Miongo ya uongozi, hatua mpya ya taifa ya Deogratius Ndejembi

Miongo ya uongozi, hatua mpya ya taifa ya Deogratius Ndejembi

Zack Abdul

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2026
Posts
731
Reaction score
658
Kila safari ya uongozi huanza na hatua moja na kwa Deogratius John Ndejembi, hatua hiyo imejengwa kwa miaka ya uzoefu, utumishi na majukumu mbalimbali katika uongozi wa umma.

Kutoka katika ngazi za Serikali za Mitaa, hadi uongozi wa Wilaya, Bunge na Serikali Kuu Ndejembi amepitia katika nafasi zilizompa fursa ya kukutana moja kwa moja na changamoto, matarajio na mahitaji ya Watanzania.

Ni safari iliyompeleka kutoka Chamwino, Dodoma… hadi kwenye majukumu ya kitaifa,
akiwa na taaluma ya International Relations kutoka University of Lincoln nchini Uingereza, pamoja na uzoefu katika utawala na uongozi, ameshika nafasi mbalimbali serikalini, ikiwemo Naibu Waziri na Waziri katika wizara tofauti.

Soma Pia: Deogratius Ndejembi ateuliwa kuwa Makamu wa Rais

Lakini sasa, safari hiyo imefika kwenye ukurasa mwingine.

Mteule wa nafasi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ….Deogratius John Ndejembi.

Kutoka kwenye uongozi wa wananchi… hadi kwenye jukumu linalogusa taifa zima.

#TanzaniaYetu
IMG-20260828-WA0054.jpg
 
Back
Top Bottom