Misemo ya Kiswahili inayotumika sana siku hizi itokanayo na tafsiri ya Kiingereza

SHIEKA

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,244
4,258
Habari zenu wanaJF? Naleta mbele yenu misemo miwili ya kiswahili inayotumika sana siku hizi lakini ni direct translation ya Kiingereza.Misemo hiyo na kiingereza chakei ni kama ifuatavyo:

1.Mwisho wa siku= Ni kiingereza cha: at the end of the day. Fungua tv au redio yako, kaa dakika tano tu hutaacha kusikia huu msemo wa mwisho wa siku. Kwanini tusiseme 'hatimaye' au 'baadaye?
2. Kwa namna moja au nyingine= Ni kiingereza cha: in one way or another.Hii sipendi kuisikia; inanipa kichefchef kwa sababu kama ni namna moja au nyingine, maana yake ni namna mbalimbali. Kwa nini hatusemi kwa namna mbalimbali?
3.Unaboa = Ni kiingereza cha you are boring. Hata hapa JF, hii inatumika sana.Kwa nini hatusemi unachosha au thread yako ni ndefu inachosha? Kila mara utasikia au kusoma Huyu anaboa sana.
4.Ongeza misemo mingine uliyosikia au kusoma
.......................................................................
........................................................................
 
Chini ya kifungu cha X cha katiba - Under article X of the constitution: Hili ni kosa kwani unaposema "chini ya kifungu X maana yake hukusudii kifungu Y bali "Katika kifungu hicho hicho cha X".
Aidha...au - Either ...or: Si sahihi badala yake ingekuwa "ama ...au"
 
Ila hiyo namba 2; tafsiri haijakaa vizuri (namna mbali mbali); ni bora ungesema kwa "kwa namna yoyote" kidogo hiyo yaweza kuwa karibu na sawa na hiyo "in one way or another".

Lkn pamoja na hayo mimi sioni shida sana kutafsiri Maneno kama!
4: sina machaguo .... I have no options
5: karibu na kutowezekana .... Next to impossible
6: kwani we ni nani.... Who do u think u r
7: nakukosa.... I miss u
Na kadhalika
 
Habari zenu wanaJF? Naleta mbele yenu misemo miwili ya kiswahili inayotumika sana siku hizi lakini ni direct translation ya Kiingereza.Misemo hiyo na kiingereza chakei ni kama ifuatavyo:

1.Mwisho wa siku= Ni kiingereza cha: at the end of the day. Fungua tv au redio yako, kaa dakika tano tu hutaacha kusikia huu msemo wa mwisho wa siku. Kwanini tusiseme 'hatimaye' au 'baadaye?
2. Kwa namna moja au nyingine= Ni kiingereza cha: in one way or another.Hii sipendi kuisikia; inanipa kichefchef kwa sababu kama ni namna moja au nyingine, maana yake ni namna mbalimbali. Kwa nini hatusemi kwa namna mbalimbali?
3.Unaboa = Ni kiingereza cha you are boring. Hata hapa JF, hii inatumika sana.Kwa nini hatusemi unachosha au thread yako ni ndefu inachosha? Kila mara utasikia au kusoma Huyu anaboa sana.
4.Ongeza misemo mingine uliyosikia au kusoma
.......................................................................
........................................................................

Kwenye rangi pale
Nahisi hapa umeenda tofauti. Tukisema kwa namna moja au nyingine hapa ni vitu viwili tu vinaongelewa. Moja au nyingine, vile vile huendana na Kwa hali na mali.

Pia hii inamaanisha kitu cha kwanza kinajulikana lakini cha pili hakijulikani. Nadhani hakuna kosa lolote!
 
Ila hiyo namba 2; tafsiri haijakaa vizuri (namna mbali mbali); ni bora ungesema kwa "kwa namna yoyote" kidogo hiyo yaweza kuwa karibu na sawa na hiyo "in one way or another".

Lkn pamoja na hayo mimi sioni shida sana kutafsiri Maneno kama!
4: sina machaguo .... I have no options
5: karibu na kutowezekana .... Next to impossible
6: kwani we ni nani.... Who do u think u r
7: nakukosa.... I miss u
Na kadhalika
4. Sina hakika kama umoja na wingi ni chaguo/machaguo. Kwa hali yoyote ile, I have no option(s) inasikika vizuri zaidi kama itasema "Sina budi"
6. Kwani wewe ni nani...Tungo tata kwani katika maudhui mengine jawabu ingekuwa "Mimi ni John", lakini kama ingekuwa "Unajiona/jihisi, unafikiri wewe ni nani, tafsiri yake ingekuwa hiyo "Who do you think you are".
7. Miss nahisi ni neno ambalo tunalilazimisha tu kulipa maana ya "kukosa" wakati hujamwona mtu kwa muda mrefu. Fikiria sentensi hizi:
a) We (will) miss you. b) We have missed you.
Nahisi neno "kukumbuka" ndio sahihi zaidi kwa maana ya a) Tuna/tuta-kukumbuka b) Tunakumbuka.

Tatizo letu ni kuwa mara nyingi hatukisemi/hatukizungumzi Kiswahili katika uhalisia, uasili wake bila ya kukilinganisha na Kiingereza. Ukitaka kusikia Kiswahili kizuri na sahihi, wasikilize wale ambao hawaelewi Kiingereza.
 
Labda ! Ila historia za lugha ni pana sana! kwanini useme ni tafsi ya moja kwa moja toka kingereza kwenda kiswahili na sio kiswahili kwenda kingereza. Pili, je madhara ya tafsiri ya moja kwa moja kwenye lugha nyingine maana yake na tatizo lake nini? Maana nikiangalia misemo yote hiyo, imebebwa katika matendo ya kijamii ndio maana inaishi! lugha bila matendo wala hisia inakufa! Lugha hajengwi tu hewani! kama tunaitumia kila siku na ikahimili uhalisia wetu, na ekaendelea kuwepo! Je itakuwa sio lugha yetu bado!
 
Habari zenu wanaJF? Naleta mbele yenu misemo miwili ya kiswahili inayotumika sana siku hizi lakini ni direct translation ya Kiingereza.Misemo hiyo na kiingereza chakei ni kama ifuatavyo:

1.Mwisho wa siku= Ni kiingereza cha: at the end of the day. Fungua tv au redio yako, kaa dakika tano tu hutaacha kusikia huu msemo wa mwisho wa siku. Kwanini tusiseme 'hatimaye' au 'baadaye?
2. Kwa namna moja au nyingine= Ni kiingereza cha: in one way or another.Hii sipendi kuisikia; inanipa kichefchef kwa sababu kama ni namna moja au nyingine, maana yake ni namna mbalimbali. Kwa nini hatusemi kwa namna mbalimbali?
3.Unaboa = Ni kiingereza cha you are boring. Hata hapa JF, hii inatumika sana.Kwa nini hatusemi unachosha au thread yako ni ndefu inachosha? Kila mara utasikia au kusoma Huyu anaboa sana.
4.Ongeza misemo mingine uliyosikia au kusoma
.......................................................................
........................................................................

Mimi kinachoniudhi kabisa ni ile hali tuliyonayo sasa ya kubadilisha majina ya vitu na mbadala wake tunatumia maelezo
mfano
Albino kwa Kiswahili sahihi ni Zeruzeru, lakini sasa wanaitwa watu wenye ulemavu wa ngozi, sasa ulemavu wa ngozi uko wa aina nyingi mno, uwezi kutoa neno moja Zeruzeru na mbadala wake kuweka maelezo

sasa Wanaliua neno KIPOVu na mbadala wake watatumia maelezo, mtu asiyeona au mtu mwenye matatizo ya kuona, hayo ni maelezo na wala sio jina, mtu asiyeona ni kipofu
 
4. Sina hakika kama umoja na wingi ni chaguo/machaguo. Kwa hali yoyote ile, I have no option(s) inasikika vizuri zaidi kama itasema "Sina budi"
6. Kwani wewe ni nani...Tungo tata kwani katika maudhui mengine jawabu ingekuwa "Mimi ni John", lakini kama ingekuwa "Unajiona/jihisi, unafikiri wewe ni nani, tafsiri yake ingekuwa hiyo "Who do you think you are".
7. Miss nahisi ni neno ambalo tunalilazimisha tu kulipa maana ya "kukosa" wakati hujamwona mtu kwa muda mrefu. Fikiria sentensi hizi:
a) We (will) miss you. b) We have missed you.
Nahisi neno "kukumbuka" ndio sahihi zaidi kwa maana ya a) Tuna/tuta-kukumbuka b) Tunakumbuka.

Tatizo letu ni kuwa mara nyingi hatukisemi/hatukizungumzi Kiswahili katika uhalisia, uasili wake bila ya kukilinganisha na Kiingereza. Ukitaka kusikia Kiswahili kizuri na sahihi, wasikilize wale ambao hawaelewi Kiingereza.

nieleweshe tafsiri ya "missed calls" ikiwa miss=kukumbuka!!
 
Habari zenu wanaJF? Naleta mbele yenu misemo miwili ya kiswahili inayotumika sana siku hizi lakini ni direct translation ya Kiingereza.Misemo hiyo na kiingereza chakei ni kama ifuatavyo:

1.Mwisho wa siku= Ni kiingereza cha: at the end of the day. Fungua tv au redio yako, kaa dakika tano tu hutaacha kusikia huu msemo wa mwisho wa siku. Kwanini tusiseme 'hatimaye' au 'baadaye?
2. Kwa namna moja au nyingine= Ni kiingereza cha: in one way or another.Hii sipendi kuisikia; inanipa kichefchef kwa sababu kama ni namna moja au nyingine, maana yake ni namna mbalimbali. Kwa nini hatusemi kwa namna mbalimbali?
3.Unaboa = Ni kiingereza cha you are boring. Hata hapa JF, hii inatumika sana.Kwa nini hatusemi unachosha au thread yako ni ndefu inachosha? Kila mara utasikia au kusoma Huyu anaboa sana.
4.Ongeza misemo mingine uliyosikia au kusoma
.......................................................................
........................................................................

Kuna "kitu " - sema kuna jambo
kuna vitu nataka nikwambie BADALA YA kuna mambo/masuala nataka nikwambie
 
Back
Top Bottom