Mimi ni mvivu kweli, naombeni ushauri

Mimi ni mvivu kweli, naombeni ushauri

hali hio hata mi ninayo na imeniathiri kwa sababu ni last born ila kuhusu time nimejifunza kama natakiwa kufika sehemu saa 2 nitajitahidi niweke alam ya saa kumi na mbili kasoro itani disturb alarm mpaka saa moja kasoro nitaamka na nitawahi niendako kuhusu kuvaa nguo na kuvaa nina tatizo hilo pia so huwa naaandaa jana yake kabisaa baada ya kuridhika na chaguo lake hii inasaidia kuokoa muda
 
wale masalia wa udom naombeni mkae pembeni maana sitaki maneno yenu naongea na watu wazima wenzangu!

wadau nin shida moja katika maisha yangu mimi ni mvivu halafu huwa natake easy kila kitu kitu ambacho kinanisababishia hasara nyingi maishani.
kuhusu darasani nina akili za kutosha toka primary top ten ilikuwa hainikosi hata chuo sikuwa kupata supp hata kuna wakati somo moja lililamba robo tatu ya darasa tena nilikuwa nimelazwa nikatoka hosptal asubuhi nikaingia saa tisa kwenye paper nikapata zangu B. niliosoma nao humu wanaweza kunikumbuka.
sasa tatizo linakuja kwenye maisha mimi ni mvivu kuamka nitashtuka tu saa kumi na moja najiongeza kidogo kidogo hadi inafika saa moja najiandaa kivivuvivu hivo hivo mara nivae nguo hii mara nione sijapendeza nivue hadi saa mbili natoka nduki kwenda job maana sio mbali kwahiyo hapo naacha chumba kikiwa rafu maana muda wa kupanga na kutandika kitanda unakuwa hamna. hadi nirudi jioni.

nikialikwa kwenye party najiandaa kivivu hadi wakati mwingine naacha tu maana muda unakuwa hamna tena sherehe imeisha
nikienda benk sihesabu hela jana nimeibiwa elf 10 duka la kubadilishia fedha maana sikuhesabu kwenye daladala nilipewa hela feki hivihivi maana hata sikuangalia.
naombeni ushauri nifanyeje maana mimi mtu mzima naitaji kuwa na familia na kuwa mama bora.ndo maana nilitamani kuadopt mtoto ili niwe busy nae haya maisha ya kuishi peke yangu yananilemaza jamani nifanyeje? natamani kuwa active . hapa nimeandika hivi nimechoka kweli yaani
Afu wewe tafuta kuku mweupe niinbox nitakupa namba za mtaalamu, utapiga kaZi kama mfanyakazi wa muhindi
 
Back
Top Bottom