Mleta mada ni vema ukakiri asilimia kubwa ya andiko lako umehadithiwa. Nimefika huko na kukaa kwa muda, mengi yanayosemwa ni hadithi tu. Ingawaje aliyeweka point ya kijiji cha Kalundi huko Nkasi kuwa na watu waliofukuzwa sehemu nyingine kwa imani za kishirikina yuko sahihi kwa kwa kiasi Fulani maana hicho kijiji hakuna paka hata mmoja, usiniulize kwa nini!!
katavi nimekaa sana na mwezi ujao ntakuwa huko, daa! watu wanga sana roho mbaya kiwango cha lami
kuna familia mtoto/watoto wakiwa wanasoma wanapigwa juju ya kukataa shule ama kupata mikosi ya kila namna?
watoto wadogo nao wanga tu, wakubwa ni ndagu mwanzo mwisho kupata familia 20 ambazo sio wanga ni mtihani.
kuna mama mmoja (diwani ) alishindwa kura ya maoni kugombea udiwani na kijana wa 4m6 dogo hakuchukua round chaliiii
hata mkurugenzi aliye fariki mwaka huu (yule kijana niliona bandiko la tanzia humu) alipigwa juju na mzee mmoja aliye taka mwajibisha baada ya upotevu wa pesa za umma mzee akafanya yake.
radi zinauzwa mkuu ushishangae, kanatokea kakijiwingu kadogo tu hata kama umejificha kwenye kundi la watu radi inakuchomoa na kukugalagaza vibaya muno.
Tangu nianze kutembelea hii mikoa katika maeneo mbalimbali kama Inyonga,Majimoto,sumbawanga,mpimbwe na hapa katavi mjini nimekutana na watu wenye magonjwa ya kushangaza sana.Nilikutana na mama mmoja ambaye mwili wake wote ulikuwa umeharibika(Ni dhambi kusema umeoza) huku ukimwaga maji chapachapa.
Siku nyingine ndani ya basi nilishangaa kumuona mzee mmoja aliyekuwa amepanda na dumu la maji la lita tano na kila baada ya muda mfupi alikuwa akijimwagia maji kwa madai kuwa miguu yake inawaka moto.
Pia wakazi wa huko walinishangaza baada ya kuniambia kuwa huko kwao radi inauzwa,nilishngaa kwa sababu najua radi ni umeme tuli.Lakini jamaa waliniambia nikitaka hata kwa elfu kumi ninaipata [emoji102][emoji102][emoji102].
Pia mtu alishawahi kupanda basi na kuwafanya wasafiri wenzake wote kushindwa kula wala kunywa maana alikuwa na kidonda kikubwa ambacho kilikuwa na wadudu na kilifanya hali ya hewa ya basi zima kubadilika na hata aliposhuka hali haikuwa shwari.
Nimetembea sehemu nyingi sijawahi kukutana na maradhi ya aina hii lakini nilipowauliza wakazi wa maeneo haya walihusisha maradhi hayo na imani za kishirikina.
Najua mtaomba picha,picha ninazo lakini sina ujasiri wa kuzianika mtandaoni.
mkuu nakupa mifano ya uchawi katavi.Acheni uongo na kutuchafulia mikoa yetu.!
katavi sio mkoa mkuu wa kuishi wanga wako wengi sanaBora unisaidie ndugu maana mimi nimeona na kusikia.
Heeh!wanapaweza wenyewe tuHuko kunguru hanyakui vifaranga vya kuku ananyakua Ng'ombe tu
na hapo napo ndo mikoa inayoongoza kwa manunuzi makubwa ya vilevi mf pombe balimi ukona ukiangalia ndio mikoa maskini ya kutupwa.
Ukienda mgeni unaweza usirudi kama hasa kama nidhamu BashiteHeeh!wanapaweza wenyewe tu
swaxy townSijui labda mabushi bushi huko... Mjini hatuoni hayoo...
Nimeishi sana Swanga..
Hunidanganyi kitu...swaxy town
wacha wee npe AB C kidgo maana niliwah fika siku moja na kesho yake kurud tundumaHunidanganyi kitu...
Tanga hawana hizo mambo.Halafu cha kushangaza mikoa hiyo yenye hizo imani potofu RUKWA/KATAVI na ndugu zao katika teknolojia TANGA wana ardhi kubwa nzuri na yenye rutuba sisi wageni tunaogopa kwenda kufanya kilimo huko kwa ajili ya taaluma zisizo na matiki za hao wenyeji