Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Nimeishia sehemu bwana mkubwa alipohamishia stori telegram, vp ndio kusema haijaendelea jf mpaka hapa. Mimi natumia tecno kitochi haisapoti telegram.
 
Nimeishia sehemu bwana mkubwa alipohamishia stori telegram, vp ndio kusema haijaendelea jf mpaka hapa. Mimi natumia tecno kitochi haisapoti telegram.
Huko sio kwa kwenda labda kama una ishu zako huko utakutana na maudhi tu sasa hivi anabembelezwa kuweka story na buku kala
 
Kuna aliye walazimisha kusoma uzi wake? Yani buku linawatoa jasho kiasi hicho? Ngoja nikakulipie
Buku sio tatizo hata ingekuwa zaidi ila tunauzoefu na mambo hayo story mara nyingi ikishaenda kwenye magroup wachangiaji huanza kumbembeleza mleta story ndicho kinachotokea huko na mlioko huko nasikia hamuwezi kulalamika poleni sana
 
Buku sio tatizo hata ingekuwa zaidi ila tunauzoefu na mambo hayo story mara nyingi ikishaenda kwenye magroup wachangiaji huanza kumbembeleza mleta story ndicho kinachotokea huko na mlioko huko nasikia hamuwezi kulalamika poleni sana
Kwahiyo kuna kipiki piki posta yupo kule anakùletea maswala ya kule?? Vipi unamlipa huyo mbeya mwenzio??
#FOOLISH AGE
 
MKASA WA PILI - Sehemu ya 14

Inaendelea.............

Tuliendelea na safari kwa muda mrefu na kwakuwa ilikuwa mchana niliendelea kulishangaa ziwa Tanganyika namna lilivyokubwa na kwa upande wa Kongo kiukweli kulikuwa na misitu mikubwa sana!
Ile nchi ya Kongo ilibarikiwa sana kuwa na uoto wa Asili na kijani kibichi!

Kwenye lile boti kulikuwa na vijana 5 lakini mmoja wao ambaye ndiye niliyemlipa kile kiasi cha fedha ilionekana kama ndiye Bosi wa ile Boti,Ile boti ilikuwa ni boti fulani tu la mbao lakini lilikuwa limepachikwa injini lakini ilikuwa kubwa!,Nilimuuliza jamaa itatuchukua muda gani mpaka kalemii,Jamaa akanambia kama masaa 3!
Basi kweli,baada ya Masaa 3 tulikuwa tumefika kalemii!,Kiukweli ule mji wa kalemii ulikuwa mkubwa sana kama vile kigoma tu!,

Kwakuwa mimi safari yangu haikuishia pale nilimuuliza jamaa aniambie namna ya kufika kwenye kijiji cha Kirungu!,Jamaa alishangaa sana "Kirungu unaenda kufanya nini"?
Nilimwambia kuna shughuli inanipeleka kule!
Jamaa alinambia Kijiji cha kirungu kiko mbali kutoka hapo kalemii na endapo nikitumia Usafiri wa pkpk itanighraimu pesa nyingi,pia kupita maporini huko kuna uwezekano kukutana na waasi wakanifanya kitu mbaya !

Yale maeneo tuliyokuwa tumetia nanga yalikuwa nje kidogo ya Bandari ya kalemii kwasababu inaonekana wale jamaa walikuwa wanafanya Biashara za magumashi hivyo walikwepa mkono wa serikali!
Jamaa aliniambia hiyo kirungu ipo kusini mwa Kalemii hivyo ningepaswa kutumia njia ya maji ili iwe rahisi mimi kufika huko!,Jamaa aliendelea kunipatia maelekezo pale kwamba Kabla ya kufika Kirungu kuna Bandari bubu inaitwa Moba,sasa nikishafika hapo Moba nitatafuta bodaboda za kunipeleka Kirungu maana ukitoka hapo Moba kwenda Kirungu si mbali!

Aliniambia sasa hapo Kalemii itabidi nikutafutie bodaboda akupeleke ng'ambo ya pili kuukwepa mji halafu kuna njia ya kurudi tena ziwani kwa ng'ambo ya kusini!,Utakapofika huko lazima utazikuta boti za kwenda Moba,na ukifika Moba ni kama umefika Kirungu!

Basi nilishuka pale nikatafuta Boda maeneo yale na nilimpo mpata nilimwambia jamaa amwelekeze namna nilivyo mwambia!,Yule jamaa alimwambia "Mpeleke huyu jamaa kwenye Boti za kwenda Moba",Yule Boda aliniambia nimpe faranga 3000!
Tuliondoka zetu kupita mitaani ambako alikuelewa yeye,Ule mji ulikuwa umechangamka sana nami kawa kawaida niliendelea kushangaa mitaa hiyo ya kalemii,Baada ya muda si mrefu jamaa alifika maeneo ya ziwani kwa upande wa kusini!,alielekeza kulikuwa kuna maboti ya mbao kibao yamepaki pembeni mwa ziwa!

Niliachana na yule jamaa wa Boda boda pale mi nkaelekea kutafuta usafiri wa boti unaoelekea huko Moba!
Kuna jamaa mmoja nilimkuta pale anafuma nyavu za samaki na nikamsalimia!,Jamaa alionekana kama kiswahili anakijua vyema na nilimuomba anielekeze wapi ambapo ningepata usafiri wa kwenda Moba!
Jamaa aliniambia mara nyingi usafiri wa kwenda Moba unategemeana na mizigo ya kwenda huko ila kama hakuna mizigo inakuwa ngumu sana kwenda huko labda nipite barabarani!

Nilianza kuishiwa nguvu pale maana sikutaka kupita barabarani kwa maana sikuwa na pasipoti na ukizingatia ile nchi ya Kongo kulikuwa na mambo ya Waasi,hivyo nilijua inaweza kuniingiza matatani!
Jamaa aliniambia kwanini nisikodi mtumbwi unipeleke Moba?,Nilimuuliza gharama za kukodi mtumbwi mpaka Moba ni kiasi gani?,Jamaa aliniambia ni namna nitakavyoelewana na mwenye mtumbwi!

Basi nilimwambia yule jamaa aniulizie kukodi mtumbwi mpaka Moba ni kiasi gani kwa wale wavuvi wenzie!
Kuna jamaa alikuja pale tukaanza kuelewana nae na alikubali kunipeleka ila nimlipe faranga 40000/=,nilimlipa ile hela nami nikabaki mfukoni kama na faranga 38000/=,Hizi faranga nilizobaki nazo ni zile nilizochenji Kule kigoma na nilikuwa na pesa za kitanzania kama 202000/=

Kabla ya kuondoka maeneo hayo nilimuomba jamaa anielekeze maeneo ya kupata chakula maana nilikuwa nina njaa sana!
Muda huo ilikuwa kama saa 8 mchana!,Jamaa alinichukua mpaka kwenye banda moja lililokuwa jirani nikakuta wanauza vyakula kadhaa wa kadhaa,Mimi niliagiza wali samaki,Nilipomaliza kupata msosi nilishusia na maji na nikamlipa yule mama pale kama faranga 2000/= nikaondoka zangu!

Jamaa alimchukua rafiki yake mwingine hivyo kwenye ule mtumbwi tukawa watu 3,mimi nilikaa katikati na kibegi changu halafu wale jamaa mmoja alikaa nyuma na mwingi mbele wakaanza kupia makasia!
Tuliyakata maji kwa umbali mrefu sana na mida ya saa kumi na moja tukawa tumefika pale Moba,Nakumbuka Jamaa alinielekeza kwamba nikifika hapo moba nitafute usafiri wa kunipeleka Kirungu maana si mbali!
Nilitafuta usafiri pale Moba nikafanikiwa kupata na safari ya kuelekea kirungu ilianza!
Wakati tukiwa njiani nilijaribu kumuuliza yule jamaa wa boda boda kama anamfahamu mganga maarufu maeneo hayo ya Kirungu anafahamika kama Nchibaronda!
Jamaa aliniambia alikuwa akimfahamu na atanipeleka mpaka kwake maana alikuwa anakaa nje ya mji wa Kirungu huko milimani maporini!

Baada ya mwendo mrefu tuliingia hapo mjini kirungu,Kiukweli mimi Kongo nilipapenda kwasababu kila mji ulikuwa mkubwa na ulikuwa na huduma zote mpaka usafiri wa Anga,yaani unakuta mji ni mdogo tu lakini mpaka una kiwanja cha ndege tofati kabisa na Tanzania ambapo viwanja vya ndege ni kwenye miji mikubwa ambayo ni makao makuu ya mikoa lakini kongo ilikuwa tofauti kidogo!
Tuliikamata barabara ya kuelekea huko milimani kwa Nchibaronda na haikuchukuwa muda mrefu tukawa tumefika pale!

Nilimlipa jamaa pesa tuliyokuwa tumekubaliana na akanielekeza kwa Mzee Nchibaronda!,Nilitembea kidogo maana haikuwa mbali na pale Boda aliponiacha!
Nilipofika hapo kwa huyo mzee nilipokelewa na mama mmoja na nilikaribishwa kwa lugha ya kilingala "boyei bulamu"
Boyei bulamu alimaanisha "Karibu",sasa kwakuwa mimi nilikuwa sielewi kilingala na kifaransa nilimwitikia kwa kiswahili "Ahsante"
Nilipokuwa huko kuna maneno baadhi ya lugha ya kilingala nilikuwa nimeshayaelewa hivyo sikupata taabu sana!

Baada ya kuwa nimekaribishwa niliambiwa nikae hapo nje maana mtaalamu (Mganga)kuna watu kaenda nao polini kuwaagua!
Hiyo ilikuwa mida ya saa 12 jioni mpaka nafika pale!
Kiukweli nilikuta kuna watu wengi kidogo na kuna jamaa kama wawili walikuwa wametoka Tanzania,nilipowaona nilijua tu hizi njema ni kutoka Bongoland maana mbongo anafahamika tu hata mkikutana nae nchi za watu!
Niliwasalimia na kwa bahati nzuri walinionyeshea ushirikiano,mmoja alikuwa mnene alionyesha alikuwa na maisha mazuri,basi hatukupiga sana stori maana niliona kama wana nikwepa ile kiaina!

Kwenye hilo eneo la Mganga Nchibaronda kulikuwa na vijumba vingi vya nyasi vilivyokuwa vidogo vidogo!,kama kawaida ya pale pia ulipofika usiku walikoka moto tukawa tunaota pale nje!
Ilipofika mida kama ya saa 2 Usiku yule Mzee Nchibaronda alifika na Alisema wageni waitwe waingie mmoja mmoja,sasa kwakuwa mimi kuna watu niliwakuta pale ilibidi waanze wao!,Zamu yangu ilifika ilikuwa kama mida ya saa 4 za usiku!,Nilipofika ndani nilimsalimia yule Mzee na kabla ya kuongea nae chochote nilitoa kile kingozi kilichokuwa kimekazwa kama kijiti ambacho nilipewa kule Kasulu na yule Mama akiambia ile ni rufaa ya mimi kwenda pale!

Mzee Nchibaronda alikipokea na akaniambia alifahamu ninakuja na alikuwa akiniona kila hatua niliyopiga,Yule Mzee aliniambia hata kabla sijamweleza chochote mimi pale nimefata utajiri na nitaupata!
Aliniuliza "JE UTAWEZA"?,kwakuwa nilikuwa nimedhamiria nilimwambia "Nitaweza"
Mzee Nchibaronda aliniambia hakuna aliyefata hapo kwake utajiri na akashindwa kufanikiwa kwani wote wanafanikiwa,Aliendelea kuniambia kwamba hata hao watanzania niliowakuta hapo nje wamekuja kumlipa shukurani baada ya kufanikiwa kwenye shughuli zao!

Baada ya mazungumzo mle ndani aliniambia kwakuwa kazi yangu ilikuwa ngumu kidogo alinitaka nikae pale wiki nzima maana kuna safari ya kwenda ziwa Tanganyika ambako huko ndiko nitapatiwa utajiri,na akaendelea kusisitiza kwamba yupo atakayenipa Utajiri ila siyo yeye!,Yeye kazi ambayo angeifanya ni kuniandaa ili safari ya kwenda Ziwani itakapofika nisije kupata madhara!


Itaendelea................

Piga namba hii kwa ajili ya maswali na maulizo yoyote 0757453320
.
 
MKASA WA PILI - Sehemu ya 18


Inaendelea.............


Asubuhi kulipokucha nilijianda na nilimuaga Mzee Nchibaronda na kuondoka!
Yule Mzee Nchibaronda nilimwachia shilingi laki moja ile ya kitanzania pamoja na kiasi kidogo nilichokuwa nacho cha faranga!

Mzee usiku alikuwa ameniambia kwamba siku nitakayofanikiwa inabidi nirudi kumpa shukurani maana shukurani huwa ni lazima!

Kwakuwa wakati huo nilikuwa nina uwezo wa ajabu kutokana na ile irizi niliyowekewa mkononi kuna jambo nilifanya pale si la kawaida!,Nilitamka ya kwamba "Ninataka muda huu niwe ziwa Tanganyika",na kweli nilijikuta nipo ziwani kwa upande wa kongo!.
Kiukweli nilijiona kama nina bahati kuliko binadamu wote walioko kwenye hii sayari ya dunia!
Nilitembea hapo ufukweni kuelekea kaskazini mwa Congo na muda si mrefu nilifika pale kwenye Bandari ya Kalemii!,Bado nilikuwa sielewi ule uwezo wa kutembea kwa haraka ulitoka wapi lakini yawezekana ilikuwa ile Irizi ya malikia!

Nilipofika pale Bandarini nilikuta Boti nyingi za kisasa na niliuliza pale boti inaelekea kigoma nikaonyeshwa!,nipofika kwenye hiyo boti nilipanda na kuingia ndani na hakuna aliyeweza kuniuliza kuhusu nauli maana nilikuwa ninatamka tu na inakuwa!
Huu mtindo wa kusafiri bila nauli ndo yalikuwa maisha yangu siku zote tangu nilipotoka huko chini ya maji!
Ile boti haikuchukua muda sana ilianza safari kuelekea kigoma na masaa kadhaa ikawa imetia nanga bandari ya kigoma!

Nilipofika kigoma nilijaribu kumtafuta yule jamaa wa Mwanza kwenye simu lakini alikuwa hapatikani,Baada ya kumkosa jamaa nilijaribu kumtafuta mama na alipopatikana tulisalimiana na akaniambia wao wanaendelea vizuri!,Mama aliniuliza "Kwani ukowapi wewe?,mbona hujaja nyumbani takribani wiki mbili?"
Nilimwambia mama "Nitakuja kesho maana nilikuwa bize kuna kazi nilikuwa naifanya"
Baada ya mazungumzo na mama nilielekea hapo kigoma nikatafuta hotel kwa ajili ya kupata msosi!

Baadae nilitafuta hotel maeneo ya hapo kigoma kwa ajili ya kupumzika ili kesho nianze safari ya kuelekea Mwanza!
Usiku huo nilikuwa nawaza namna nitakavyokuwa tajiri na namna ya kufanya watu wasigundue utajiri wangu kuwa niwa kishirikina!
Kulipokucha Asubuhi nilielekea kupanda basi lililokuwa linaelekea Mwanza na kama kawaida nilipanda bure sikuweza kulipa nauli!

Wakati huo mrume ndago nilikuwa nina jeuri na kiburi kisichokuwa na mfano,maana niliona mimi ndiyo mimi na kwamba hakuna mbwa yeyote wa kunibabaisha!,
Kama kawaida Mwanza tuliingia mida ya usiku!
Nilipofika hapo stendi ya Nyegezi nilipanda bodaboda mpaka Geto kwangu!,Kwakuwa ile nyumba tuliyokuwa tumepanga ilikuwa na geti niligonga na kuna jamaa mmoja alikuja kunifungulia!
"Mwanangu mambo vp",jamaa alinisalimia,nkamwambia" poa kaka"
"Ulikuwa wapi kaka maana nilijaribu kukuulizia lakini kila mtu hakuwa na jibu"jamaa aliendelea kuniuliza!
Nilimwambia "Nilisafiri kidogo kaka,siunajua tena utafutaji?"

Basi nilielekea chumbani kwa yule jamaa ambaye tulienda nae kasulu maana nilikuwa nimempa funguo zangu anitunzie!,Nilijaribu kugonga akafungua lakini ilikuwa sura ngeni machoni kwangu!
Alikuwa mwanamke na mimi nilidhani uenda angekuwa mwanamke wa jamaa lakini kumbe kulikuwa na mpangaji mpya kwenye hicho chumba!
Nilimuuliza "Vp jamaa kalala",Yule dada aliniambia "jamaa yupi"?,Aliendelea kuniambia yeye hapo kahamia ana kama wiki mbili hivi!.
Nilimuomba samahani sana maana nilijua uenda ni mwanamke wa jamaa na nkamwambia hapo mwenye chumba alichohamia kulikuwa na mpangaji ambaye nilimwachia funguo za chumbani kwangu maana mimi nilikuwa nimesafiri!

Yule dada aliniambia nijaribu kuwauliza wapangaji wengine maana yeye hafaamu kitu chochote!

Nilienda kumgongea yule jamaa aliyenifungulia nikijaribu kumuulizia labda jamaa atakuwa kamwachia funguo!,Jamaa akasema "Hapana sikuachiwa funguo"

Kuna jamaa mmoja yeye shughuli zake zilikuwa za viwandani huko Igoma na uenda nadhani jamaa ndo alimwachia funguo!
Niliona isiwe taabu sana!,Nilielekea chumbani kwangu na niligusa kile kitasa kwa mkono wa kushoto ulokuwa na ile irizi na ukafunguka nikaingia ndani!
Kiukweli sikutaka mtu yeyote lile tukio alione na ndo maana nilijaribu kuutafuta ufunguo wangu na kwakuwa ilishakuwa usiku sikuwa na namna ingawa hakuna aliyeona nafanya nini!
Asubuhi jamaa alipokuja kutoka shift huko kiwandani alishangaa kunikuta nafanya usafi ndani kwangu!

"Aisee mambo vp"?,Umerudi lini"?,yalikuwa ni maswali aliyoniuliza,Nilimjibu nimefika jana usiku!
"Ulikuwa na funguo nyingine nini!,maana jamaa aliniachia funguo zako",Nilimwambia "Ndiyo nilikuwa na funguo moja maana hii niliyompa jamaa naiachaga kama dharula"

Nilimuuliza jamaa kahamia wapi?,Jamaa aliniambia Yule mshikaji tuliyeenda naye kasulu kahamia Kahama mkoani shinyanga maana jamaa anasema alimwambia kuna chimbo la dhahabu kalipata hivyo aliona aachane na ile kampuni ya Ujenzi aelekee mgodini kutafuta mali!

Tuliendelea kupiga stori pale na jamaa na akanipatia ule ufunguo wa chumba changu mi nikaendelea na mambo mengine!
Nilipomaliza kufua nguo nilijilaza ndani nikiwa nawaza namna ya kuianza ile kazi maana niliambiwa nijitahidi ndani ya mwezi huo mwishoni damu iwe imepatikana!

Niliamka na kujianda na kuelekea nyumbani kwa Bi mkubwa na nilipitia sokoni nikanunua matunda na vyakula baadhi nikawapelekea!
Nilimkuta Bi mkubwa pale na nikamsalimia na mambo mengine yakaendelea!

Baadae niliwaaga nikaondoka zangu kurejea geto kwangu!

Siku zilizidi kuyoyoma na nilikuwa na wazo sasa la kuanza kazi rasmi!
Kumbuka niliambiwa nihakikishe kuna chumba maalumu nilichokitenga kwa ajili ya kukiweka kile kibuyu alichonipa Mzee Nchibaronda baada ya kufanya tukio na kiwe na damu!

Hiko kibuyu kilikuwa ni kidogo sana kwa muonekano wa kawaida lakini kilikuwa na uwezo wa kujaza damu kama lita 200 kwa wakati mmoja!,Na kwa kawaida ulikuwa huwezi kukinyanyua mpaka uwe na nguvu za ziada kama nilizokuwa nazo mimi!

Baada kama ya siku mbili nakumbuka ilikuwa mida ya saa tatu usiku nilielekea mitaa ya bugando na kuna ajali niliisababisha ya bodaboda ambapo waligongwa na lori mpaka vichwa vikasagika kabisa!,Nilienda pale na kibuyu changu na nikaweka damu yao wote bodaboda na abiria wake na sikubakiza hata tone la damu maana kuna dawa nilichanganya na nilipofika hapo ilivuta damu zote kwenye ile miili hakikubaki kitu!
Tukio hilo nililifanya pasipo kuonekana na mtu yeyote yule!

Wakati nafika Mwanza nilienda kuitafuta ile miti ya dawa na kuivuna na kuihifadhi ndani,pia kuna dawa nyingine nilitoka nazo kongo pia kuna miti ya dawa baadhi nilienda kununua kwenye maduka ya dawa za asili!

Basi baada ya kuwa nimeiweka ile damu kwenye kibuyu nilielekea nyumbani n nilipofika nilikiweka kile kibuyu chini ya uvungu!
Asubuhi nilipoamka nilikiangalia na sikukuta damu yoyote ndani!nikajua tayari wazee wa kazi watakuwa wamekuja wamechukua chakula chao!
Siku hiyo nilisikia sauti ikinielekeza kwamba nielekee maeneo ya Nyegezi maeneo ya hapo stendi kulikuwa na sheli(kituo cha mafuta),Nisingependa kukitaja jina!
Ile sauti iliniambia kwamba nikifika hayo maeneo kuna dada atakuwa kashika hela na nisiwe na wasiwasi nimsalimie kisha atanipa hizo hela !,Niliambiwa yeye atakuwa anaona ameshika hela kumbe kashikilia gunzi la muhindi!

Nilifanya kama nilivyoagizwa,nilipofika nilimsalimia maana nilimfahamu tu kwa kumuona!,Baada ya kumshika mkono na kumsalimia alinipa pesa zote alizokuwa nazo na yeye alikuwa kashika gunzi la muhindi akidhani pesa!
Nilipozihesabu zile hela zilikuwa kama laki tatu na hamsini!
Nikarud zangu geto kwangu!,Nilipofika ndani kwangu pia kuna hela nilizikuta kitandani zilikuwa burungutu zimefungwa na rubber bendi!
Kiukweli nilifurahi sana na nilianza kuzihesabu zilikuwa milioni 2



Itaendelea.....................

Piga namba hii kwa ajili ya maswali na maulizo yoyote 0757453320
..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom