Mikasa ya Kutisha,vituko,visa na vioja miaka ile tunasafiri wiki moja Dar-Mwanza. Siku 3 Dar-Singida

K
Nakumbuka zamani mikoa ya kusini kwenda dar kabla daraja la mkapa halijajengwa pale mto wa rufiji palikuwa na pantoni hilo la kwanza la pili ni barabara ya nyamwage, muhoro ilikuwa mbaya sana.

Tuanze na barabara ya eneo la nyamwage na muhoro ile barabara ilkuwa zikinyesha mvua tu aisee mtazama kwenye tope mkae hapo hata siku 3. Mkitoka hapo mnakutana na foleni la mto rufiji kupia kwenye pantoni hapo napo hata siku 2.

Mbaya zaidi usiombe pantoni libume, ma wweeeee!mnavuka na mitumbwi midogo sana ya watu wa3 kiasi kwamba ukitoa mkono pembeni umegusa maji.
Palikuwa na mamba na kiboko wengi na washakula watu wengi sana miaka hiyo ya zamani.

Ashukuriwe mkapa maana aliokoa mengi yule baba, nampongeza kwa hilo.

Mikate ilikuwa inaning'inizwa haswa....
Kwa mara ya kwanza wakati nafanya safari ya Dar- Mtwara,nilipopanda gari pale Ubungo alfajiri nilikuta mikate imening'inizwa ndani ya basi nikadhani inapelekwa kama zawadi na abiria lakini hadi siku tunafika Lindi mikate yote ilikuwa imekwisha kuliwa maana tulilala njiani siku nne na pale Nyamwage ilikuwa ni noma sana,kwa mtu ambaye hakuwahi kuipita njia hiyo hawezi kujua adha za kipindi hicho
 
K

Kwa mara ya kwanza wakati nafanya safari ya Dar- Mtwara,nilipopanda gari pale Ubungo alfajiri nilikuta mikate imening'inizwa ndani ya basi nikadhani inapelekwa kama zawadi na abiria lakini hadi siku tunafika Lindi mikate yote ilikuwa imekwisha kuliwa maana tulilala njiani siku nne na pale Nyamwage ilikuwa ni noma sana,kwa mtu ambaye hakuwahi kuipita njia hiyo hawezi kujua adha za kipindi hicho
Yaani hawezi kujua kabisa..
Ile sehemu ni kichwa cha mwendawazimu ilikuwa. Ni hatati sana yaani, watu tuli suffer kweli kweli.
 
Dodoma iringa,kiti king cross na yarabi salama,mnapitia mtera,mlima nyang'oro,hapo ndio ule Msemo unaosema safari ni nusu ya kifo unapokuwa na maana
Siku moja natoka mbeya iringa pale siku 2 tunangoja king cross toka dom mkata ticket kaingia mitini tumemsaka tukamkuta kilabuni akala kipondo akarudisha pesa,
Tukaona hapo ni kuunga safari, tukalipata bus shala-wambe renault inaishia mtera tukalipa wanakijiji kibao wanashuka njiani, basi katiza tu nje ya Iringa tu hapo pancha.
Mwenyeji mmoja akatupa tip jirani hapo kuna mama anauza ulanzi
Basi tukashtua konda wakimaliza watuite
Tukaenda kula ulanzi, konda kaja akapiga lita tunarudisha kwenye bus.
Då konda kanogewa kumbe juu carrier kuna
Ulanzi kibao, we akapanda juu kanyonya mrija ule wa petrol akashuka nao basi aaah anajaza dumu tunapasha, kufika nyang'oro zile kona konda kalewa ulanzi gari imekula kona kali si akachomoka na mlango kaangukia bondeni huko tukamfata kumtoa, 🤣🤣🤣
Tukamrudisha juu safari inaendelea.
Mvua hatari tumekaribia Mtera usiku mnene.
Kuna kilima pale.
Kabla kufika darajani bus kila dereva akipanda mlima hatufikishi juu linarudi reverse mpaka chini
Mwisho lilirudi akagonga mbuyu kwa nyuma ndo kusimama.
Badae sota sana na konda kuweka kigogo
Hilo tope balaa.
Tulifika hoi ndo tukazama ndani ya bus ingine urafiki mpk dom.
Adventure ilikua safi sana kula mpunga na samaki watamu pale mtera
Asb ndo tukaunga kwenda dom.
Safari ilikua sinema tu.
 
Kuna mtu anaikumbuka Sharuks luxure ya kwanza Sgd -Dar?
Ilikua Scania bus moja kali sana sijawahi kupanda hela nilikua sina.
Sahib je Arusha-Sgd hilo mbio tu kupitia makiungu njia vumbi tu.
Tawaqal Mwanza -Dar
Najmunisa Shy-Dar
Azan express.Sgd-Dar
Ilikua tabu sana enzi hizo maana hizo ngoma zikiingia Sgd pale zinapiga misele kwanza honi nyingi sana kisha ndo dereva anapaki abiria wapande ye anapiga supu e bana akiamka tena honi kona mbili anazunguruka pale stendi honi nyiingi akiipata njia ile ya kwenda Manyoni anapiga kile kilima pale sasa mtakoma akikimaliza ni kula matuta tu,
Kinachochekesha Ajali enzi hizo hamna kabisa ni mwendo tu,njia vumbi tu mpk Dom ni kubamizwa tu juu chini kushoto kulia dere hana habari,Mkifika dom mmeisha kabisa unaambiwa mna vumbi,matope utafkiri mmetoka kulima .
 
Kuna mtu anaikumbuka Sharuks luxure ya kwanza Sgd -Dar?
Ilikua Scania bus moja kali sana sijawahi kupanda hela nilikua sina.
Sahib je Arusha-Sgd hilo mbio tu kupitia makiungu njia vumbi tu.
Tawaqal Mwanza -Dar
Najmunisa Shy-Dar
Azan express.Sgd-Dar
Ilikua tabu sana enzi hizo maana hizo ngoma zikiingia Sgd pale zinapiga misele kwanza honi nyingi sana kisha ndo dereva anapaki abiria wapande ye anapiga supu e bana akiamka tena honi kona mbili anazunguruka pale stendi honi nyiingi akiipata njia ile ya kwenda Manyoni anapiga kile kilima pale sasa mtakoma akikimaliza ni kula matuta tu,
Kinachochekesha Ajali enzi hizo hamna kabisa ni mwendo tu,njia vumbi tu mpk Dom ni kubamizwa tu juu chini kushoto kulia dere hana habari,Mkifika dom mmeisha kabisa unaambiwa mna vumbi,matope utafkiri mmetoka kulima .
😜😋 Niliuea nawashuhudiakaka zangu wakija likizo wako kamawametoka shamba!
Halafu mwishoni mwa 1980s kunaMwarabu alileta Bus Luxury Fulani hivi Singida - Dar lilikuwa linaitwa ShaAlly,sijui kama lilidumu hata miezi 6
 
😜😋 Niliuea nawashuhudiakaka zangu wakija likizo wako kamawametoka shamba!
Halafu mwishoni mwa 1980s kunaMwarabu alileta Bus Luxury Fulani hivi Singida - Dar lilikuwa linaitwa ShaAlly,sijui kama lilidumu hata miezi 6
Ndio hiyo Shaally Sharuks nimechapia ilikua kali kweli ile bus ilikufa kifo cha mende.
Enzi hizo vinatamba vi bus kipanga km hiyo Azan ,Sahib ,na Nissan UD tu Luxure haiwezi njia ilikua kimeo sana
 
Aisee...nimekuja kukumbuka miaka ile baada ya jamaa mmoja kuandika kisa chake ingawa actually hakikuhusiana na aina ya usafiri sana.

Nakumbuka miaka ile ilikuwa unaposafiri kwenda mwanza ilikuwa inabidi ujipange sana.tena kama ndo familia ilikuwa mnajiandaa ile kufa mtu. Mama atapika maandazi, nyama za kukaanga, atakaanga na ndizi au viazi, atanunua juice za chemicola/black current na kubeba madumu makubwa ya maji ya kunywa.

Wakati huohuo pia anaweza akabeba na viberiti kadhaa na hata mchele na maharage just in case. Miaka hiyo usafiri ulikuwa mgumu sana. Mabasi yalikuwa ni Leyland Daf ,TATA au Isuzu body lake chuma kitupu na viti vya chuma au mbao na ka sponge kwa mbali. ilikuwa issue hasa.

Ilikuwa mnaposafiri mnabeba mito ya kukalia au kuegemea na wakati huohuo mmebeba vyakula vya dharura ikitokea mmelazimika kulala njiani kutokana na barabara kuharibika.

Suala la kukwama au kukuta daraja limevunjika ilikuwa ni kawaida kabisa kipindi cha masika na ikitokea hivyo mnaweza abiria mkapiga kambi sehemu hata siku mbili mkisubiri daraja litengenezwe au mkatafute njia nyingine.

Hapo mnakaa na kuzoeana kama wote mnafahamiana. Wale wakware hapo wanakamata mabinti na kupotea nao maporini kwa muda kadhaa wakirudi wanaendelea kupiga story n.k

Milima maarufu ilikuwa ni mlima nyoka, sekenke na kitonga.
Ilikuwa si jambo la kushangaza kusikia bus limeshindwa kupanda mlima au limerudi baada ya kukosa nguvu kupanda mlima.

Kondakta alikuwa mtu muhimu sana miaka hiyo na aliheshimika sana maana kama dereva akimkwaza kondakta na kondakta akaamua kuahirisha safari basi mnaweza msiondoke maana kondakta alikuwa anashikilia kigogo flan kinatumika kama brake wakati mwingine milimani.

Pia alihusika sana kumwelekeza dereva apite maeneo gani kwenye madimbwi makubwa ili msikwame. Haikuwa ajabu kuambiwa mshuke kwanza gari lipande mlima likifika juu mnapanda tena kuendelea na safari yenu.

Kutumia week au siku 5 kwenda mwanza ilikuwa jambo la kawaida kabisa. kipindi hicho abiria wanasafiri na kuku, njiwa na vyakula kibao tu ili ikitokea dharura watu wapige kambi.

Nakumbuka ilikuwa tukitoka Dar kwenda mkoani lazima apeleke zawadi ya mikate...na utakuta bas lililotoka Dar limepambwa ndani kwa mikate inayoning'inia madirishan na kwenye siti kwa ajili ya kupeleka zawadi mkoani.

Njiani tulikutana na changamoto nyingi kama bus kuharibika, barabara kufunga, kutekwa na majambazi, kuishiwa mafuta n.k.
Safari zilikuwa miaka ile siyo sasa. Kwa sasa hata hufurahii dk chache tu mara upo Mwanza, mara upo Mbeya, mara upo Arusha, mara upo Mtwara.

unakumbuka safari gani utushirikishe uzoefu wako njiani miaka ile ya nyuma?

Hizi ndo zilikuwa Bus zetu.
View attachment 535242 View attachment 535243 View attachment 535244

NA HIZI NDIZO BUS ZENU
View attachment 535247
View attachment 535248 View attachment 535249
Ofisi sana we jamaa.
Safari ya Dar kwenda Mwanza halafu umepita Kitonga?
Na basi ya Railway?

Anyway kwa wasiojua, umeandika hadithi nzuri!
 
Nimesafiri Dodoma to Iringa kupitia Mtera na King Cross Bus safari ilikua ni ua siku nzima siku hizi na masaa matatu .
 
Back
Top Bottom