Mila na desturi zetu

Mila na desturi zetu

CharmingLady

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2012
Posts
18,304
Reaction score
12,997
Thanks God its Friday

Hamjambo

Back to Topic: Nchi yetu ya Tanzania imejaaliwa kuwa makabila mengi sana zaidi ya mia moja kama sikosei. Katika haya makabila huwa kuna mila na desturi mbalimbali ambazo mtu akifanyiwa huwa anaona kama amepewa heshima ya pekee.

Mfano: Katika kabila nitokalo mimi, mkwe akienda kusalimia kwao na mkewe huandaliwa uji wa aina fulani ambao umetengenezwa kwa unga wa ulezi na mafuta ya ng'ombe, Almaarufu kama "Ikirunguri cha Bhairwa" yaani mkwe akipewa huu uji huwa anakuwa amapewa HESHIMA ya PEKEE. Hiyo ni kifungua kinywa.

Baada ya hapo atapewa togwa "Ubhusara" tena kichwaji hiko kitakuwa kimewekwa kwenye "Ikisonzo" (nimekosa kiswahili chake) wakati akisubiri chakula cha mchana.

Chakula cha mchana anapikiwa ugali wa Udaga, ugali huu utakwua umepikwa kwa kutumia unga wa mtama uliochanganywa na muhogo, Pia ugali huu ukitengwa mezani utakuwa umeweka namna hii.
attachment.php

ugali huu utaliwa kwa nyama ya ng'ombe au mbuzi bila kusahau "Kichuri" pembeni.

HAYA MNAWEZA KUTUPIA CHAKULA AMBACHO NI CHA HESHIMA AU JAMBO LOLOTE LA HESHIMA AMBALO MGENI ANAWEZA KUFANYIWA PINDI AFIKAPO NYUMBANI


CL
 

Attachments

  • ugali.jpg
    ugali.jpg
    37.7 KB · Views: 481
Kina msosi wa ndizi na maharage huko Kibosho, Utadhani ni keki!
 
Mimi mambo ya kimila na utamaduni naona kama kuzinguana. Vitu vingine kuachana navyo tu.
 
Mimi mambo ya kimila na utamaduni naona kama kuzinguana. Vitu vingine kuachana navyo tu.

Mkuu unasema kwa vile unaishi mjini ama wazee wako wapo mjini. Hebu rudi kule "Ushagoo" uone kama tutafanyiwa mambo ya kimila?

Wazee wetu bado wanaipractice sana tu!!!
 
wakwe wa siku hizi wanataka smartfone na maipad hayo mengine tupa kule lol!!!! TGIF though....
 
Nimezaliwa nje ya mkoa wangu, nimekulia nje ya mkoa wangu na hata kuongea kabila langu sijui ila napenda saana asili yangu mila yangu pia, huenda kijijini mara chache sana.

Kabila langu mimi, huko kijijini akija mgeni hukaribishwa chakula cha mchana nacho: Anapikiwa wali kama kilo mbili hivi na kuku mzima amle asipommaliza jioni wakati anarudi alikofikia hufungashiwa chakula chake anarudi nacho na kila siku utaalikwa nyumba nyingine, na unaporudi mjini wanakupa zawadi ya nsansa, uyoga mkavu na swalu ukibahatisha na matobholwa ni moja ya makabila ambayo ni wakarimu sana Tanzania najivunia hilo
 
Wengine tumechanganya makabila mpaka tumedata....

Ila mojawapo la kabila kwa wali na samaki weeeeeeeeeeeee

Yaani kama kaja kwako hajala wali samaki ujue hujamlisha........

Kabila nyingine nilizomix sisemi
 
wakwe wa siku hizi wanataka smartfone na maipad hayo mengine tupa kule lol!!!! TGIF though....

Uko sahihi lakini nahisi hujanisoma vizuri.. Namaanisha wewe hapo ukienda ukweni kwako utapewa hayo macare, sio kwamba ukienda utawapa hayo macare!
 
Wengine tumechanganya makabila mpaka tumedata....

Ila mojawapo la kabila kwa wali na samaki weeeeeeeeeeeee

Yaani kama kaja kwako hajala wali samaki ujue hujamlisha........

Kabila nyingine nilizomix sisemi

Mkuu hata uchanganye vp bado lipo moja lenye nguvu nalo ni la baba wa baba yako na ndio kabila lako, tz tumechanganyika sana makabila hadi inafikia ukiulizwa kabila unajibu "mimi mswahili" lakini bado asili ipo tu mkuu huwezi kuiepuka na ndio asili yako.
 
Hayo ni mambo ya kizamani ndo mana hata kule kwetu, sku izi hakuna zile nyumba za kimaskini.

Siku izi watu wanakula mabaga na kujenga nyumba zenye tiles.
 
Thanks
God
its Friday

Hamjambo

Back to Topic: Nchi yetu ya Tanzania imejaaliwa kuwa makabila mengi sana
zaidi ya mia moja kama sikosei. Katika haya makabila huwa kuna mila na
desturi mbalimbali ambazo mtu akifanyiwa huwa anaona kama amepewa
heshima ya pekee.

Mfano: Katika kabila nitokalo mimi, mkwe akienda kusalimia kwao na mkewe
huandaliwa uji wa aina fulani ambao umetengenezwa kwa unga wa ulezi na
mafuta ya ng'ombe, Almaarufu kama "Ikirunguri cha Bhairwa" yaani mkwe
akipewa huu uji huwa anakuwa amapewa HESHIMA ya PEKEE. Hiyo ni kifungua
kinywa.

Baada ya hapo atapewa togwa "Ubhusara" tena kichwaji hiko kitakuwa
kimewekwa kwenye "Ikisonzo" (nimekosa kiswahili chake) wakati akisubiri
chakula cha mchana.

Chakula cha mchana anapikiwa ugali wa Udaga, ugali huu utakwua umepikwa
kwa kutumia unga wa mtama uliochanganywa na muhogo, Pia ugali huu
ukitengwa mezani utakuwa umeweka namna hii.
attachment.php



ugali huu utaliwa kwa nyama ya ng'ombe au mbuzi bila kusahau "Kichuri"
pembeni.

HAYA MNAWEZA KUTUPIA CHAKULA AMBACHO NI CHA HESHIMA AU JAMBO LOLOTE LA
HESHIMA AMBALO MGENI ANAWEZA KUFANYIWA PINDI AFIKAPO NYUMBANI


CL

mgeni atapewa maziwa yatawekwa kwenye kibuyu( ekyanzi) kinang'aa na
kunukia vizuri. mbuzi au ng'ombe ni lazima achinjwe.maziwa ni lazima
sana na vyakula vingine vya kisasa+ kimila
 
Mkuu hata uchanganye vp bado lipo moja lenye nguvu nalo ni la baba wa baba yako na ndio kabila lako, tz tumechanganyika sana makabila hadi inafikia ukiulizwa kabila unajibu "mimi mswahili" lakini bado asili ipo tu mkuu huwezi kuiepuka na ndio asili yako.


Ni kweli mkuu hebu BADILI TABIA tuambie mila na desturi za kwao baba wa babu yako zipoje??
 
Last edited by a moderator:
mgeni atapewa maziwa yatawekwa kwenye kibuyu( ekyanzi) kinang'aa na
kunukia vizuri. mbuzi au ng'ombe ni lazima achinjwe.maziwa ni lazima
sana na vyakula vingine vya kisasa+ kimila

Hapo kwenye kibuyu pamenikuna.... Mila nyingi za kiafrika hufanana??
 
Ni kweli mkuu hebu BADILI TABIA tuambie mila na desturi za kwao baba wa babu yako zipoje??

Mkuu labda hukunielewa ni baba wa baba yangu ambaye nimeshakueleza huko juu, kuhusu babu wa baba yangu nitakudanganya ila kwa vile histori hujirudia bado mila itakuwa ni ile ile , mkuu kukubali ni maamuzi ila nimeeleweka ndio maana sikumgusa bibi mzaa baba au mama yangu
 
Back
Top Bottom