Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

WAKUU PM WAMEKUJA WATU WENGI ISHU YA COPY YA KITABU CHA GAMBOSHI WAPO NIMEWATUMIA ILA PIA KUNA AMBAO WANAHITAJI NAMBA YA ZABRONI NI HII (0628638308) HII NAMBA MPIGIE SIO MESEJ NI NGUMU KUJBU NASISITZA MPIGIE KWA WANAO HITAJI KITABU CHAKE CHA GAMBOSHI
 
MKASA WA PILI - Sehemu ya 20

Inaendelea.............

Niliondoka hapo geto kwangu nikiwa nimejianda kikamilifu kwa ajili ya kuelekea Shinyanga,Nilifika maeneo fulani hv panaitwa Tinde,pale Tinde kuna njia moja ilikuwa ikielekea Kahama.
Sasa kabla hujafika kahama hapo katikati huwa kuna ka mji kanaitwa Isaka,Tukio nililoenda kupiga siku hiyo ilikuwa katikati ya Tinde na Isaka!

Nilipofila pale nilianza kuangalia magari yanayopita pale!,Nilikuwa nina uwezo wa kuliona gari lote na uwezo wa abiria waliokuwemo!,Kama hilo gari lilikuwa limebeba watu waliokuwa wamejizindika nilikuwa nina achana nalo!

Sasa hapa labda nieleze kidogo!,Iko hivi,Mara nyingi mshirikina yeyote au mchawi akimuona mtu hata kama analindwa na Mungu yeye kwa akili yake anajua huyo mtu atakuwa na dawa kali kuliko zake!
Hiyo hali na mimi nilikutana nayo kwenye baadhi ya magari na kiukweli nilikuwa ninaachana nao maana nilijua naweza kupata majanga!
Nilipokaa kwa muda mrefu kidogo yale maeneo niliona kuna Gari aina ya Noah lilikuwa linakuja kwa kasi sana!,nilipopiga darubini yangu niliona waliokuwa ndani ya hilo gari walikuwa emptiness(Hawakuwa na chochote ambacho kingenizuia mimi kufanya tukio).

Basi kuna tego nililiweka pale Barabarani na gari ilipofika yale maeneo ilikula mzinga wa maana na palepale walikufa watu 3,Ndani ya lile gari kulikuwa na Mwanaume na mwanamke wamekaa mbele na nyuma kulikuwa na abiria kama 5 hivi,kwa muonekano wa lile gari nadhani wale wa Mbele walikuwa ni mke na mume ambao walionekana kabisa ndiyo wamiliki wa lile gari wale wengine nadhani walikuwa tu abiria ambao walikuwa wamewachukua njiani ili kupata hela kidogo!
Nililisogelea lile gari na nikachukua kibuyu kile na kuanza kuweka damu!,Nilihakikisha siachi hata tone la damu na wale ambao niliwakuta hai nilihakikisha nawanyonya damu yote kiasi kwamba hata wangepelekwa hospitali wasingefika kabla hawajafa!,Na hivyo ndivyo ilivyokuwa!

Nilipomaliza zangu kufanya kilichonipeleka niliondoka yale maeneo pasipo kuonekana na yeyote!
Nilipofika geto kama kawaida nilichukua kile kibuyu nikakiweka chini ya uvungu na mimi nikaondoka zangu kupiga mishemishe zangu za ualimu!
Kwa wakati huo nilikuwa ninapiga pamba kali na nilikuwa nina pendeza sana na isingekuwa rahisi kwa mtu yeyote kujua ninachokifanya!

Sasa pale shuleni nilipokuwa nikifundisha kama kuzuga ili nionekane nina kazi,kuna demu mmoja alikuwa Mwalimu ameajiriwa,kumbuka mimi nilikuwa mwalimu temporary mpaka wakati huo!
Yule Maalimu alikuwa mzuri sana na alikuwa na maringo sana,kuna wakati unaweza kumsalimia na asikuitikie kisa tu alikuwa mzuri na wengine tulionekana vibaka tu,Kwa wakati huo alikuwa na gari ambayo inasemekana alinunuliwa na jamaa yake ambaye tuliambiwa alikuwa na mshiko!
Alikuwa na kigari fulani hivi kinaitwa Duet,nadhani kalikuwa kametengeneza na kampuni ya Toyota kama sikosei!

Nilijiapiza ya kwamba wikiendi itakayofuata,yaani ndani ya wiki hiyo lazima atanitambua maana nilisema lazima nimkung'ute shipa la maana!
Basi baada ya vipindi nilirudi zangu nyumbani na nilipofika nilikuta kama kawaida begi lile limejaa pesa na nkaanza kuzihesabu mara hii zilikuwa kama milioni 15,Nilizitoa kwenye Begi na nikaziweka kwenye sanduku moja ambalo ndo nilikuwa natunzia hela na lile begi nikalirudisha uvunguni!
Wakati huo kwakuwa ndo kwanza mwezi ulikuwa umeanza nilikuwa nimelipwa vi-hela vya kazi yangu hiyo niliyokuwa naifanya!

Kiukweli nilikuwa sioni faida yeyote ya ile hela kwa wakati huo maana nilijiona kama ni pesa ninayo ya kutosha hivyo kule nilienda tu kufanya kazi kama geresha tu!
Sasa niliamua kulivalia njuga suala la yule Maalimu aliyekuwa na maringo,Kuna dawa nilitengeneza hapo ndani na nikaiweka mfukoni nikaondoka zangu!

Ndugu zangu kwa ile dawa hakukuwa na kiumbe yeyote anayeitwa mwanamke ambaye alikuwa anachomoa,sema mimi na wanawake ilikuwa ni mbalimbali ila nilikuwa na dili na wale tu waliokuwa na nyodo na dharau!
Nilipofika shuleni niliendelea na shughuli zangu kama kawaida na nilipopata wasaa wa mapumziko nilimfata yule demu aliyekuwa kaumbika kila idara,nikamsalimia na aliitikia siku hiyo kwa uchangamfu kama wote!
Nilimuomba baadae atakapotoka taka kuondoka anipe lift na akakubali akasema "Ondoa shaka".
Sikuwa na wasiwasi maana nilijua huyu tayari ni wa kwangu!
Baadae nilipomaliza kufundisha kama kawa ilibidi nimsubiri na alipomaliza tuliondoka zetu akanibeba kwenye hicho kigari chake!

Tukiwa ndani ya gari sikutaka kupoteza muda nilimgusa mkono na palepale alisema "leo naenda kulala kwako", Nilimuuliza "Kwanini"?,Akaendelea kusema "Huwa nakupendaga muda mrefu sema hujuagi tu",nilitambua tayari kitu kimeshatiki! Kwa maana alikuwaga hanaga muda na mtu hasa ukizingatia kipindi kile nilikuwa nimechoka na isingekuwa rahisi kupendwa na mtoto mzuri kama yule!
Kwakuwa hapo kwenye hiyo nyumba niliyopanga kulikuwa na geti hivyo kuliwezesha lile gari lake kupata nafasi ya kupaki!
Ilikuwa mida ya jioni na wapangaji wenzangu walikuwa wakishangaa namna nilivyokuja na yule demu mkali,wengi walishangaa maana hawakuwahi kuniona pale nyumbani na demu yeyote!
Tulipofika nyumbani nilimwacha mi nikaelekea zangu kununua nyama ya kuchoma na viazi vilivyokaangwa(chips)nikamletea!
Mle ndani kwangu nilikuwa najitahidi kupaweka safi maana sikutaka yeyote afahamu kilichokuwa kinaendelea na nilihakikisha kile kibuyu nimekificha kimazingara hakuna yeyote aliyekiona ila mimi tu!

Kiukweli usiku huo yule mwanamke hatokuja kuusahau maana nilimkung'uta shipa la ki-mkakati na namna alivyokuwa mzuri nilihakikisha hatonisahau!
Asubuhi kulivyokucha alikataa kuamka kabisa na akasema kama nikufukuzwa kazi basi afukuzwe ila pale aondoki maana hajawahi kukutana na mwanaume kama mimi!,Nilimsihi sana tuende kazini lakini aligoma katakata!
Basi siku hiyo nzima tulichapana mle ndani bakora za hali ya juu na kiukweli nilikuwa sichoki maana nilikuwa nina uwezo huo!,Nilimchapa bakora sana na alishindwa kuamka kabisa akawa kama mgonjwa siku nzima hiyo!

Kuanzia hapo nilimtengenezea dawa yaani amsahau yule jamaa yake na aniwaze mimi tu lakini baadae nilikuja kuona anaweza kuwa mwendawazimu maana alikuwa kama kachanganyikiwa kwa ajili yangu!,Nililegeza kidogo na akawa anaenda kwake kama kawaida ila nilipomuhitaji nilimpata kwa wakati niliotaka mimi!

Yule jamaa wa Igoma mwenye nyumba alinipigia simu na akawa ananikumbushia kuhusu kile kiasi kilichokuwa kimebaki na nilimwambia ndani ya siku mbili hizo nitampa!
Kwenye begi nilikuwa nina milioni 15 hivyo pungufu ya kumpa mzee ilibaki milioni kumi na tano nyingine!,Na kwa wakati huo haukuwa mwisho wa Mwezi ambapo niingeenda kufanya tukio!
Basi nilimshawishi yule demu ticha amwambie mumewe ampe milioni kumi na tano,Kuna kitu nilitamka pale kwenye mkono wangu wa kushoto uliokuwa na ile Irizi ya kwamba amuombe yule bwana yake hiyo milioni kumi na tano aniletee na asihoji chochote!
Hivyo ndivyo ilivyokuwa!,Yule mwanamke alionekana sana kuchizika na mimi laki sikutaka iwe hivyo sana maana niliona ntampoteza!
Baada ya siku hizo nilizomuahidi mzee kweli nilimpelekea ile hela na kutakaandikishiana pale na nkakabidhiwa ile nyumba rasmi!

Kiukweli lilikuwa bonge la nyumba la kisasa na nikaona litanifaa sana kwenye shughuli zangu!
Hivyo nilijisema kwamba ikifika mwisho wa mwezi nikienda kupiga tukio pesa nitakayo ipata nitanunua kila kitu cha ndani na kuhamia huko Igoma.



Itaendelea...................
Duh aiseee...
 
🅾🅷🅾🅾🅾 🅹🅰🅼🅰🅰 🅺🅰🅸🅽🅶🅸🅰 🅼🅸🆃🅸🅽🅸..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom