Mikutano ya hadhara sio ruksa, ya ndani ruksa

Mikutano ya hadhara sio ruksa, ya ndani ruksa

Basi hakukuwa na sababu ya kuitisha. Wangesubiri mpaka muda uruhusu. BTW 1. mbona wasanii wamechukuwa muda mrefu kufanya mambo yasiyo na umuhimu? 2. Je unajua kuwa mikutano na waandishi ni moja ya kazi muhimu na za lazima za rais?
Kumbuka vikao vya aina hiyo kila mtu hawezi kuongea na matatizo yanaweza kuwasilishwa kwa njia ya maandishi na yakapatiwa utatuzi.
 
Mama kasema wazi kabisa, mikutano yenu imejaa vurugu hivyo itakimbiza wawekezaji
Kwa kuizuia ndio anajiingiza kwenye mtego wa kuwashughulikia wale watakao kaidi. Atajikuta analazimika kuruhusu polisi watumie nguvu za ziada kuwazuia na kuwaweka ndani baadhi yao. Tutajikuta tumerudi kulekule ambako anasema anataka kututoa. Hawezi kutegemea chama kama Chadema kikubali kukiachia chama chake peke yake uwanja wa kufanya siasa na kuuza sera zao kwa wananchi. Hiyo rebranding anayoizungumzia itaingia doa. Angeeleweka vizuri zaidi kama angezuia mikutano yote ya hadhara pamoja na ile ya wabunge. Hiyo iwe pamoja na viongozi wa serikali kutumia nafasi zao kufanya siasa za kichama.

Amandla...
 
Mama akikutana na akina Mbowe atabadilisha msimamo wake.

Hii kusema mpk uchumi ukae sawa nadhani mama anatumia jiwe methodology.

Tutampinga kwa nguvu zetu zote. Mama kwa hili abadilike. Uchumi haupandi kwa kuzuia mikutano ya hadhara.

Mwendazake alikuwa dikteta uchwara, huyu mama ni dikteta laini.
Nano aruhusu tena fujo zenu mitaanii?? Tumeshasahau mipasho na matusi jamaaniii.
 
Kwasasa tunapiga mikutano ya ndani yenye impacts za maana hadi nyie mataga pori mtatamani mikutano ya hadhara iruhusiwe.
Nyumbu leo ndiyo wamejua mama aliposema yeye ni kitu kimoja alimanisha.

Samia = Magufuli
 
JF siku hizi imejaa ngumbaru kila mahali kiasi kwamba inaboa kuingia humu.

Unaelewa kuwa haki ya mikutano ya kisiasa siyo tu kwamba ni haki ya kikatiba bali ni universal declaration of human rights?

Nikikuita kuwa wewe ni punguani nitakuwa nimekuonea?

Unamshobokea mtu anaevunja katiba ambayo ameapa kuilinda?Wewe ni tahira?
109_20210628_200150.jpg
 
Kumbe Nae Anauogopa upinzani
Wala haogopi chochote, ni kwamba hataki tu propaganda za kijinga maana hakuna cha maana kinachopatikana kwenye hivyo vikao ambacho ni masilahi ya Watz kwa ujumla.

Upinzani hauna sababu ya kuogopwa hata kidogo.
 
Mama yuko sahihi.

Watanzania hawa masikini wa kutupwa wanahitaji kuhamasishwa kufanya kazi za uzalishaji na sio kuandamana sijui kushinda kwenye mikutano ya siasa isio na faida kwao.

Mtu hana uhakika mchana atakula nini Mbowe anataka akaandamane toka asubuhi hadi jioni halafu watoto watakula nini wakati Mbowe kawekewa hela kwenye akaunti yake na wazungu.

Hata huko Ulaya watu hawashindi wanaandamana tu kila siku, wanapiga kazi ndio maana tunaenda kuomba misaada na mikopo kwao, wangekua wanashinda kila siku ni kuandamana wasingekua hapo walipo.

Siasa zifanywe zenye kuleta tija.

Kwanza turudie kura ya kuamua kama tuwe na vyamavya siasa vingi ama kimoja.
 
Hawezi kuruhusu mikutano huku anatoa tahadhari ya korona.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Mikutano hauruhusiwi sio sababu ya corona bali ni ujinga kufanya mikutano uchumi ukiwa haujakua.
Kama sababu ingekuwa corona basi hata mechi zsa mpira mashabiki wasingeruhusiwa
 
Wewe nikkwa2 badilisha heading yako. Nani kakuambia mikutano ya hadhara hairuhusiwi.
Ya hadhara ndani ya eneo lako kama ni mbunge ruksa. kusema ya hadhara ni misleading statement wewe Nikkwa2 sijui chawa wake
Haya sawa, je kwani nyie mna wabunge? Au wale 19??[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom