Mirathi hii igawanywe vipi?

KAPONGO

JF-Expert Member
May 29, 2009
1,661
668
Bwana Omar (jina la kupanga) amefiwa na mkewe mwezi uliopita. Alimwoa kwa mila na taratibu za kiislam baada ya kumbadilisha dini, kutoa ukristo kuwa muislam, na kabla hajamwoa mke huyo alishawahi kuzaa mtoto wa kiume na Mtu mwingine. Marehemu amemwachia watoto wawili waliozaliwa katika ndoa, na wazazi wote wawili wa marehemu mke wake bado ni hai na ni wakristo. Sasa ikiwa marehemu ameacha amana ya kiasi cha shilingi 600,000/= Je mirathi hiyo igawanywe vipi kwa mujibu wa sheria za mirathi ya dini ya kiislamu? Plse only knowledgable should contribute
 
Bwana Omar (jina la kupanga) amefiwa na mkewe (1) mwezi uliopita. Alimwoa kwa mila na taratibu za kiislam baada ya kumbadilisha dini, kutoa ukristo kuwa muislam, na kabla hajamwoa mke huyo alishawahi kuzaa mtoto wa kiume na Mtu mwingine (2). Marehemu amemwachia watoto wawili waliozaliwa katika ndoa (3), na wazazi wote wawili wa marehemu mke wake bado ni hai na ni wakristo (4) . Sasa ikiwa marehemu ameacha amana ya kiasi cha shilingi 600,000/= Je mirathi hiyo igawanywe vipi kwa mujibu wa sheria za mirathi ya dini ya kiislamu? Plse only knowledgable should contribute

Kapongo, hii habari yako, uoni kwamba inajichanganya kwenye maelezo?
 
Kapongo, hii habari yako, uoni kwamba inajichanganya kwenye maelezo?
, Najichanganya! Ngoja nikurahisishie: Huyo jamaa ni muislamu na alimwoa binti wa kikristo kwa sheria za kiislamu baada ya kumsilimisha. Lakini kabla ya kumwoa binti huyo alishazaa na mtu mwingine mtoto mmoja wa kiume ambaye hadi sasa ni mkristo (dini ya awali ya mama yake). Jamaa alibahatika kuzaa naye mke wake huyo watoto wawili(ambao wote ni waislamu km wazazi wao). Na kwamba baba na mama wa mke wake huyo ni wakristo. Sasa kama marehemu ameacha kiasi hicho, mirathi yake igawanywe vipi kwa kuzingatia sheria ya dini ya kiislam ambayo mume na mke ni waumini wake?.
.. issue at context: mf. mtoto ambaye si mwislamu ananufaikaje na mirathi ya mzazi wake ambaye ni mwislamu, wazazi ambao si waislamu nao haki yao ikoje mbele ya sheria hizo?.
 
, Najichanganya! Ngoja nikurahisishie: Huyo jamaa ni muislamu na alimwoa binti wa kikristo kwa sheria za kiislamu baada ya kumsilimisha. Lakini kabla ya kumwoa binti huyo alishazaa na mtu mwingine mtoto mmoja wa kiume ambaye hadi sasa ni mkristo (dini ya awali ya mama yake). Jamaa alibahatika kuzaa naye mke wake huyo watoto wawili(ambao wote ni waislamu km wazazi wao). Na kwamba baba na mama wa mke wake huyo ni wakristo. Sasa kama marehemu ameacha kiasi hicho, mirathi yake igawanywe vipi kwa kuzingatia sheria ya dini ya kiislam ambayo mume na mke ni waumini wake?.
.. issue at context: mf. mtoto ambaye si mwislamu ananufaikaje na mirathi ya mzazi wake ambaye ni mwislamu, wazazi ambao si waislamu nao haki yao ikoje mbele ya sheria hizo?.
Ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipatia fursa hii ya kujibu swali lako.

Kuna maelekezo kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusiana na swali lako, amesema katika Hadithi iliyosimuliwa na Abdullah bin Amri (r.a) kuwa: Watu wa dini mbili tofauti hawatarithiana
(Abu Dauwd, Ibn Majah, Tirmidh).

Hivyo, ni wazi kuwa Muislamu hawezi kumrithi asiyekuwa Muislamu na kinyume chake pia. Kwa hivyo, ikiwa yule mzazi aliyekuwa ni Muislamu ndiyo aliyeaga dunia basi huyo kijana aliyekuwa si Muislamu hatamrithi mama yake kwa kuwa dini zao ni tofauti. Huyo mtoto atarithi tu ikiwa umri wake ni chini ya barekh, yaani bado kimawazo na kiuwezo (kiuwamuzi ambao kiserikali ni miaka 18 au 21 kwa nchi zingine), hapo atarithi. Lakini ikiwa mtoto ni mkubwa na ana uwezo wa kujitegemea, basi hatarithi na hata kama mtoto ndie aliyetangulia kufariki na umri wake ni mkubwa kwa maana anajitegemea na wazazi wake ni Waislam kinyume na imani ya mtoto wao nao hawatarithi.

Vile vile mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa hana haki ya kumrithi baba aliyemzaa na baba hana haki katika mirathi yake. Mtoto atarithi kwa mama yake tu, na mama atarithi kwa mtoto wake.

Zingatia:
Lakini ikiwa Mzazi/Mtoto Muislamu ameacha wasia na amemtunukia kitu mfano baadhi ya mali, basi atapewa bila ya wasiwasi wowote, lakini hizo mali za usia hazitakiwi kuzidi zaidi ya theruthi moja (1/3).

Kwa ufupi ni kuwa Muislamu hamrithi hasiyekuwa Muislam mfano: Mkristo au Myahudi au Baniani na wao hawatamrithi Muislamu hata akiwa karibu naye kiasi gani katika nasaba.

Mirathi itakwenda kwa Wale watoto wake wawili na kiasi kidogo atarithi mume wake. Lakini kuangaliwa hapa kama mtoto bado mdogo, si barekh kwa maana yupo chini ya uangalizi wa mama yake au alikuwa chini ya uangalizi wake, huyu atarithi pamoja na nduguze wa mama mmoja.


Cha kuzingatiwa kabla ya kugawanywa kwa mirathi zitolewe pesa za maziko na madeni aliyonayo marehemu, pamoja na kutimiza usia wa marehemu.


May Allah guide you and set your affairs right.

Allahu A’lam
 
Bwana Omar (jina la kupanga) amefiwa na mkewe mwezi uliopita. Alimwoa kwa mila na taratibu za kiislam baada ya kumbadilisha dini, kutoa ukristo kuwa muislam, na kabla hajamwoa mke huyo alishawahi kuzaa mtoto wa kiume na Mtu mwingine. Marehemu amemwachia watoto wawili waliozaliwa katika ndoa, na wazazi wote wawili wa marehemu mke wake bado ni hai na ni wakristo. Sasa ikiwa marehemu ameacha amana ya kiasi cha shilingi 600,000/= Je mirathi hiyo igawanywe vipi kwa mujibu wa sheria za mirathi ya dini ya kiislamu? Plse only knowledgable should contribute
Rejea sura ya 4 annisaa aya 12
Mume anapata robo ya hiyo amana na watoto 2 watagawana kutokana na jinsia zao, kama ni wanaume au wanawake nusu kwa nusu, kama mume na mke, itakuwa 2/1. Yule ambae si muislam hatapata kitu.
 
Ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipatia fursa hii ya kujibu swali lako.

Kuna maelekezo kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusiana na swali lako, amesema katika Hadithi iliyosimuliwa na Abdullah bin Amri (r.a) kuwa: Watu wa dini mbili tofauti hawatarithiana
(Abu Dauwd, Ibn Majah, Tirmidh).

Hivyo, ni wazi kuwa Muislamu hawezi kumrithi asiyekuwa Muislamu na kinyume chake pia. Kwa hivyo, ikiwa yule mzazi aliyekuwa ni Muislamu ndiyo aliyeaga dunia basi huyo kijana aliyekuwa si Muislamu hatamrithi mama yake kwa kuwa dini zao ni tofauti. Huyo mtoto atarithi tu ikiwa umri wake ni chini ya barekh, yaani bado kimawazo na kiuwezo (kiuwamuzi ambao kiserikali ni miaka 18 au 21 kwa nchi zingine), hapo atarithi. Lakini ikiwa mtoto ni mkubwa na ana uwezo wa kujitegemea, basi hatarithi na hata kama mtoto ndie aliyetangulia kufariki na umri wake ni mkubwa kwa maana anajitegemea na wazazi wake ni Waislam kinyume na imani ya mtoto wao nao hawatarithi.

Vile vile mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa hana haki ya kumrithi baba aliyemzaa na baba hana haki katika mirathi yake. Mtoto atarithi kwa mama yake tu, na mama atarithi kwa mtoto wake.

Zingatia:
Lakini ikiwa Mzazi/Mtoto Muislamu ameacha wasia na amemtunukia kitu mfano baadhi ya mali, basi atapewa bila ya wasiwasi wowote, lakini hizo mali za usia hazitakiwi kuzidi zaidi ya theruthi moja (1/3).

Kwa ufupi ni kuwa Muislamu hamrithi hasiyekuwa Muislam mfano: Mkristo au Myahudi au Baniani na wao hawatamrithi Muislamu hata akiwa karibu naye kiasi gani katika nasaba.

Mirathi itakwenda kwa Wale watoto wake wawili na kiasi kidogo atarithi mume wake. Lakini kuangaliwa hapa kama mtoto bado mdogo, si barekh kwa maana yupo chini ya uangalizi wa mama yake au alikuwa chini ya uangalizi wake, huyu atarithi pamoja na nduguze wa mama mmoja.


Cha kuzingatiwa kabla ya kugawanywa kwa mirathi zitolewe pesa za maziko na madeni aliyonayo marehemu, pamoja na kutimiza usia wa marehemu.


May Allah guide you and set your affairs right.

Allahu A'lam

JF ina ma-THINK TANK wa kutosha kila idara, respect kwako
 
Kwa swala la mirathi hilo ni halali kwa watoto wa ndani ya ndoa.

Kwa swala lako hao watoto wawili ndio watakuwa warithi lakini hizo mali zitakuwa chini ya uangalizi wa mama yao mapaka wafikishe miaka 18.

Na maelezo ya X-pastor yamejitosheleza kwa upande wa dini na hapo mtoto wa kiume ndio atapata gawio kubwa!
 
Back
Top Bottom