Kwa maoni yangu,yafuatayo ndiyo maneno maarufu kwenye Vyuo Vikuu vyetu hapa Tanzania:
1.'Boom'(fedha za kujikimu zitolewazo na Bodi ya Mikopo ya Elimu Ya Juu kwa wanachuo/wanafunzi)
2. 'Kuuza chai'(Kupiga stori hasa za kuchekesha/au sizizo za kweli)
3.'Nyanga'(Supplementary exams)
4.Kutiwa nyavuni/kukamatwa(kufeli somo hivyo kutakiwa kulirudia)
5.Nondo(vitu visivyoruhusiwa mtihanini lakini vinavyoingizwa kimagendo)
6.Exile(kumpisha mwanachumba mwenzako 'atumie' chumba pekeyake kwa muda fulani
7.'Kupiga Dash'(kushinda bila kula kwasababu ya kuishiwa fedha za kujikimu)
8.Kipanga(mwanafunzi anayejiweza darasani kwa kuelewa haraka au kutosahau haraka)
9.Kilaza(mwanafunzi ambaye uelewa wake ni wa mashaka/haelewi mapema na hachelewi kusahau)
10.'Ungwini'(Masomo ambayo hayaambatani na mahesabu)
11.'Kudesa'(kuiga kwa mwanafunzi mwingine au kuandika kitu kama kilivyokutwa mahali fulani au kwa mtu fulani)
12.'Desa'/'Madesa'(Kitabu/Vitabu visivyo rasmi
Wana JF tuendelee...
Kulishwa matango pori....kufundishwa majibu ya uongo-off topic!!
September conference-----kurudi kufanya sap mwezi wa tisa!!
Swadakta!!Kulishwa matango pori au Kulishwa "Kasa"
Swadakta!!
Unakuta mtu kameza madesa yake alafu anawakusanya wenzie pale mdigrii au kwenye vimbweta na kuanza kuwalisha wenzie kasa/matango pori mpaka atokee anayejua topic hapo mda ushaenda sana!!!
Dah no 6 hiyo exile inakuwaga kwa madhumuni gani?
Fafanua...