Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,730
- 536
Miradi ya barabara kibao imekamilika bongo
Mrema alisema kuwa miradi minane ambayo imekamilika na inasubiri kufunguliwa na Rais ni Kyamyorwa-Buziyarombo, Mbwemkulu-Mingoyo, Sam Nujoma Road, Daraja la Ruvu, Tarakea-Rongai-Kamwanga, Kidahwe-Uvinza, Kisili-Buhigwe, na Uvinza-Malagasi.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM
Sijaangalia vitu vingine, lakini hiyo ya rangi nyekundu sio ya lami.....au ni mchanganyiko wa lami na changarawe?
Asante Roy kwa kushitukia huo usanii kuhusu hizo barabara, mimi nimeongezea moja ya bluu.
Inaonekana Rais wetu huwa anadanganywa mno na Watendaji wake. Hizo barabara ni mbovu kuliko na zimekuwa hivyo tangu enzi za Adamu na Eva!
Kinachoshangaza zaidi ni kauli kuwa haitajwi ni kiwango cha changarawe au lami ila tunaambiwa zimekamilika. Mimi nadhani ni vema Rais awe mjanja na ajitolee kufunguamwenyewe hizo barabara ili ajionee mauza-uza ya Serikali yake.