mito
JF-Expert Member
- Jun 20, 2011
- 10,513
- 10,404
Jamani kuna malalamiko miongoni mwa wanaume waliooa wanawake wafanyakazi kuhusu mchango wa mishahara yao ktk matumizi ya familia. Nina marafiki wangu kadhaa (waliooa wake wafanyakazi) wote wanadai eti ukitaka kuishi kwa amani na mkeo usimuulize kuhusu mshahara wake. Nilishangaa sana kusikia hivi kwani mara nyingi huwa nasikia vijana wengi wanataka kuoa wasichana wenye kazi ili waweze kusaidia ktk kupunguza ukali wa maisha. Naombeni uzoefu wenu ktk hili jamani. Natanguliza samahani kama topic ilishaongelewa huko nyuma, ila ningetamani kuona hizo sred ili nisome maoni ya wadau!