SHIEKA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,244
- 4,258
Habari zenu wanaJF? Naleta mbele yenu misemo miwili ya kiswahili inayotumika sana siku hizi lakini ni direct translation ya Kiingereza.Misemo hiyo na kiingereza chakei ni kama ifuatavyo:
1.Mwisho wa siku= Ni kiingereza cha: at the end of the day. Fungua tv au redio yako, kaa dakika tano tu hutaacha kusikia huu msemo wa mwisho wa siku. Kwanini tusiseme 'hatimaye' au 'baadaye?
2. Kwa namna moja au nyingine= Ni kiingereza cha: in one way or another.Hii sipendi kuisikia; inanipa kichefchef kwa sababu kama ni namna moja au nyingine, maana yake ni namna mbalimbali. Kwa nini hatusemi kwa namna mbalimbali?
3.Unaboa = Ni kiingereza cha you are boring. Hata hapa JF, hii inatumika sana.Kwa nini hatusemi unachosha au thread yako ni ndefu inachosha? Kila mara utasikia au kusoma Huyu anaboa sana.
4.Ongeza misemo mingine uliyosikia au kusoma
.......................................................................
........................................................................
1.Mwisho wa siku= Ni kiingereza cha: at the end of the day. Fungua tv au redio yako, kaa dakika tano tu hutaacha kusikia huu msemo wa mwisho wa siku. Kwanini tusiseme 'hatimaye' au 'baadaye?
2. Kwa namna moja au nyingine= Ni kiingereza cha: in one way or another.Hii sipendi kuisikia; inanipa kichefchef kwa sababu kama ni namna moja au nyingine, maana yake ni namna mbalimbali. Kwa nini hatusemi kwa namna mbalimbali?
3.Unaboa = Ni kiingereza cha you are boring. Hata hapa JF, hii inatumika sana.Kwa nini hatusemi unachosha au thread yako ni ndefu inachosha? Kila mara utasikia au kusoma Huyu anaboa sana.
4.Ongeza misemo mingine uliyosikia au kusoma
.......................................................................
........................................................................