Mimi naogopa sana mke wa mtu

Mimi naogopa sana mke wa mtu

Goku 255

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2025
Posts
432
Reaction score
838
Nakumbuka baba alivyokataa kunisomesha, ila aliweza kuhudumia wake za watu. Baba alikuwa na jeuri, sana alinitishia kuwa hataye hakusoma ila mama alimwacha kisa tabia zake.

Hata baba hakujenga alibakia kwenye nyumba ya urithi yaani makuti, na venye baba alivyotesa enzi hizo uchagani na kahawa ila aliambulia kwenye uhuni.

Nimepambana na kumjengea nyumba, sikuamua kulipa kwa mabaya, nilitenda mema ila sasa hivi hao waliokula naye hawapo naye. Sasa hivi baba hajiwezi mimi ndio ninayemhudumia.

Mke wa mtu sumu, yaani hayo maisha yamenifanya nikaogopa mwanamke. Bora tu niwe mseja maana unapendwa ukiwa na nguvu, zikiisha we ni tambara bovu.
 
Sasa umeulizwa? Umeulizwa🙄
Mdau kawasilisha tu yake, bila shaka ni mmoja kati ya wengi katika jamii zetu.

Anaikumbusha jamii kuwa hakuna faida ya kuitenga familia huku mtu akitunza vimada ambao ni wake za watu.

Kingine muhimu zaidi ni kutambua kuwa yote tufanyayo maishani finali ipo uzeeni kama tukifika uzeeni.
 
Duhh hebu kuwa na akiba ya maneno, sio kila kitu uje kuanika humu kijana 😳
hebu muache kijana atoe ya moyoni,,, hauwezi jua leo ameamka na machungu yapi😪

kama niko hapa kukusikiliza bila kukujudge wala kukufikilia vibaya,,, pole sana kwa maumivu ila mi sijaona hiyo sumu ya mke wa mtu nieleweshe taratibu😊🤗
 
na wew ndo ujiite majina ya contraceptive pills🤭🤭😅😅 why lakin
20260227_063939.jpg
 
Nakumbuka baba alivyokataa kunisomesha, ila aliweza kuhudumia wake za watu. Baba alikuwa na jeuri, sana alinitishia kuwa hataye hakusoma ila mama alimwacha kisa tabia zake.

Hata baba hakujenga alibakia kwenye nyumba ya urithi yaani makuti, na venye baba alivyotesa enzi hizo uchagani na kahawa ila aliambulia kwenye uhuni.

Nimepambana na kumjengea nyumba, sikuamua kulipa kwa mabaya, nilitenda mema ila sasa hivi hao waliokula naye hawapo naye. Sasa hivi baba hajiwezi mimi ndio ninayemhudumia.

Mke wa mtu sumu, yaani hayo maisha yamenifanya nikaogopa mwanamke. Bora tu niwe mseja maana unapendwa ukiwa na nguvu, zikiisha we ni tambara bovu.
Acha kumsimanga baba yako...kama vipi ungejileta mwenyewe duniani....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom