Millen Magese (Happiness Magese) apata mtoto

Kuna mama humu jf alikuja na uzi akasema ameambiwa kwamba hatoweza kuzaa kabisa..ila baadae akapata mimba na akazaa.
Kuna ndugu yangu alikua anaumwa ini na hospital akaambiwa kwa hatua aliyofikia hatoweza kupona.
Ila akabadili tiba na sasa ni mzima kabisa na viroba anakunywa.
Nadhani hauamini katika kufanya yanayoaminika kwamba hayawezi kufanyika..
Au basi wewe umezoea ubishi.

love thé love or hâte thé love.....
Achana na huyo jamaa,yani jamaa ana wivu huyo mrembo kapata mtoto. Hongera kwa aliyepiga mashine. Hopeless.
 
Mtu ambae hajawahi zaa na watu wanajua kuwa hajazaa apate mimba akae kimya?
Miezi 9. Hivi unadhani mimba ni sawa na mswaki kuwa unaweza uficha mfukoni?
Asilimia kubwa ya watu wanaotafuta mtoto hawapendi kushow off pindi wapatapo ujauzito mpaka siku anajifungua, inaelekea ujapenda alivyopata mtoto sio vizuri ndugu yangu mtu akipata neema au baraka flani ni vizuri kuifurahia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asilimia kubwa ya watu wanaotafuta mtoto hawapendi kushow off pindi wapatapo ujauzito mpaka siku anajifungua, inaelekea ujapenda alivyopata mtoto sio vizuri ndugu yangu mtu akipata neema au baraka flani ni vizuri kuifurahia

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwanini alidanganya umma kuwa hawezi pata?
Watu walimuonea huruma kumbe alikuwa anadanganya....
Alitumia matatizo yake kuanzisha foundation kumbe mjanja anataka ale hela za watu
 
Mtu ambae hajawahi zaa na watu wanajua kuwa hajazaa apate mimba akae kimya?
Miezi 9. Hivi unadhani mimba ni sawa na mswaki kuwa unaweza uficha mfukoni?
mange alishatudokeza siku nyingi tu kwamba dada ni mjamzito....
nadhan yeye aliamua kuwa kimya kwa sababu ya mazingira ya mimba yake ambayo ni ya kupandikizwa so inakuwa na complications nyingi.....imagine angetangaza halafu ije itoke, lazima matomaso kama ww mngemdiss kwamba muongo....
ni mara ngapi watu wamekuwa wakimtukana kutokana na kuweka wazi tatizo lake..
dunia hii hawezi kumfurahisha kila mtu.
 
Kwanini alidanganya umma kuwa hawezi pata?
Watu walimuonea huruma kumbe alikuwa anadanganya....
Alitumia matatizo yake kuanzisha foundation kumbe mjanja anataka ale hela za watu
Hivi ukiambiwa kitu na daktari ni vibaya kushare na jamii kama inahitajika kufanya hivyo? Unajua ni wangapi wana ilo tatizo ila wameligundua kupitia yeye? Imekuuma sana yeye kuzaa? Duuh haya Mkuu siku njema.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watanzania wengi ni kama hawana akili, hata ukiwadanganya watajitokeza na kusema hongera, na kuna uwezekano mkubwa san akuwa huwa hawasomi kinacho andikwa kwenye makala husika ila baada ya kuona wenzao wanasifia na wao pia wanasifia.

Huyu mdada aliwahi sema kuwa hana uwezo wa kuzaa, na keshafanyiwa operations zaidi ya mara 3 kuhusiana na hilo tatizo.

Huyu atakuwa kapata mtoto kupitia surrogate mothers
atakuwa amefanya in vitro fertilization kwasababu kuna jamaa ameweka picha enzi za ujauzito!
 
kama ni hivyo ni sawa ila watu hawataki hata kuuliza mbona huyu alituaminisha kuwa hawezi zaa kabisa
ila ukifuatilia vizuri interviews zake hakusema hawezi kuzaa kabisa, alikuwa akisema hawezi kupata ujauzito kwa njia ya kawaida. aliongea anaweza kuzaa kwa in vitro au surrogate mother, naona yeye amechagua hiyo ya kwanza!
 
Back
Top Bottom