Mimi ni Belinda, sikitiko langu mwenyewe!

Mimi ni Belinda, sikitiko langu mwenyewe!

Poker

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2016
Posts
6,534
Reaction score
19,089
Mimi ni Belinda Wagiri, nilizaliwa yapata miaka 40 iliopita huko kidabaga njombe, wakati huo Iringa. Ni mtoto wa mwisho kwa mzee Wagiri na kikabila mimi ni mhehe. Elimu yangu ya msingi niliipata huko huko kidabaga ila sikumaliza nilikatisha masomo yangu baada ya baba kurehemika. Nilikaa kwa muda kidogo kabla yakutafutiwa kazi za ndani huko Dar es salaam. Ndio ilikuwa mara yangu kufika dar kulikuwa kumepoa sana maeneo mengi yalikuwa bado mapori, nakumbuka hata barabara nyingi zilikuwa bado ni vumbi. Nilipofika dar nilipokelewa na mwenyeji wangu ambae nilikaa kwake kwa wiki nzima akinichunguza na kunifundisha. Kisha alinipeleka katika kituo changu cha kazi kwa muhindi mmoja jina kapuni maeneo ya upanga. Kazi ilikuwa ni yakulala huko huko na mshahara ulikuwa ni shs 10,000/= kwa mwezi! Kazi na mimi, mimi na kazi yaani kazi kazi. Nikafanya ile kazi ya house girl kwa miezi 2 kwa kujituma sana na uaminifu mkubwa bila kulipwa ujira wangu, kila nikidai naambiwa kaonane na dada yako. Yapata kama miezi 4 kukatika niliumwa sana nikaomba wanipeleke hospital wakakataa, nikaomba ruhusa niende kumuona dada yangu wakagoma! Aloo! Kweli Dunia hadaa ulimwengu shujaa! Hata kama wanasema mtumikie kafiri upate mtaji wako hapana hii ilikuwa maji ya shingo. Nyakati za asubuhi saa kumi na moja wakati mke wa boss anaamka akanikuta natetemeka hoi sana, akaniuliza shida nini wewe? Wewe lala sana bana! Mimi pana taka vivu vivu, akiwa amenikazia macho kisha akatoka akaendelea na yakwake baada ya muda kupita kausingizi kalinipitia kidogo nikaja kushtuka na kitu cha moto wa ajabu mno! Nikapiga mayoee! Mamaaa! Kuhamaki namwona mke wa boss yupo na pasi mkononi amenikazia macho. Dakika 3 mbele kwa yale maumivu na kuumwa nilizimia. Kuja kuzinduka nikajikuta nyumbani kwa yule dada yangu cha kwanza tu hakunipa pole na kunihoji kulikoni ila alianza kunishambulia kuwa nimeenda kuwaibia waajiri wangu, nilipojaribu kujitetea akasema nimemtia hasara ya kunilipia hela polisi, hospitali na bado hata gharama zake za kunitoa njombe hazikirudi. Kumbuka hapo nilifanya kazi miezi 4 bila kuuona mshahara wangu! Masikini Belinda mimi. Akaniambia niondoke kwake nirudi zangu njombe, nikamuuliza sasa dada narudije ilihali sina hata mia? Akanijibu kamfufue baba yako aje akupe nauli; Ooh Belinda mimi nalia mwenyewe sina wa kumwangukia.
Itaendelea.........
This is a true story ila majina sio halisia.
 
Inaendeleaa...
Ilikuwa yapata majira kama ya saa 6 mchana jua ni kali sana nikampigia sana magoti, nikambembeleza sana lakini wapi msimamo wake ni ule ule siitaji kuwa na mwizi kwangu! Ilinibidi nikusanye rambo langu nichanganye malapa, jua linawaka kweli kweli lile la utosoni linakuja mpaka kwenye paji la uso, koo limenikauka maumivu bado makali, sina hela, sina ndugu mwingine nayemfahamu huku dar niko nakuzunguka huku mwili umechoka alaf kizungu zungu. Ooh mimi Belinda nikakaa pembezoni mwa barabara ambayo saivi ndio inaitwa mwai kibaki, sehemu niliyokuwa nimekaa ni karibu na msasani pale saiv ni Mayfair plaza ila kulikuwa bonde la mpunga hpo na manyasi yakutosha. Nikajivuta vuta dakika 5 mbele nikaanguka yaani nikazimia tena kuja kuzinduka niko kwenye nyumba ya msamaria mwema. Akanihoji maswali mengi nilipopata nafuu nami nikamjibu bila kumficha; akanipa pole kwa kweli dar kipindi hicho ilikuwa ni ya ujamaa na upendo. Nilikaa kwake kwa muda wa wiki 2 nikapata nafuu. Hapo kwa huyo msamaria saiv limejengwa ghorofa, huyo msamaria alipata ajali akarehemika watoto wakauza eneo! Basi huyo msamaria ni kama alileta tumaini jipya kwenye maisha yangu, kwani alinitaftia kazi kwenye kiwanda kimoja jina kapuni saiv kimeshafungwa. Tajiri pale kwa bahati nzuri sijui niseme mbaya alikuwa mtu mwenye asili ya Asia. Nikaanza kazi mimi Belinda nakumbuka nilikuwa mdogo kuliko wote hivo nilikuwa natumwa kila mara hata walinzi wakiniona utasikia we mtoto! Nikafanya pale kazi kwa muda wa miezi 2 huku nakaa kwa msamaria. Basi shida huwa haziishi mpaka siku ya kufa unaeza kufa pia kwa shida. Nikajikuta nimeingia kwenye mtego wa mtoto wa msamaria, abee nami ckuwah kumjua mwanaume naye akawa wa kwanza asali akanionjesha, mmh hapana ilikuwa asali mbaya sana sitaisahau daima uchungu wake na karaha yake. Maisha yakasonga na fumbo tukamfumbia mjinga, lakini msamaria akalifumbua mmh, nayeye akataka kula dodo abee! Ndio akaniambia nimepanda maembe yangu, tena shambani kwangu alafu nikayatunza kisha aje mpumbavu kuyavuna? Ikawa imeisha hio baba na mtoto wakanimega kama mkate kila mtu kwa muda wake; nami nikaona sawa kwakuwa mtoto mtu hakujua na baba mtu alijua nimeshaachana na mtoto mtu. Mshahara wa dhambi ni mauti, yakanipata nilibeba mimba nikabaki nahamaki cjui A wala Be. Mke wa msamaria akanigundua jioni jioni hivi kikaitishwa kikao cha kifamilia na jambo langu likawekwa mezani baada ya kujaribu kuficha ila wapi. Nakumbuka kila mtu aliniuliza kwa ukali ni ya nani? Pasipokujua mbele kukoje, na ule utoto nikajikuta natema nyongo kali sana, nilisema sijui ni ya nani kati ya baba na mtoto! Looh! Usiombe yakufike sali sana familia ilivurugika ndani ya sekunde, huyu anasema mwongo! Mwingine anasema haezi ongopa! Mwisho baba na mtoto wakashikana mashati, mimi nikaona huu ndio ule wakati nikatimua mbio mbaya mno kiwango ambacho hata usain bolt angeshangaa sana. Niliacha huko nguo zangu na kila kitu na wala sikutaka kuangalia nyuma. Nikalala mitaani siku hiyo kesho yake sikurudi tena kazini kwa hofu wangenitafuta huko huko, nikaamua kwenda pale ubungo ambapo nilikutana na mama moja akanipa kazi ya mgahawa alikuwa maarafu kidogo kila alfajiri tunaamka tunaogea kwenye beseni na dawa za asili kisha yale maji tunaenda nayo kazini kupikia chai na kupikia chakula. Basi biashara inaenda vizuri mno wateja wengi na wanasifia sana chakula. Basi siku ya siku huyo mama akanipa dawa za mitishamba ckujua ni za nini kuna ambazo niliweka ukeni na nyingine nilikunywa 😞 sitaki kabisa kukumbuka 😭( hapa Belinda analia kwa uchungu sana) kwanini hapa belinda alilia kwa uchungu, nikwasababu ndio ilikuwa mara yake ya kwanza kubeba mimba, kutoa mimba yaani abortion na kizazi kiliharibika hakuwahi tena kuja kubeba mimba maishani mwake up-to-date. Mateso aliyoyapitia Belinda ikiwa ni tumbo kumuuma alienda mpaka chooni akihisi mtoto anatoka yaani nishida turuke hiki kipande sababu wengine kitawakera. Mimi Belinda niliishia kulazwa tena hospital kwa hicho kitendo chakinyama lakini yote yalipita nami nikarudi mtaani nikiwa vizuri. Yule mama alinipenda sana kwa kweli akaanza kunifundisha mambo mengi, kuniamsha ubongo wangu uliolala na kunifanya kuwa mpya yaani sista du kwa kipindi hicho. Nami nikawa sio Belinda tena bali Lindy abee ndio sasa nikawa naitwa Lindy! Nikaanza kukanyagia uchawi sana kwa waganga sipungui, na wanaume nikaanza kuchagua wale wenye noti kwa kipindi hicho kwa huku dar walikuwa waoga sana kutokana na janga la ukimwi kushika kasi mno. Hivo naweza sema weekend nilikuwa naenda kutega kwenye viwanja vikubwa vikubwa kusaka wanaume wenye noti. Nikawa nawapata ila hela zikawa bado ni ndogo. Ndipo nilipokutana na Twinny akanishawishi twende bagamoyo kwa mganga mzuri na mashuhuri, kweli tulienda tukafanyiwa dawa za kutosha na chale. Hivo tukapanga twende Arusha mererani kwa wachimba madini huenda tukatoboa kule kule. Ila wazo lilinijia kwanini nisirudi kwanza nyumbani kwani ni siku nyingi sana tangu nitoke huko sijawahi kurudi, nikajipa moyo kuwa nikitoka mererani nitaenda kuwasalimia huko nyumbani! Siku ikawadia mimi na Twinny kuelekea Arusha mererani, tulipanda basi la (ngo***a) kwa kipindi hicho lilikuwa linambio kweli. Safari hioooo ya Mererani.......
Itaendelea......
This is a true story ila majina sio halisia
 
Pata muda ongezea ongezea nyama story iwe ndefu weekend hii watu hawana cha kufanya... Ila pia usiache kusisitiza kuwa HII STORY NI KWELI KABISA ILIKUTOKEA WEWE. hapo utawagusa zaidi wadau
 
Jamanie mkuje uku kuna Belinda kaanzisha kijiwe kipya tokeni uko kwa Sina akili , uku siti bado zipo tupu
20220520_203901.jpg
 
Mimi ni Belinda Wagiri, nilizaliwa yapata miaka 40 iliopita huko kidabaga njombe, wakati huo Iringa. Ni mtoto wa mwisho kwa mzee Wagiri na kikabila mimi ni mhehe. Elimu yangu ya msingi niliipata huko huko kidabaga ila sikumaliza nilikatisha masomo yangu baada ya baba kurehemika. Nilikaa kwa muda kidogo kabla yakutafutiwa kazi za ndani huko Dar es salaam. Ndio ilikuwa mara yangu kufika dar kulikuwa kumepoa sana maeneo mengi yalikuwa bado mapori, nakumbuka hata barabara nyingi zilikuwa bado ni vumbi. Nilipofika dar nilipokelewa na mwenyeji wangu ambae nilikaa kwake kwa wiki nzima akinichunguza na kunifundisha. Kisha alinipeleka katika kituo changu cha kazi kwa muhindi mmoja jina kapuni maeneo ya upanga. Kazi ilikuwa ni yakulala huko huko na mshahara ulikuwa ni shs 10,000/= kwa mwezi! Kazi na mimi, mimi na kazi yaani kazi kazi. Nikafanya ile kazi ya house girl kwa miezi 2 kwa kujituma sana na uaminifu mkubwa bila kulipwa ujira wangu, kila nikidai naambiwa kaonane na dada yako. Yapata kama miezi 4 kukatika niliumwa sana nikaomba wanipeleke hospital wakakataa, nikaomba ruhusa niende kumuona dada yangu wakagoma! Aloo! Kweli Dunia hadaa ulimwengu shujaa! Hata kama wanasema mtumikie kafiri upate mtaji wako hapana hii ilikuwa maji ya shingo. Nyakati za asubuhi saa kumi na moja wakati mke wa boss anaamka akanikuta natetemeka hoi sana, akaniuliza shida nini wewe? Wewe lala sana bana! Mimi pana taka vivu vivu, akiwa amenikazia macho kisha akatoka akaendelea na yakwake baada ya muda kupita kausingizi kalinipitia kidogo nikaja kushtuka na kitu cha moto wa ajabu mno! Nikapiga mayoee! Mamaaa! Kuhamaki namwona mke wa boss yupo na pasi mkononi amenikazia macho. Dakika 3 mbele kwa yale maumivu na kuumwa nilizimia. Kuja kuzinduka nikajikuta nyumbani kwa yule dada yangu cha kwanza tu hakunipa pole na kunihoji kulikoni ila alianza kunishambulia kuwa nimeenda kuwaibia waajiri wangu, nilipojaribu kujitetea akasema nimemtia hasara ya kunilipia hela polisi, hospitali na bado hata gharama zake za kunitoa njombe hazikirudi. Kumbuka hapo nilifanya kazi miezi 4 bila kuuona mshahara wangu! Masikini Belinda mimi. Akaniambia niondoke kwake nirudi zangu njombe, nikamuuliza sasa dada narudije ilihali sina hata mia? Akanijibu kamfufue baba yako aje akupe nauli; Ooh Belinda mimi nalia mwenyewe sina wa kumwangukia.
Itaendelea.........
This is a true story ila majina sio halisia.
Umeanza kuharibu pale uliposema Dar ilikwa mapori lakini ukawa unalipwa Tshs 10,000/=.
Unatuona papasi? Miaka ya 1980 na 1990s huo ulikuwa mshahara wa mfanyakazi serikalini
 
Mimi ni Belinda Wagiri, nilizaliwa yapata miaka 40 iliopita huko kidabaga njombe, wakati huo Iringa. Ni mtoto wa mwisho kwa mzee Wagiri na kikabila mimi ni mhehe. Elimu yangu ya msingi niliipata huko huko kidabaga ila sikumaliza nilikatisha masomo yangu baada ya baba kurehemika. Nilikaa kwa muda kidogo kabla yakutafutiwa kazi za ndani huko Dar es salaam. Ndio ilikuwa mara yangu kufika dar kulikuwa kumepoa sana maeneo mengi yalikuwa bado mapori, nakumbuka hata barabara nyingi zilikuwa bado ni vumbi. Nilipofika dar nilipokelewa na mwenyeji wangu ambae nilikaa kwake kwa wiki nzima akinichunguza na kunifundisha. Kisha alinipeleka katika kituo changu cha kazi kwa muhindi mmoja jina kapuni maeneo ya upanga. Kazi ilikuwa ni yakulala huko huko na mshahara ulikuwa ni shs 10,000/= kwa mwezi! Kazi na mimi, mimi na kazi yaani kazi kazi. Nikafanya ile kazi ya house girl kwa miezi 2 kwa kujituma sana na uaminifu mkubwa bila kulipwa ujira wangu, kila nikidai naambiwa kaonane na dada yako. Yapata kama miezi 4 kukatika niliumwa sana nikaomba wanipeleke hospital wakakataa, nikaomba ruhusa niende kumuona dada yangu wakagoma! Aloo! Kweli Dunia hadaa ulimwengu shujaa! Hata kama wanasema mtumikie kafiri upate mtaji wako hapana hii ilikuwa maji ya shingo. Nyakati za asubuhi saa kumi na moja wakati mke wa boss anaamka akanikuta natetemeka hoi sana, akaniuliza shida nini wewe? Wewe lala sana bana! Mimi pana taka vivu vivu, akiwa amenikazia macho kisha akatoka akaendelea na yakwake baada ya muda kupita kausingizi kalinipitia kidogo nikaja kushtuka na kitu cha moto wa ajabu mno! Nikapiga mayoee! Mamaaa! Kuhamaki namwona mke wa boss yupo na pasi mkononi amenikazia macho. Dakika 3 mbele kwa yale maumivu na kuumwa nilizimia. Kuja kuzinduka nikajikuta nyumbani kwa yule dada yangu cha kwanza tu hakunipa pole na kunihoji kulikoni ila alianza kunishambulia kuwa nimeenda kuwaibia waajiri wangu, nilipojaribu kujitetea akasema nimemtia hasara ya kunilipia hela polisi, hospitali na bado hata gharama zake za kunitoa njombe hazikirudi. Kumbuka hapo nilifanya kazi miezi 4 bila kuuona mshahara wangu! Masikini Belinda mimi. Akaniambia niondoke kwake nirudi zangu njombe, nikamuuliza sasa dada narudije ilihali sina hata mia? Akanijibu kamfufue baba yako aje akupe nauli; Ooh Belinda mimi nalia mwenyewe sina wa kumwangukia.
Itaendelea.........
This is a true story ila majina sio halisia.
Sisi wengine tunapenda kusoma story mpaka kwenye conclusion na fundisho.

Jaribu kutulia angalau siku mbili uandike kitu kinachofaa kusoma.
 
Umeanza kuharibu pale uliposema Dar ilikwa mapori lakini ukawa unalipwa Tshs 10,000/=.
Unatuona papasi? Miaka ya 1980 na 1990s huo ulikuwa mshahara wa mfanyakazi serikalini
Acha ubishi basi mkuu hii si ya kusadikika ni true!
 
Pata muda ongezea ongezea nyama story iwe ndefu weekend hii watu hawana cha kufanya... Ila pia usiache kusisitiza kuwa HII STORY NI KWELI KABISA ILIKUTOKEA WEWE. hapo utawagusa zaidi wadau
Hapana ni story ya mdau inamafundisho mengi!
 
Umeanza kuharibu pale uliposema Dar ilikwa mapori lakini ukawa unalipwa Tshs 10,000/=.
Unatuona papasi? Miaka ya 1980 na 1990s huo ulikuwa mshahara wa mfanyakazi serikalini

Ni Stori ya kutunga yenye ukweli MKUU au kahadithiwa hivyo kuna Baadhi ya ishu lazima aongeze mwenyewe Hali itakayomfanya aonekane muongo ingawaje Stori inaweza kuwa kweli
 
Rekebisha kuhusu mshahara wako elfu10 kwa mwezi otherwise umeicopy somewhere sio yako umeedit baadhi ya vitu
 
Andiko lako halina alama nzuri za uandishi kama vile “Aya”. Mtu unasoma hadi unapatwa kwikwi
 
Acha ubishi basi mkuu hii si ya kusadikika ni true!
Hakuna ukweli hapo... Kwa umri wa miaka 40 ni wazi kazi huyo mtu angefanya miaka ya 1990s mpaka nwanzoni mwa 2000. Huo mshahara sio kweli hivyo hadithi nzima ni ya uongi
 
Back
Top Bottom