UKOLONI UKOLONI! jamani mnashindania HISTORIA. NCHI ikishapata UHURU na kuvunja minyororo ya wakoloni hakuna mkataba unaoabudiwa wala kufuatwa wa makoloni ya zamani. Huu USULTANI unaoutetea hauna tija tena! Unachotakiwa kukiangalia wewe na Wazenj wenzio ni kukaa meza moja na Tanganyika mukaona namna ya kuvunja au kuimarisha muungano. Hayo madai ya kikoloni yatakuharibieni kila kitu. Hamtapata Zenji wala tone la ardhi ya Coast mnayodai. Tafuteni Haki kistaarabu. Wewe kama unadai mali yako kwa jirani yako unadai hata ile mali yake halali UTAKOSA VYOTE!!!Jerrytz,
Si afrika yote laki east afrika yote kuanzia somalia hadi msumbizi ilikuwa zanzibar. yaani zenj empire.
Hili neno Mozambique unajuwa nini? ni Mussa Bin Mbek, walipokuja wareno walimkuta yeye ndie gavana pale wa zazniabr. hawakuweza kulitamka jina lake na wakawa wanamwita mussambek ikawa Mozambique hii kama ujuwayo wewe.
Kadhi wa Kwanza wa zanziabr 1832 alitokea somalia ya leo, Sheikh Muhidin Bin Abdullah Al Qahtan, kwasababu somalia ilikuwa ni part of zenj empire wakati huo. Ndio maana haikuwa noma kuweka mtu wa huko katika sehemu nyeti kabisa katika uwongzi wa dola ya zanzibar.
Kuhusu zanzibar kuonewa na tanganyika hilo halitaki darubini, mara ngapi nyinyi watanganyika munapeleka jesho lenu kutuuwa kule pemba, kwa kutumia kichaka cha uchaguzi wa siasa.....
ahsante
Android 00
nyaraka zipo za kodi
fukwe za tanganyika zilikodishwa kwa mjerumani na zitarudi znz
hilo halina shaka yoyote
nakushauri uunde jeshi lenu la ukombozi mje mkachukue ardhi yenu mnayoidai Tanganyika. Tutawasubiri.Mangikule
Nadhani hata muungano wa nyerere na karume ni historia na karibu vitabu vitabadilishwa.
Haki kistaarabu haipatikani....Mzee Karume alipowakataa kuwapokea mawaziri aloletewa na Nyerere kuwapandikiza katika SMZ na aliposema koti likianza kutubana tutalivua akauliwa, Jumbe alipojaribu kuvunja muungano akauzuliwa madarakani na kuwekwa kizuizini tanganyika, uamsho walipojaribu kuwaamsha wazanzibari wamewekwa kizuizini.....sasa nakuomba uwashauru wazanzibari wafanye ustaarabu gani ili mtanganyika aitowe ndoana katika koo ya zanzibar?
wewe utauita usultan, mimi naiita serkali ya Zanzibar.
Nipe sababu moja tu ya kisheria itakayoiwezesha Tanganyika kuiiba sehemu ya Zanzibar iliopo mipakani mwake, yaani maeneo ya pwani ya tanganyika?
Waungwana
Hii ndio ilyokuwa mipaka ya zanzibar katika awamu mbali mbali
hapa munaona ukubwa wake![]()
Tanzanzia kushneii.. Ndo bas tena mizozo imeanza bado vita sasa tuwapishe wenye akili wachote rasilimali ..
nnguo007
tuseme ndio huujui ukweli au ndio unaonesha utanganyika wako tu
Historia ya Zanzibar inaonekana kuanzia 600s AD.
Mreno alipofika Msumbiji walimkuta gavana wa zanzibar pale aitwae Mussa Bin Mbek wao wakawa hawawezi kulitamka vyema jina lake ndio wakawa wanamwita mussabek ikawa Mozambique.
Na hichi kitabu ulichokinuu kimeandikwa na John Okelo au nani?
Kama unajuwa historia ninataka utuambie safaru ya Tanganyika kabla hii![]()
Heller ya Deutsch Ost Afrika
Ninaomba uniambie mtawala wa Tanganyika kabla ya kuja kwa Mjerumani?
Lete ushahidi kamili hapa
Ahsante