Mishahara midogo kazini

Mishahara midogo kazini

Ty tanick

Member
Joined
Jun 18, 2021
Posts
8
Reaction score
6
Mkoa wa Katavi, wilaya ya Mpanda kuna kampuni moja ni maarufu sana inajihusisha na mambo ya mazao inatoa mikataba feki kwa mwafanyakazi wake pia inachelewa sana kulipa mishahara, kima chao cha misharaha ni 100k hadi 225k ila kupata ni hadi kelele kwanza

Hii ndo Tanzania wewe kama una kazi na unalipwa bila shida yoyote haijalishi ni kiasi gani wewe piga kazi
 
Tatizo ni kwamba mambo kama hayo hayapigiwi kelele.

Watu wanapigia kelele Tume huru ya uchaguzi na katiba mpya.

Kwasababu wao siyo waathirika wa hii mishahara midogo.
Upo sahihi. Wanaamini tume huru itawapeleka bungeni ili walipwe 12M per month wakati wananchi walio wengi mishahara yao haivuki posho za wabunge 300k per month kama basic salary.

Ila siwalaumu maana wanatetea matumbo yao.

Tatizo kubwa kuliko hilo la mishahara midogo ni ukosefu wa ajira. Ndoto za vijana wengi zimekufa na hivyo kulazimika kufanya kazi kwa kunyonywa na kulipwa 125k per month.

Huo ndio uchumi huria mkuu. Wenye nguvu watatoboa, wanyonge watajifia.

Dunia haina huruma
 
Back
Top Bottom