Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,641
- 46,292
Kwenye mkutano wa Makonda huko Moshi kumejetokeza kwamba Manisipaa imechukua eneo la mtu (Mhindi) na kulipima kimakosa kisha kuwauzia wananchi. Mhindi kaenda mahakamani, kashinda kesi dhidi ya manisipaa lakini wanaotakiwa kulipia eneo ni raia badala ya manisipaa!, raia waliouziwa ardhi na manisipaa wanamlalamikia Muhindi na kumshitaki kwa Makonda badala ya manisipaa iliyowauzia ardhi ya mtu na manisipaa yenyewe imeuchuna tu!
Kwenye mkutano mwingine Meneja wa TANESCO hajui vigezo wanavyotumia kugawa umeme kwa mida tofauti kwa maeneo tofauti! Hata kama hakuna vigezo si angesema tu hakuna vigezo kwa sababu umeme ni hitaji la muhimu kwa watu wote
Mbunge wa Arusha mjini, Mrisho Gambo anawashitaki mgambo wa Arusha walio chini ya Halmashauri inayoongozwa na chama chake na watendaji walioteuliwa na chama chake kwa mwenezi wa chama chake na anashangiliwa na watu wa chama chake!
Kuna burudani nyingi sana katika mikutano ya katibu mwenezi wa CCM hata kwa kufuatilia kwa uchache tu, bahati mbaya sana hatuna wachekeshaji wa kisiasa katika tasnia ya comedy nchi ambao wengejipatia content za comedy za kutosha kila siku kutoka katika siasa zetu.
Kwenye mkutano mwingine Meneja wa TANESCO hajui vigezo wanavyotumia kugawa umeme kwa mida tofauti kwa maeneo tofauti! Hata kama hakuna vigezo si angesema tu hakuna vigezo kwa sababu umeme ni hitaji la muhimu kwa watu wote
Mbunge wa Arusha mjini, Mrisho Gambo anawashitaki mgambo wa Arusha walio chini ya Halmashauri inayoongozwa na chama chake na watendaji walioteuliwa na chama chake kwa mwenezi wa chama chake na anashangiliwa na watu wa chama chake!
Kuna burudani nyingi sana katika mikutano ya katibu mwenezi wa CCM hata kwa kufuatilia kwa uchache tu, bahati mbaya sana hatuna wachekeshaji wa kisiasa katika tasnia ya comedy nchi ambao wengejipatia content za comedy za kutosha kila siku kutoka katika siasa zetu.