Miiko ya wafu na kaburi

Miiko ya wafu na kaburi

Usingenialika kwenye hii mada ningelia sana! Shukrani zikuendee mkuu Waterbender umeniita kunakonihusu kwa asilimia miamoja
Mengi yaliyoandikwa hapa ni kweli kabida na baadhi nina mada zake
Nimemiss Sana mada zako Kaka,japo mleta Uzi nae kaanza kurithi mikoba yako Kabla hujafa.
 
Hivi kaburi likichimbwa likanyeshewa likawa na maji inakuaje tunaweka hivo hivo au tunaahirisha
Mimi Kuna Bibi yangu alizikwa mvua imenyesha hatari maji yanachotwa na ndoo,Ila mwaka huohuo tulizika wajomba wawili wa maana,wale wajomba wenye msaada kwa familia😭 yaani hapa nimesoma ndio naunganisha dots..
 
Hapo number 12 Ina maana tutasimamisha saa kwa muda gani?

Na hapo 16,kitanda kitabaki na hizo shuka kwa muda gani?
 
Hizo ni roho mbili zinapingana, automatically moja yenye nguvu inaweza kuizidi isiyo na nguvu na kuivutia kwakwe
Wakati wa ujaUzito wa kwanza bibi yangu alifariki alikuwa mlokole sana niliweka udongo na hakuna mtu alinikataza ,nadhani ni mila na desturi hutofautiana kati ya kabila na kabila
 
Ame
Hakuna lolote ni uoga tu,hizo Tamaduni ni za wapagani tu, siye tuliyempokea YESU KRISTO, aliyeteswa kikatili na kufa msalabani kwa ajili yetu hatuna miiko yoyote.

Na hatufi hovyo hovyo,Tunaishi na kushiba wingi wa miaka na utajiri pia.

BWANA YESU ASIFIWE
Amen. Dah...pole sana
 
Habari za muda sisi waafrica tuna miiko ya mambo na vitu mbali mbali, 2010 mpaka sasa miiko imekuwa ikipuuziwa tu na wengine wakisema ni mambo ya kizamani ebu tuone, moja wapo ya miiko hiyo ni hii, lakin kutoka kwa source nilipo ipata iko zaidi ya mia tisa🤔lakin naweka michache tu na wengine wataongezea .

KARIBUNI TUJADILI WAFU😀😀😀

1. Kaburi lilisale wazi, likilala wazi, basi mwanafamilia mwingine katika familia ya marehemu atafariki ndani ya mwaka huo huo. Kaburi lizikwe siku liliyo chimbwa.

2. Vifaa vilivyo tumika kuchimba kaburi, vinatakiwa vibakie kaburini kwa siku nyingine saba. Kuvipeleka nyumbani vifaa hivyo siku hiyo hiyo au kabla ya siku saba, ni nuksi kubwa sana.

3. Kuondoka makaburini kabla kaburi lote halijafukiwa, kutasababisha msiba kwenye familia yako wewe uliye ondoka kabla watu hawajamaliza kuzika. Mvua ikinyesha kwenye kaburi ambalo bado halijafukiwa, ni ishara mbaya sana kwa familia ya wafiwa. Ili kuepukana na nuksi hiyo, inabidi kuwe na mtaalamu wa kuzuia mvua.

4. Ni nuksi kubwa sana kusonta kaburi
5. Ni nuksi kubwa sana kurukia kwenye kaburi
6. Ni nuksi kutembelea makaburini baada ya jua kuzama
7. Wafiwa wasiondoke nyumbani wala kujichanganya mtaani na watu wengine, hadi matanga yatakapo inuliwa. Kwa mfano watu wengine, unakuta mtu amefiwa, lakini kabla hata matanga hayajainuliwa, anakwenda bar kunywa na kurudi msibani. Hayo ni makosa makubwa sana.

8. Wafiwa wote wakuu, yaani ndugu wa karibu wa marehemu, wasioge hadi baada ya siku tatu, ambayo ndio siku ya kuanua matanga, na maji watakayo oga yawe maji ya moto.

9. Wafiwa wasishiriki ngono hadi matanga yatakapo inuliwa.

10. Waombolezaji msibani, wasiongee kwa nguvu wala kucheka kwa nguvu. Ni makosa makubwa sana kufanya hivyo.

11. Endapo mtu anae karibia kukata roho, atakun’gata, basi na wewe utamfuata baada ya muda mfupi. Ili kujiepusha na kifo cha namna hiyo, basi unatakiwa na wewe umng’ate katika sehemu ile ile aliyo kun’gata.
12. Kama kiongozi wa familia atafariki dunia, basi mnatakiwa kusimamisha saa kubwa ya ukutani inayo kaa sebuleni, vinginevyo wanafamilia walio baki nao watamfuata ndani ya kipindi kichache, vitatokea vifo mfululizo vya wanafamilia.
13. Baada ya kuuosha mwili wa marehemu, na kuuvisha nguo zake, unatakiwa kuweka punje moja ya chumvi kwenye kifua cha marehemu ili kuwafukuza roho na majini wabaya.
14. Kama marehemu atakuwa akiwa ameacha macho wazi , hiyo ni ishara mbaya sana. Maana yake ni kwamba,anatafuta watu ( ndugu zake ) wa kwenda nae kaburini. Kujiepusha na hilo, funikeni macho yake kwa kutumia sarafu .
15. Usifagie chumba cha marehemu kabla marehemu hajatolewa. Endapo utafanya hivyo, basi amini nakwambia wewe ndie utakae mfuata marehemu.
16. Msitoe shuka wala nguo yoyote iliyopo kwenye kitanda alicho kilalia marehemu, na ambacho umauti ulimkuta. Endapo mtakiuka hilo, basi mwanafamilia mwingine atafariki ndani ya mwaka huo huo.
17. Endapo Kundi la wanandugu, jamaa na marafiki, mtaenda kuuchukua mwili wa marehemu halafu ghafla mkaona anatoa damu kwenye tundu za pua, basi mjue kuwa marehemu amekufa kwa mkono wa mtu, na aliye husika na kumuua, yu miongoni mwenu,ndani ya chumba hicho hicho.
18. Kwa mara nyingine tena narudia, mwili wa marehemu unapotolewa kwenye jengo lolote lile, iwe nyumbani, kanisani, au msikitini ni lazima miguu ndio itangulie kutoka na sio kichwa, vinginevyo roho au mzimu wa marehemu huyo, utatazama katika jengo hilo na kumuita mtu mwingine wa kufuatana nae.
19. Marehemu azikwe mahali alipo pachagua wakati wa uhai wake, au la sivyo endapo mtaenda kinyume chake, vifo vitatokea katika familia hiyo. Na kama mtalazimisha kusafirisha mwili wa marehemu, basi msafara huo lazima utapata ajali njiani, na mtu mmoja lazima atakufa.
20. Ukiugusa mwili wa marehemu, utakuwa na uhakika kwamba, roho ya marehemu haitakusumbua. Na endapo utaugusa mwili wa marehemu usoni, hutoota ndoto mbaya kuhusu marehemu huyo.
21. Usipeleke mwili malaloni kwa kutumia gari lako binafsi. Ni nuksi kubwa sana kufanya hivyo. Mwili wa marehemu unapelekwa malaloni kwa kutumia gari maalumu.
22. Endapo mtasafirisha mwili wa marehemu kwa basi, kichwa kitazame anapotoka na miguu itazame anapoelekea.
23. Usi hesabu magari kwenye maziko (makaburini), ukifanya hivyo unakuwa unahesabu siku zako mwenyewe za kuishi.
24. Kuwa muangalifu usione taswira yako kwenye gari lililo beba mwili wa marehemu, vinginevyo wewe ndio utakae fuatia kubebwa kwenye gari hilo.
25. Usiende na mtoto mchanga kwenye msiba, vinginevyo atakufa kabla hajatimiza mwaka mmoja.
26. Ni nuksi kubwa sana kutangulia makaburini ( kwenye maziko) au kupita bila kushiriki kwenye maziko . Kama utafanya hivyo, utakufa ndani ya muda si mrefu.
27. Kama paka mweusi atakatisha mbele wakati wa maziko (makaburini ) mwanafamilia mmoja katika familia ya marehemu atakufa ndani ya siku tatu.
huyo mwingine atapata nafuu kubwa.
28. Kuna ndege mmoja anapatikana porini ( SIMTAJI KWA SABABU ZA KIMIIKO), ukichukua nyoya la huyo ndege halafu ukaliweka kwenye mto wa kitanda anacho lalia mgonjwa, basi mgonjwa huyo atakufa wala hatopona. Nyoya hilo hilo likiwekwa kwenye kitanda anacholalia mtoto mdogo, litamzuia mtoto huyo kukua.
29. Kitanda anacho lalia mgonjwa mahututi, kitazame mashariki na magharibi, na kamwe sio kaskazini na kusini. Kichwa kiangalie magharibi na miguu itazame mashariki.
30. Jina la mwisho kutajwa na marehemu wakati anakaribia kukata roho, litakuwa jina la mtu atakae fuatia kufa baada ya marehemu.
View attachment 2434580View attachment 2434581
"19. Marehemu azikwe mahali alipo pachagua wakati wa uhai wake, au la sivyo endapo mtaenda kinyume chake, vifo vitatokea katika familia hiyo. Na kama mtalazimisha kusafirisha mwili wa marehemu, basi msafara huo lazima utapata ajali njiani, na mtu mmoja lazima atakufa."


Hapo umenikumbusha kisa na mkasa wa Ajali ya Kologwe iliyo ua watu zaidi ya 19 mwezi huu
 
"19. Marehemu azikwe mahali alipo pachagua wakati wa uhai wake, au la sivyo endapo mtaenda kinyume chake, vifo vitatokea katika familia hiyo. Na kama mtalazimisha kusafirisha mwili wa marehemu, basi msafara huo lazima utapata ajali njiani, na mtu mmoja lazima atakufa."


Hapo umenikumbusha kisa na mkasa wa Ajali ya Kologwe iliyo ua watu zaidi ya 19 mwezi huu
marehemu hawana mchezo wakikwambia usifanye hichi acha kwel
 
Habari za muda sisi waafrica tuna miiko ya mambo na vitu mbali mbali, 2010 mpaka sasa miiko imekuwa ikipuuziwa tu na wengine wakisema ni mambo ya kizamani ebu tuone, moja wapo ya miiko hiyo ni hii, lakin kutoka kwa source nilipo ipata iko zaidi ya mia tisa🤔lakin naweka michache tu na wengine wataongezea .

KARIBUNI TUJADILI WAFU😀😀😀

1. Kaburi lilisale wazi, likilala wazi, basi mwanafamilia mwingine katika familia ya marehemu atafariki ndani ya mwaka huo huo. Kaburi lizikwe siku liliyo chimbwa.

2. Vifaa vilivyo tumika kuchimba kaburi, vinatakiwa vibakie kaburini kwa siku nyingine saba. Kuvipeleka nyumbani vifaa hivyo siku hiyo hiyo au kabla ya siku saba, ni nuksi kubwa sana.

3. Kuondoka makaburini kabla kaburi lote halijafukiwa, kutasababisha msiba kwenye familia yako wewe uliye ondoka kabla watu hawajamaliza kuzika. Mvua ikinyesha kwenye kaburi ambalo bado halijafukiwa, ni ishara mbaya sana kwa familia ya wafiwa. Ili kuepukana na nuksi hiyo, inabidi kuwe na mtaalamu wa kuzuia mvua.

4. Ni nuksi kubwa sana kusonta kaburi
5. Ni nuksi kubwa sana kurukia kwenye kaburi
6. Ni nuksi kutembelea makaburini baada ya jua kuzama
7. Wafiwa wasiondoke nyumbani wala kujichanganya mtaani na watu wengine, hadi matanga yatakapo inuliwa. Kwa mfano watu wengine, unakuta mtu amefiwa, lakini kabla hata matanga hayajainuliwa, anakwenda bar kunywa na kurudi msibani. Hayo ni makosa makubwa sana.

8. Wafiwa wote wakuu, yaani ndugu wa karibu wa marehemu, wasioge hadi baada ya siku tatu, ambayo ndio siku ya kuanua matanga, na maji watakayo oga yawe maji ya moto.

9. Wafiwa wasishiriki ngono hadi matanga yatakapo inuliwa.

10. Waombolezaji msibani, wasiongee kwa nguvu wala kucheka kwa nguvu. Ni makosa makubwa sana kufanya hivyo.

11. Endapo mtu anae karibia kukata roho, atakun’gata, basi na wewe utamfuata baada ya muda mfupi. Ili kujiepusha na kifo cha namna hiyo, basi unatakiwa na wewe umng’ate katika sehemu ile ile aliyo kun’gata.
12. Kama kiongozi wa familia atafariki dunia, basi mnatakiwa kusimamisha saa kubwa ya ukutani inayo kaa sebuleni, vinginevyo wanafamilia walio baki nao watamfuata ndani ya kipindi kichache, vitatokea vifo mfululizo vya wanafamilia.
13. Baada ya kuuosha mwili wa marehemu, na kuuvisha nguo zake, unatakiwa kuweka punje moja ya chumvi kwenye kifua cha marehemu ili kuwafukuza roho na majini wabaya.
14. Kama marehemu atakuwa akiwa ameacha macho wazi , hiyo ni ishara mbaya sana. Maana yake ni kwamba,anatafuta watu ( ndugu zake ) wa kwenda nae kaburini. Kujiepusha na hilo, funikeni macho yake kwa kutumia sarafu .
15. Usifagie chumba cha marehemu kabla marehemu hajatolewa. Endapo utafanya hivyo, basi amini nakwambia wewe ndie utakae mfuata marehemu.
16. Msitoe shuka wala nguo yoyote iliyopo kwenye kitanda alicho kilalia marehemu, na ambacho umauti ulimkuta. Endapo mtakiuka hilo, basi mwanafamilia mwingine atafariki ndani ya mwaka huo huo.
17. Endapo Kundi la wanandugu, jamaa na marafiki, mtaenda kuuchukua mwili wa marehemu halafu ghafla mkaona anatoa damu kwenye tundu za pua, basi mjue kuwa marehemu amekufa kwa mkono wa mtu, na aliye husika na kumuua, yu miongoni mwenu,ndani ya chumba hicho hicho.
18. Kwa mara nyingine tena narudia, mwili wa marehemu unapotolewa kwenye jengo lolote lile, iwe nyumbani, kanisani, au msikitini ni lazima miguu ndio itangulie kutoka na sio kichwa, vinginevyo roho au mzimu wa marehemu huyo, utatazama katika jengo hilo na kumuita mtu mwingine wa kufuatana nae.
19. Marehemu azikwe mahali alipo pachagua wakati wa uhai wake, au la sivyo endapo mtaenda kinyume chake, vifo vitatokea katika familia hiyo. Na kama mtalazimisha kusafirisha mwili wa marehemu, basi msafara huo lazima utapata ajali njiani, na mtu mmoja lazima atakufa.
20. Ukiugusa mwili wa marehemu, utakuwa na uhakika kwamba, roho ya marehemu haitakusumbua. Na endapo utaugusa mwili wa marehemu usoni, hutoota ndoto mbaya kuhusu marehemu huyo.
21. Usipeleke mwili malaloni kwa kutumia gari lako binafsi. Ni nuksi kubwa sana kufanya hivyo. Mwili wa marehemu unapelekwa malaloni kwa kutumia gari maalumu.
22. Endapo mtasafirisha mwili wa marehemu kwa basi, kichwa kitazame anapotoka na miguu itazame anapoelekea.
23. Usi hesabu magari kwenye maziko (makaburini), ukifanya hivyo unakuwa unahesabu siku zako mwenyewe za kuishi.
24. Kuwa muangalifu usione taswira yako kwenye gari lililo beba mwili wa marehemu, vinginevyo wewe ndio utakae fuatia kubebwa kwenye gari hilo.
25. Usiende na mtoto mchanga kwenye msiba, vinginevyo atakufa kabla hajatimiza mwaka mmoja.
26. Ni nuksi kubwa sana kutangulia makaburini ( kwenye maziko) au kupita bila kushiriki kwenye maziko . Kama utafanya hivyo, utakufa ndani ya muda si mrefu.
27. Kama paka mweusi atakatisha mbele wakati wa maziko (makaburini ) mwanafamilia mmoja katika familia ya marehemu atakufa ndani ya siku tatu.
huyo mwingine atapata nafuu kubwa.
28. Kuna ndege mmoja anapatikana porini ( SIMTAJI KWA SABABU ZA KIMIIKO), ukichukua nyoya la huyo ndege halafu ukaliweka kwenye mto wa kitanda anacho lalia mgonjwa, basi mgonjwa huyo atakufa wala hatopona. Nyoya hilo hilo likiwekwa kwenye kitanda anacholalia mtoto mdogo, litamzuia mtoto huyo kukua.
29. Kitanda anacho lalia mgonjwa mahututi, kitazame mashariki na magharibi, na kamwe sio kaskazini na kusini. Kichwa kiangalie magharibi na miguu itazame mashariki.
30. Jina la mwisho kutajwa na marehemu wakati anakaribia kukata roho, litakuwa jina la mtu atakae fuatia kufa baada ya marehemu.
View attachment 2434580View attachment 2434581
Hayo yote ni utumwa wa shetani na hayanihusu wala sishauri mtu yeyote kuyaamini na kuyafanya. Ondokeni katika utumwa huu wa Kiafrika kupitia mizimu. Hizi ni sheria za mizimu na hazina maana yoyote ni kutaka tu kumtega mwanadamu anayeamini hayo ili kummaliza, achana kabisa na imani hizi na zingine zote mbaya. Mwamini Yesu Kristo na wema wake kila kitu kitakuwa kizuri na shwari.
 
Hayo yote ni utumwa wa shetani na hayanihusu wala sishauri mtu yeyote kuyaamini na kuyafanya. Ondokeni katika utumwa huu wa Kiafrika kupitia mizimu. Hizi ni sheria za mizimu na hazina maana yoyote ni kutaka tu kumtega mwanadamu anayeamini hayo ili kummaliza, achana kabisa na imani hizi na zingine zote mbaya. Mwamini Yesu Kristo na wema wake kila kitu kitakuwa kizuri na shwari.
too slow
 
Kunyooshea kaburi kidole na kakalia kaburi au kukanyaga kaburi lisilo la ndugu, ni nuksi. Najikuta naziishi hizi kanuni bila hata ulazima.
 
Marehemu azikwe mahali alipo pachagua wakati wa uhai wake, au la sivyo endapo mtaenda kinyume chake, vifo vitatokea katika familia hiyo.

Na kama mtalazimisha kusafirisha mwili wa marehemu, basi msafara huo lazima utapata ajali njiani, na mtu mmoja lazima atakufa.

Hilo limeshawatokea wengi mno hasa watani zangu
Wachagga na ajali ya Tanga na vifo vya wanafamilia 14 ni mfano hai wa mwiko huu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom