MIPANGO NA MUME MTARAJIWA

MIPANGO NA MUME MTARAJIWA

Mwambie next week waanze kuweka msingi,hayo mahusiano hayafiki mbali yatakula mweleka na atabakiwa na faida ya nyumba.
 
Hakuna mume wala ndoa hapo, mwambie rafiki yako STUKA! Mwambie rafiki yako aje kuusoma huu uzi 😜😜😜

Habari zenu wanajamvi, nina rafiki yangu ana boyfrend wake, hawajafika stage yyte ya ndoa ndio wana mpango wa kutambulishana hivi karibuni ila kinachomtatiza bi dada ni mipango ya huyu kijana, ameng'ang'ania wajenge nyumba yao katika kiwanja kinachomilikiwa na bi dada.

Sasa kinachomtatiza bi dada mbona kung'ang'ania kujenga ktk kiwnja chake?

Kujenga ni jukumu la mwanaume, mbona bwana huyu ana ng'ang'ania wajenge wote?

Huyu Kijana kutwa kucha kwenda kula dinner kwa bi dada na hachangii chochote hata wakienda shoping hatoi hata sh10 kuchangia.

Kijana ana gari yake, ila kutwa kucha anapenda kuendesha gari ya bi dada kisa ni nzuri na hachangii hata mafuta.

Wenye experience nahii naombeni maoni yenu.
 
Hivi ungejisemea kwa nafsi yako ungepungukiwa na nini?

Next jaribu pia kupunguza chumvi sawa we mtoo...
 
Kama hatoi sh 10 hyo nyumba atashiriki vip kujenga huyo tapeli tu aachane nae tu...wanaume husema piga chini
 
Dooh!! Nna beach plot Ila kabla hatujaanza kujenga ntakuhonga ka I S T [emoji23]
Tehteh...ila nyie wanawake ni wagumu bwana....

Hata mwanamke akiwa anatoa pesa kwa ATM huwa anaichungulia.
 
Kwani kazi za ndani tunafanya wote?
Kujenga sio jukumu la mwanaume...kama mmefunga ndoa ni jukumu la wote wawili. Wanawake tusipende vya wanaume..ni jukumu la wote. Ila kwa wao sina la kuwashauri zaidi ya kumwambia akili kichwani
 
Back
Top Bottom