi. unakili zakutosha. ongela sana niayo tu, ningekuwa no. yako ningekutafuta

 
mshahara wa mwanamke ni kuishia saluuni .
No way.
Mke si mchumba. Ana wajibu kwa familia yake lazima achangie pato la familia. Mchumba hana wajibu huo. Ukishaolewa/oa, mapato yote ya waliooana shurti yawe mali ya familia, otherwise mvunjiko mkubwa lazima utokee.
..na hata mkitoka sio ujionyeshe wwe ndio kidume kwa kulipia kila kitu...unaweza kumwambia unalipia chakula yeye alipie drinks.....
Hapo kwenye bold hapo.
Kwa mabinti wa siku hizi (CBE/IFM/Mabibo Hostel type) lazima akumwage. Cost sharing huwa inakera mabinti wengi, ingawa ni nzuri in a long term.

na pia mkeo ni rafiki yako,tangu mwanzo kuwa na tabia ya kuwasiliana naye jambo unalopenda na usilopenda....hii itakurahisishia baadae kumface na kumwambia jambo lolote kama unaona anaenda sivyo.usiwe mtu wa kunyamaza kimya au kujifanyia mambo mwenyewe itakucost siku moja.
Nakubaliana na wewe kwa pointi hizi, ila uwazi usizidi sana, na wenyewe una gharama zake katika mahusiano.

mwanaume aliambiwa na muumba, uzae uwe na familia na mtakula kwa jasho lako. mwanamke akaambiwa utazaa kwa uchungu. Labour naingia mwenyewe kusukuma mtoto kwa machungu, halafu eti mshahara wangu niweke mezani..! nyie wababa vipi? mbona hamnazo? wanaume wa kileo kupenda dezo! hebu tuleeni sisi na watoto wetu kwa jasho kama mlivyotumwa, achaneni na mishahara yetu. nikisaidia ni mapenzi yangu lakini sio wajibu wangu na huna sababu ya kuuliza au kukwazika juu ya hilo.
Madame Sal,
Hala hala vidole na macho. Povu lote hilo hilo kisa mshahara tu? Share pato lako na mwandani wako.

Anadamka asubuhi kwenda kibaruani, anachelewa kurudi kibaruani sababu ya foleni afu nisiujue mshahara wake na unatumikaje?....... I better marry my mom!

Othetwise akae nyumbani anilelee wanangu.... PERIOD!
Teh teh teh. Hapo kwenye bold hapo
 

Dunia imebadilika kwanza hilo tulijue.
Hapo mwanzo Mungu alipoweka mgawanyiko wa majukumu-Adamu kwa jasho utakula na wewe Hawa kwa uchungu utazaa, mambo yalikuwa kama hivyo . Waume mashambani na wanawake majumbani kuzaa na kulea watoto. Ila ninaposema dunia imebadilika ni kwamba haya nayo yamebadilika.
Leo hii wanawake si lazima wazae kwa uchungu- Tunashuhudia operations nyingi wakati wa kujifungua , wasichana wengi wanazaa kwa visu. Hapo hakuna Uchungu uliosemwa na Muumba.
Hali ya maisha/Uchumi unamlazimisha mwanamke atafute kazi. Wengi wameenda shule na kupata nafasi/ madaraka makubwa.

Kwa maana hiyo basi Mshahara wa mwanamke unapaswa kuingia katika mipango mizima ya kuinua familia kiuchumi.Nasema hivi kwasababu zile roles zilizokuwepo zamani zimebadilishwa na binadamu kubadilishwa (kwa kupenda au kutokupenda) na mabadiliko ya dunia (ya kiuchumi, kijamii kama elimu n.k)

Kwa busara kabisa mshahara wa mwanamke lazima utumike kuijenga familia (kidole kimoja hakivunji chawa) Hii haimaanishi heshima ya baba kama kichwa cha nyumba itaondoka.
Ila cha kuzingatia mchango wa baba uonekane zaidi, siyo akae tu kusubiri mshahara wake na wa mkewe awe na akili ya ziada ya kujishughulisha na kuleta ziada nyumbani.Hii inatokana na ukweli kwamba physical ability alio pewa na Mungu unamfanya afanye zaidi kuliko mkewe.
Let say kama ni fundi ujenzi wa kulipwa anaweza kujishughulisha na ziada ya kubeba zege kama kibarua kingine kuleta ziada atleast na tofauti yake na mkewe.




Nimependa mtizamo wako!
 
hata mwanamke awe waziri (mshahara mkubwa kiasi gani) na mwanamme awe mwendesha mkokoteni (mshahara mdogo kiasi gani), bado mwanaume ndie atakaewajibika kwa matumizi ya ndani! ni moja kati ya vitu vinavyosababisha migogoro ndani ya ndoa maana ni lazime utamuuliza, na ukishamuuliza huyo mwanamke atanuna wiki nzima na vyote likizo ie unyumba n.k.
ndoa za sasa ivi, Mungu ashushe rehema zake tu lakini kazi nzito!!!!

Hapo pekundu: Dah, hii silaha yao huwa inaniacha hoi kabisa yaani!!! sijui wanapasishana huko kwenye ma-kitchen party yako!
 
Changu ni chetu, chako ni chako. mkatae mkubali huo ndio ukweli, kutegemea utakiona kipato cha mwanamke sahau mpaka uingie kaburini, yaani utaombwa hata kiberiti cha tshs 50, mshahara wa mwanamke ni kusaidia ndugu zake, ukitaka ufahamu ukweli linganisha maisha ya mwanamme ambaye ameoa mfanyakazi na mwanamme ambaye hajaoa mfanyakazi maisha hutaona tofauti katika maisha.
 
simuuliz mke wangu mshahara coz she is
da best house keeper and budgeter ever!
Hajawahi lalama nimempa pesa ndogo so it means mayb anaongeza na zake samtimes.

Shabby, zake anazipata wapi? Do you know all her sources? LOL
 
[/I][/B][/COLOR]Wewe akili yako ndogo kama "pelege" au "kamongo" maana unacho ongea ukielewi, kama unajuwa mshaala wako ni wako pee,

Qn. kwanini ulikubali kuolewa naye kwanini usingekaa alone ukafaidi matumizi yako pekee. iyo ndiyo akisawa mnayo lilia everday acha mbwembwe na acha tabiaya ya hooogoo?.

nakasubilia kwa haamu sana ikikupeni njoo tuongee

haijanipain. Bye bye.
 
Kama ndio hivyo afadhali nioe asiye na kazi, ni jue moja. Inavyo onekana walio na wanawake wanao fanya kazi ni shida tupu hasa wanawake wakibongo. Na hili ndoo linalo sababisha mwanamake kufanya hata vitu visivyo na maana kwa kuwa huwezi kumfanya chochote ana pesa yake. Nikifikilia hili naogopa kuoa mwanamke aliye soma kwa sababu najua anakaujinga kalekale kanako zungumzwa hapa. think like men but act like a woman.
 
Changu ni chetu, chako ni chako. mkatae mkubali huo ndio ukweli, kutegemea utakiona kipato cha mwanamke sahau mpaka uingie kaburini, yaani utaombwa hata kiberiti cha tshs 50, mshahara wa mwanamke ni kusaidia ndugu zake, ukitaka ufahamu ukweli linganisha maisha ya mwanamme ambaye ameoa mfanyakazi na mwanamme ambaye hajaoa mfanyakazi maisha hutaona tofauti katika maisha.

Mkuu nitafanya kautafiti kadogo nijue kama upo sahihi hapo kwa red!
 
Kama ndio hivyo afadhali nioe asiye na kazi, ni jue moja. Inavyo onekana walio na wanawake wanao fanya kazi ni shida tupu hasa wanawake wakibongo. Na hili ndoo linalo sababisha mwanamake kufanya hata vitu visivyo na maana kwa kuwa huwezi kumfanya chochote ana pesa yake. Nikifikilia hili naogopa kuoa mwanamke aliye soma kwa sababu najua anakaujinga kalekale kanako zungumzwa hapa. think like men but act like a woman.

Mkuu hapo kwa red unamaanisha hili tatizo lipo kwa wanawake wasomi tu?
 
Mie simuulizi mshahara wake ila ananinulia apendacho km shati, viatu n.k kwangu inatosha tu
 
Back
Top Bottom