"Mimba hiyo siitambui"

"Mimba hiyo siitambui"

mwanamke anaenyonyesha huwa hapati siku zake
kwaiyo kwa vile hapati siku zake akaona ni kawaida kumbe kuna jingine
hyo mimba ni yake tena amuombe mungu amsamehe elimu ya biologioa ni muhimu jamani msikurupuke
Nilikuwa silijui hilo..
 
Huyo ndugu yako awe mwanaume uvulana umuishe, kitanda hakizai haramu.
 
maelezo yanaonesha hiyo mimba ni ya muhusika. Ina maana hata shule ya msingi mlikuwa amsikilizi kile kipindi wanafunzi wanakipenda hao cha "AFYA YA UZAZI".
 
utagunduaje kama una mimba ndani ya mwezi
kwa taarifa yako kuna watu wana mimba miezi ya mwanzo wanaendelea kubleed kama kawaida
pia hyo mama anaonekana alikuwa ananyonyesha na mtu anaenyonyesha hapati siku zake kwaiyo isingekuwa rahisi kujigundua
usiwe mwepesi kuhukumu kama hujui jambo kaa kimya

Umesema eti ndani ya mwezi mmoja mtu hawezi kujua kama ana mimba? Kama ni hivo Ngoja nilianzishe nirudishiwe hela zangu haraka sana.
 
Umesema eti ndani ya mwezi mmoja mtu hawezi kujua kama ana mimba? Kama ni hivo Ngoja nilianzishe nirudishiwe hela zangu haraka sana.
kwqa situation ya hyo mama kwamba ananyonyesha na kwamba alikuwa haoni siku zake kwa ajili ya kunyonyesha ingekuwa ngumu kugundua kama ana mimba kama hakupata shida ingiune yoyote kumbuka kipimo rahisi kwa mwanamke ni kutokuona siku zake.sasa hapo angejuaje
 
Kwanza nadhani jamaa asubiri mtoto akizaliwa aende akachukuwe DNA kwasababu kuna siku nilikuwa naangalia show mmoja. Kuna mdada alikuwa amekaa na wazee wake akajisikia kuumwa sana wazee wake wakampeleka hospital. Wote hawakujua tatizo mpaka doctor alisema akapigwe x-ray akidhania huyo mgonjwa ana vidonda vya tumbo. Kufika chumba cha x-ray kuna mdada akasema huyu mgonjwa mbona ana dalili za uja uzito? Mgonjwa mwenyewe akabisha na wazazi wake pia. Wote wakakubaliana apewe vipimo vya mimba kabla ya kupigwa hio x-ray. Majibu yalikuja mdada ana mimba ya miezi saba na kweli baada ya miezi miwili alijifungua mtoto. Kwahio mwambie huyo rafiki yako asikatae kwanza mpaka apime DNA. Hata mimi sitaki niwe kwenye kundi la 49% lakini sitokataa kama hivyo.
 
Napita...!sina utaalamu wa sayansi ya uzazi wala biology.
 
Habarini wakuu,

Bila kupoteza muda kama kichwa cha habari kinavyojieleza, ni jamaa yangu mmoja alinifuata na kuniambia kuwa wana ugomvi na mke wake juu ya mimba aliyonayo kwani mazingira aliyoipata hiyo mimba hayana udhibitisho au uhalali wa jamaa kuwa mmiliki.

Labda nieleze kwa kifupi juu ya mazingira menyewe, Kwa mujibu wa maelezo ya jamaa yangu, Jamaa ni mtu wa kusafiri safiri sana. Jamaa aliondoka nyumbani kwake tangu mwezi wa pili Mwaka huu 2016, mpaka sasa hajarudi nyumbani, na aliacha hali ikiwa shwari kabisa wala hakukuwa na dalili zozote za ujauzito.

Sasa juzijuzi tu mke wake amempigia simu akamwambia ana ujauzito wa miezi minne, jamaa alichanganikiwa na kukawa na mvutano mkali sana kati yake na mkewe, jamaa alihoji, mimba ina miezi minne hujaniambia kwanini? Jibu la mwisho la jamaa lilikuwa kama ilivyoandikwa kwenye kichwa cha uzi huu yaani "Mimba hiyo siitambui" Ikumbukwe kuwa mpaka saizi hajarudi nyumbani, wanawasiliana kwa njia ya simu tu, vilevile wana mtoto mmoja kwenye ndoa yao ambaye ana umri kati ya miezi 10 hadi 12.

Je, Kwa wataalamu wa mahusiano na sayansi ya uzazi na wale wenye uzoefu, pia wanawake wenyewe inawezezekana kweli kukaa miezi minne bila kujitambua kuwa una mimba?

Karibuni tunusuru ndoa ya huyu jamaa.

Nawasilisha.

Anaejua Baba wa Mtoto ni Mama Ndugu, inaonyesha kwamba kabla ya kusafiri hiyo miezi alikuwa kwake na kama Mkewe alipata Ujauzito huenda alisubiri Jamaa atoke safarini amwambie, kwa kuona muda unakwenda imembidi ampigie simu katika maongezi yao, Sasa kama kakuomba ushauri Mwambie arudi nyumbani kwanza badala ya kufoka na kukana hawa Watu wa kusafirisafiri wanajua kupanda Mbegu tu ila kasheshe mmea ukichipuka..maelezo mareefu
 
Kuna watu wana mimba bila kujijua kama Ana mimba kutokana na kutokuwa na mabadiliko mwilini mwao. Mwambia rafiki yako kabla hajakataa ni bora akae chini na kutafakari . Kama Anayo mashaka asubiri mtoto azaliwe achukue DNA ila kwa sasa aendelee kufanya majukumu yake kama mume
 
Utafiti, 50% ya watoto ni wakusingiziwa. Tuvumilie tu wanaume wenzangu
 
Habarini wakuu,

Bila kupoteza muda kama kichwa cha habari kinavyojieleza, ni jamaa yangu mmoja alinifuata na kuniambia kuwa wana ugomvi na mke wake juu ya mimba aliyonayo kwani mazingira aliyoipata hiyo mimba hayana udhibitisho au uhalali wa jamaa kuwa mmiliki.

Labda nieleze kwa kifupi juu ya mazingira menyewe, Kwa mujibu wa maelezo ya jamaa yangu, Jamaa ni mtu wa kusafiri safiri sana. Jamaa aliondoka nyumbani kwake tangu mwezi wa pili Mwaka huu 2016, mpaka sasa hajarudi nyumbani, na aliacha hali ikiwa shwari kabisa wala hakukuwa na dalili zozote za ujauzito.

Sasa juzijuzi tu mke wake amempigia simu akamwambia ana ujauzito wa miezi minne, jamaa alichanganikiwa na kukawa na mvutano mkali sana kati yake na mkewe, jamaa alihoji, mimba ina miezi minne hujaniambia kwanini? Jibu la mwisho la jamaa lilikuwa kama ilivyoandikwa kwenye kichwa cha uzi huu yaani "Mimba hiyo siitambui" Ikumbukwe kuwa mpaka saizi hajarudi nyumbani, wanawasiliana kwa njia ya simu tu, vilevile wana mtoto mmoja kwenye ndoa yao ambaye ana umri kati ya miezi 10 hadi 12.

Je, Kwa wataalamu wa mahusiano na sayansi ya uzazi na wale wenye uzoefu, pia wanawake wenyewe inawezezekana kweli kukaa miezi minne bila kujitambua kuwa una mimba?

Karibuni tunusuru ndoa ya huyu jamaa.

Nawasilisha.
bro aache ukali, mbona kazi rahisi tu , leo sio 1970 ni 2016 kuna DNA TEST,amwambie mkewe hilo alielewe na huenda jibu litapatikana kabla hata ya kujifungua kwa hofu itakayomkumba huyo mkewe kama mimba si ya huyo jamaa.
 
1.jpg
 
Back
Top Bottom