Wakuu wa mashirika ya kimataifa wakiwemo mwenyekiti wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki Bw. Thomas Bach na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres, na viongozi wa zaidi ya nchi 30 akiwemo rais Vladmir Putin wa Russia wamehudhuria ufunguzi huo.
Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing ni michezo mikubwa ya kwanza inayofanyika kama ilivyopangwa tangu kutokea kwa mlipuko wa janga la COVID-19, na inawashirikisha wanamichezo karibu 3000 kutoka nchi takriban 90. (Picha: Xinhua)