The Khoisan
Platinum Member
- Jun 5, 2007
- 18,224
- 17,377
Miradi ya barabara kibao imekamilika bongo
Na Mwandishi Maalum,
MIRADI 15 mikubwa ya ujenzi wa barabara nchini imekamilishwa katika miaka mitatu iliyopita na miradi mingine 33 iko kwenye hatua mbali mbali za kukamilishwa katika jitihada kubwa za kuboresha mawasiliano ya barabara nchini.
Kati ya miradi hiyo 15, barabara saba zenye urefu wa kilomita 441 na zilizogharimu kiasi cha sh bilioni 161.2 tayari zimefunguliwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Miradi mingine minane yenye urefu wa kilomita 370.95 na iliyogharimu kiasi cha sh bilioni 135.16 tayari imekamilika na inasubiri kufunguliwa na Rais Kikwete.
Hayo ni baadhi ya maelezo ambayo Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Ephraim Mrema alimpa Rais Kikwete mwishoni mwa wiki wakati wa mkutano wa kutathimini utendaji wa Serikali, Wizara na mashirika yaliyoko chini ya Wizara uliofanyika Ikulu, Dar Es Salaam, Ijumaa, Januari 16, 2009.
Katika mkutano huo uliohusu Wizara ya Miundombinu na mashirika yake, Mrema alimwambia Rais Kikwete kuwa miradi mingine ya barabara yenye urefu wa 2, 706.81 yenye kugarimu sh bilioni 1, 165.29 inaendelea kujengwa katika sehemu mbali mbali za nchi.
Alisema kuwa mchakato wa kwanza utekelezaji wa miradi mingine mitano mikubwa umekamilika na unasibiri kutiwa saini, mingine 18 iko kwenye hatua ya manunuzi, mingine 23 iko kwenye hatua ya maandalizi ya usanifu.
Alisema kuwa usanifu wa miradi mingine 11 umekamilika lakini bado fedha za ujenzi wa barabara hizo zinaendelea kutafutwa na Serikali.
Mrema alisema kuwa miradi saba iliyokamilishwa na kufunguliwa na Rais Kikwete katika miaka mitatu iliyopita ni Buzirayombo-Geita, Issuna-Singida, Singida-Iguguno, Iguguno-Sekenke, Sekenke-Shelui, Tinde-Mwanza/Shinyanga Border na Nzega-Tinde-Isaka. Barabara hizo zote zimejengwa kwa kiwango cha lami.
Kati ya miradi hiyo, miwili imegharimiwa na Serikali ya Tanzania (GOT), mwili imegharimiwa na Jumuia ya Ulaya (EU) na mitatu imegharimiwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia (WB).
Mrema alisema kuwa miradi minane ambayo imekamilika na inasubiri kufunguliwa na Rais ni Kyamyorwa-Buziyarombo, Mbwemkulu-Mingoyo, Sam Nujoma Road, Daraja la Ruvu, Tarakea-Rongai-Kamwanga, Kidahwe-Uvinza, Kisili-Buhigwe, na Uvinza-Malagasi.
Kati ya miradi hiyo, mitano imejengwa kwa kiwango cha lami na mitatu imejengwa kwa kiwango cha changarawe na kati ya yote, mitano imegharimiwa na Serikali ya Tanzania, na mitatu ya kiwango cha lami imegharimiwa na Shirika la Mafuta Duniani (OPEC).
Mrema alisema kuwa miradi 33 ambayo ujenzi wake unaendelea ni Geita-Sengerema, Manyoni Isuna, Sengerema-Usagara, Mwandiga-Manyovu, Kagoma-Kidahwe, Ndundu-Somanga, Dodoma-Manyoni, Naguruku-Mbwemkulu, Bagamoyo-Msata, na Mbeya-Lwanjilo ambayo yote inagharimiwa na Serikali ya Tanzania.
Mingine ni Arusha-Mananga unaogharimiwa na Banki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Kilwa Road Phase Two inayogharimiwa kwa pamoja na GOT na shirika la JICA la Japan, Chalinze-Tanga Phase One unaogharimiwa na Tanzam Highway (Iyoyi) inayogharimiwa na DANIDA, Marangu-Rombo Mkuu unaogharimiwa na NORAD, Daraja la Unity Bridge linalogharimiwa na GOT na Serikali ya Mozambique, na Nelson Mandela unaogharimiwa na EU.
Mrema aliitaja miradi mingine kama Tingi-Kipatimu, Nanganga-Ruangwa, Nachingwe-Kilimarondo, na Nachingwe-Liwale ambayo yote inagharimiwa na OPEC na inajengwa kwa kiwango cha changarawe.
Miradi mingine ni miradi mingine ni miradi miwili ya kuboresha mwasiliano Mkoani Rukwa na mingine miwili ya Jiji la Mwanza ambayo yote inagharimiwa na GOT na Wakala wa Maendeleo wa Kimataifa (IDA), Masasi-Mangaka Phase One, Masasi-Mangaka Phase Two ambayo inagharimiwa na GOT kwa kushirikiana na JICA, Rombo Mkuu-Tarakea unaogharimiriwa na BADEA, barabara mbali mbali za mikoa mbali mbali yenye urefu wa kilomita 497 na inayogharimiwa na DANIDA.
Mrema aliitaja miradi mingine kuwa ni Kidatu-Ifakara, Singida-Katesh, Katesh-Dareda, na Dareda-Minjingu.
Mrema alisema kuwa miradi mikubwa ambayo inasubiri kutiwa saini ili utekelezaji uanze ni Same-Mkumbara, Mkumbara-Korogwe, Kigoma Lusahunga na ujenzi wa barabara za Tanga mjini.
Alisema kuwa miradi iliyoko katika hatua ya manunuzi ni Tabora-Nyahua, Mkata-Handeni, Korogwe-Handeni, Handeni-Mziha, Mwigumbi-Maswa-Bariadi-Lamadi Bariadi-Lamadi, Dodoma-Babati, Sumbawanga-Mpanda, Sumbawnga-Kanazi, Sumbwanga-Mpanda-Kanazi-Kizi-Kibaoni, Kyaka-Kayanga-Bugene, Sumbawanga-Matai-Kasesya, Barabrara za Kuzungumza Mkoa wa Dar es Salaam (ring roads) ambao ni mradi maalum, na Kitumbi, Segera-Tanga.
Mingine ni Tunduma-Laela-Sumbawanga, Tunduma-Kana, Tanga-Horohoro, Songea Mbinda, Songea-Namtumbo ambayo yote itagharimiwa chini ya msaada wa MCC wa Serikali ya Marekani.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
Na Mwandishi Maalum,
MIRADI 15 mikubwa ya ujenzi wa barabara nchini imekamilishwa katika miaka mitatu iliyopita na miradi mingine 33 iko kwenye hatua mbali mbali za kukamilishwa katika jitihada kubwa za kuboresha mawasiliano ya barabara nchini.
Kati ya miradi hiyo 15, barabara saba zenye urefu wa kilomita 441 na zilizogharimu kiasi cha sh bilioni 161.2 tayari zimefunguliwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Miradi mingine minane yenye urefu wa kilomita 370.95 na iliyogharimu kiasi cha sh bilioni 135.16 tayari imekamilika na inasubiri kufunguliwa na Rais Kikwete.
Hayo ni baadhi ya maelezo ambayo Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Ephraim Mrema alimpa Rais Kikwete mwishoni mwa wiki wakati wa mkutano wa kutathimini utendaji wa Serikali, Wizara na mashirika yaliyoko chini ya Wizara uliofanyika Ikulu, Dar Es Salaam, Ijumaa, Januari 16, 2009.
Katika mkutano huo uliohusu Wizara ya Miundombinu na mashirika yake, Mrema alimwambia Rais Kikwete kuwa miradi mingine ya barabara yenye urefu wa 2, 706.81 yenye kugarimu sh bilioni 1, 165.29 inaendelea kujengwa katika sehemu mbali mbali za nchi.
Alisema kuwa mchakato wa kwanza utekelezaji wa miradi mingine mitano mikubwa umekamilika na unasibiri kutiwa saini, mingine 18 iko kwenye hatua ya manunuzi, mingine 23 iko kwenye hatua ya maandalizi ya usanifu.
Alisema kuwa usanifu wa miradi mingine 11 umekamilika lakini bado fedha za ujenzi wa barabara hizo zinaendelea kutafutwa na Serikali.
Mrema alisema kuwa miradi saba iliyokamilishwa na kufunguliwa na Rais Kikwete katika miaka mitatu iliyopita ni Buzirayombo-Geita, Issuna-Singida, Singida-Iguguno, Iguguno-Sekenke, Sekenke-Shelui, Tinde-Mwanza/Shinyanga Border na Nzega-Tinde-Isaka. Barabara hizo zote zimejengwa kwa kiwango cha lami.
Kati ya miradi hiyo, miwili imegharimiwa na Serikali ya Tanzania (GOT), mwili imegharimiwa na Jumuia ya Ulaya (EU) na mitatu imegharimiwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia (WB).
Mrema alisema kuwa miradi minane ambayo imekamilika na inasubiri kufunguliwa na Rais ni Kyamyorwa-Buziyarombo, Mbwemkulu-Mingoyo, Sam Nujoma Road, Daraja la Ruvu, Tarakea-Rongai-Kamwanga, Kidahwe-Uvinza, Kisili-Buhigwe, na Uvinza-Malagasi.
Kati ya miradi hiyo, mitano imejengwa kwa kiwango cha lami na mitatu imejengwa kwa kiwango cha changarawe na kati ya yote, mitano imegharimiwa na Serikali ya Tanzania, na mitatu ya kiwango cha lami imegharimiwa na Shirika la Mafuta Duniani (OPEC).
Mrema alisema kuwa miradi 33 ambayo ujenzi wake unaendelea ni Geita-Sengerema, Manyoni Isuna, Sengerema-Usagara, Mwandiga-Manyovu, Kagoma-Kidahwe, Ndundu-Somanga, Dodoma-Manyoni, Naguruku-Mbwemkulu, Bagamoyo-Msata, na Mbeya-Lwanjilo ambayo yote inagharimiwa na Serikali ya Tanzania.
Mingine ni Arusha-Mananga unaogharimiwa na Banki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Kilwa Road Phase Two inayogharimiwa kwa pamoja na GOT na shirika la JICA la Japan, Chalinze-Tanga Phase One unaogharimiwa na Tanzam Highway (Iyoyi) inayogharimiwa na DANIDA, Marangu-Rombo Mkuu unaogharimiwa na NORAD, Daraja la Unity Bridge linalogharimiwa na GOT na Serikali ya Mozambique, na Nelson Mandela unaogharimiwa na EU.
Mrema aliitaja miradi mingine kama Tingi-Kipatimu, Nanganga-Ruangwa, Nachingwe-Kilimarondo, na Nachingwe-Liwale ambayo yote inagharimiwa na OPEC na inajengwa kwa kiwango cha changarawe.
Miradi mingine ni miradi mingine ni miradi miwili ya kuboresha mwasiliano Mkoani Rukwa na mingine miwili ya Jiji la Mwanza ambayo yote inagharimiwa na GOT na Wakala wa Maendeleo wa Kimataifa (IDA), Masasi-Mangaka Phase One, Masasi-Mangaka Phase Two ambayo inagharimiwa na GOT kwa kushirikiana na JICA, Rombo Mkuu-Tarakea unaogharimiriwa na BADEA, barabara mbali mbali za mikoa mbali mbali yenye urefu wa kilomita 497 na inayogharimiwa na DANIDA.
Mrema aliitaja miradi mingine kuwa ni Kidatu-Ifakara, Singida-Katesh, Katesh-Dareda, na Dareda-Minjingu.
Mrema alisema kuwa miradi mikubwa ambayo inasubiri kutiwa saini ili utekelezaji uanze ni Same-Mkumbara, Mkumbara-Korogwe, Kigoma Lusahunga na ujenzi wa barabara za Tanga mjini.
Alisema kuwa miradi iliyoko katika hatua ya manunuzi ni Tabora-Nyahua, Mkata-Handeni, Korogwe-Handeni, Handeni-Mziha, Mwigumbi-Maswa-Bariadi-Lamadi Bariadi-Lamadi, Dodoma-Babati, Sumbawanga-Mpanda, Sumbawnga-Kanazi, Sumbwanga-Mpanda-Kanazi-Kizi-Kibaoni, Kyaka-Kayanga-Bugene, Sumbawanga-Matai-Kasesya, Barabrara za Kuzungumza Mkoa wa Dar es Salaam (ring roads) ambao ni mradi maalum, na Kitumbi, Segera-Tanga.
Mingine ni Tunduma-Laela-Sumbawanga, Tunduma-Kana, Tanga-Horohoro, Songea Mbinda, Songea-Namtumbo ambayo yote itagharimiwa chini ya msaada wa MCC wa Serikali ya Marekani.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.