Mimi ndiye msemaji wa UVCCM - Paul Makonda

Mimi ndiye msemaji wa UVCCM - Paul Makonda

Greenwhich

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
1,337
Reaction score
968
Kijana machachari na anayetikisa katika anga za CCM kwa sasa Paul Makonda ameweka bayana kwamba kwa wadhifa alio nao yeye ndiye msemaji wa Jumuiya ya vijana UVCCM.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa kujiamini kijana huyo machachari amesema yale yote aliyoyasema kuhusu Edward Lowassa na kundi lake ndiyo msimamamo wa Jumuiya yao na alizungumza kwa niaba ya UVCCM na siyo tamko lake binafsi kama mafisadi wanavyotaka.

Hata hivyo Mwenyekiti wa UVCCM Ndugu Sadifa Juma na Katibu mkuu wa UVCCM Sixtus Mapunda walikataa kukubali au kukanusha walipozungumza na Tanzania Daima.

Kwa sasa kuna vita kubwa ya kuwania madaraka ndani ya CCM ambapo makundi mawili yanayovutana yamekuwa yakiibuliana kila aina ya kashfa kuchafuana.

Tayari kuna tetesi zimeanza juhudi za chini kwa chini kutaka kuyapatanisha makundi hayo hasimu kwa hofu kwamba kuna hatari kwa chama hicho kuvunjika vipande vipande.
 
Kifaranga Makonda mbele,Mtetea Kinana kati,Jogoo mwoga JK nyuma akisikilizia.chochea moto
 
hili gazeti la udaku nalo kazi kuandika habari za uongo na uchonganishi ndiyo kazi yao.
 
Tayari kuna tetesi zimeanza juhudi za chini kwa chini kutaka kuyapatanisha makundi hayo hasimu kwa hofu kwamba kuna hatari kwa chama hicho kuvunjika vipande vipande.
why! why!.NO NO.i say NO.LMAO.
 
vipi mbona povu jingi unaumwa nini mkuu tulia dawa ifanye kazi.

nyoka anajimeza.jpg

Andika yote lakini yanayotokea CCM kwa sasa hayana tofauti na huyo nyoka anayejimeza
 
Wapi Ridhwani, Bashe, Sophia Simba, Anne Kilango Mallecela, Yusuph Makamba? Please tunataka haraka sana matamko yenu.
 
vipi mbona povu jingi unaumwa nini mkuu tulia dawa ifanye kazi.

siwezi kutoa povu kwny mambo yasiyonihusu.Chama cha Mizigo na mimi kamanda mwerevu wapi na wapi.We upo upande mishkaki au upande wa maneno ya kanga
 
Ndani ya ccm kuna mafisadi ambao huziba mdomo kila mtetezi wa wanyonge ndani ya chama hicho!
 
paul makonda atema cheche patamu sana CCM chocheeni moto ili kuni ziwakee ugali upikwe na watoto wale washibe chochea chochea chochea by MRISHO MPOTO
 
Dr.Mwakymbe alikuwa na anahasira kukosa Uwaziri baraza la mawaziri,Sitta alikuwa na hasira ya kuukosa Uwaziri mkuu,Nape kuukosa uwenyekiti wa umoja wa vijana,Makonda ndio yaleyale.Mtabana mwisho mutaachia,Lowasa akunaga.
 
Kijana machachari na anayetikisa katika anga za CCM kwa sasa Paul Makonda ameweka bayana kwamba kwa wadhifa alio nao yeye ndiye msemaji wa Jumuiya ya vijana UVCCM.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa kujiamini kijana huyo machachari amesema yale yote aliyoyasema kuhusu Edward Lowassa na kundi lake ndiyo msimamamo wa Jumuiya yao na alizungumza kwa niaba ya UVCCM na siyo tamko lake binafsi kama mafisadi wanavyotaka.

Hata hivyo Mwenyekiti wa UVCCM Ndugu Sadifa Juma na Katibu mkuu wa UVCCM Sixtus Mapunda walikataa kukubali au kukanusha walipozungumza na Tanzania Daima.

Kwa sasa kuna vita kubwa ya kuwania madaraka ndani ya CCM ambapo makundi mawili yanayovutana yamekuwa yakiibuliana kila aina ya kashfa kuchafuana.

Tayari kuna tetesi zimeanza juhudi za chini kwa chini kutaka kuyapatanisha makundi hayo hasimu kwa hofu kwamba kuna hatari kwa chama hicho kuvunjika vipande vipande.

Duh kwahiyo Sadifa na Sixtus Mapunda (Mtendaji Mkuu wa Jumuiya) wakae mbali na wanyamaze kabisa katika masuala ya jumuiya?

Nadhani kuna haja ya msemaji wa Jumuiya ya Wanawake naye kujitambulisha na kutoa msimammo wa jumuiya.Jumuiya ya Wazazi nayo kama vile haipo.Kuna haja ya kujitokeza msemaji wa jumuiya hiyo na kutoa msimamo.Haiwezekani jumuiya ya vijana pekee ndio iwe na ujasiri wa kutoa msimamo huku watu wazima wakiwa waoga
 
siwezi kutoa povu kwny mambo yasiyonihusu.Chama cha Mizigo na mimi kamanda mwerevu wapi na wapi.We upo upande mishkaki au upande wa maneno ya kanga

Huyu Mkuu naona yuko upande mishkaki.. Amelenga wapi kunalipa zaidi na njaa yake ilioanzia kwenye ubongo lol..
 
Hiyo ndio demokrasia paaaana kabisa ndani ya ccm. Ingekuwa chadema mtu angeshakuwa amefukuzwa kwenye chama
 
Back
Top Bottom