Michezo: Mkakati Wa Kujiajiri Na Ajira Kwa Vijana Na

sharrif

New Member
Aug 19, 2008
3
0
WAKATI Tanzania kupitia Waziri wake wa Elimu miaka kadhaa iliyopita, aliyetokea Chama cha Mapinduzi ilipiga marufuku riadha na michezo mingine mashuleni hivi leo Jamaica kwa kuendeleza michezo mashuleni imewika na kuwakawaka kila pembe ya dunia.

Nchi ndogo na isiyojulikana imefanya makubwa yaliyostahili na jinchi kama letu kama tuna nidhamu ya kupanga na kufuata yale yaliyomo katika mipango yetu na hatutarajii ushindi kutokana na kelele za vyombo vya habari na mashabiki wake.

Michezo hivi leo ni kazi. Na yeyote anayezembea kutoa fursa ya vijana wetu kustawi katika fani yoyote ile ya michezo hatendei haki kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Wito wangu ni kwa Watanzania tujiangalie upya na tuanza kuwa na utamaduni wa kuanzisha programu za michezo, muziki na sanaa ili kuendeleza vipaji vya wale waliojaliwa kuwa na ustadi katika hili au lile.

Tuache ubinafsi kwa kusema kama sio mwanangu yanini niwashughulikie hao.

Na kazi hii isiachiwe tu Wizara ya Kazi na Vijana bali pia Utalli [ambao watatangazwa vijana wakishinda lolote lile]; makampuni binafsi yaliyo na kila sababu ya kuwarudishia Watanzania kile wanachokichukua hivi sasa sawa na bure; serikali za mikoa; na wafadhili ndani na nje ya nchi.

Katika hili kama nikipata wafasdhili ningelipenda niandike kijitabu baada ya kutembelea Austalia, Croatia, Jamaica, Ujerumani na Uchina. Kitabu hicho nimekipa jina la muda:

MICHEZO: Mkakati wa Kuongeza Ajira na Kujiajiri na Kuitangaza nchi!
 
Kama unavyojua sisi kina Mwalimu [na hususan kama mie Mwalimu Jr.] sina tabia ya kujilimbikizia mbaana ile nyumba yangu ya mwisho ambayo ni futi 6x3
haiwezi kuchukua yote ninayotamani kujilimbikizia. Kwa kifupi sina njia ya kukufadhili. Lakni ninafungua mlango wa mazungumzo na jamaa wote wanaohusishwa na EPA au ni HEPA wee sijui mie, ili waweze kuunda angalau kakitu katakochoitwa TANZANIA INTERNET AND HARDPRINT AUTHORS DEVELOPMENT FUND, yaani, kwa Kiswahili MFUKO WA KUSAIDIA WAANDISHI KATIKA TOVUTI NA WALE WA VITABU PIA.

Kwa hiyo Bw. Sharrif kuwa na subira na hayawi, hayawi, sasa yatakuwa. Tazama mada yangu ya awali katika uwanja huu pia ambayo inahusu masuala haya haya ya michezo na pengine utaanza kujipatia angalau aya moja moja kama sio sura moja moja kwa ajili ya kitabu chako.
 
Sikuishia hapo kwa leo ndugu zangu nikamwahi Olivia Grange, naam, yule Waziri wa Michezo wa Jamaica ambaye ameiwezesha nchi yake kufanya maajabu katika Beijing Olympic 2008:

Na zifuatazo ni nukuu za mazungmzo yetu katika messenger ya Hotmail or MS Messenger:

Mimi: Hi, Babsy? Still remember me?

Olivia: Funny, how can I forget you Sam 'cause am just a Minister. It is what I do for my people not the position that matters!

Mimi: I respect you more for that stance dear, I wish, we had Ministers like you here dear!

Olivia: You mean after Mwalimu Senior, there, are no Ministers good as Nyerere. Did not someone learn from that great man?

Mimi: They did, dear Olly, but practised the opposite!

Olivia: My, my, that's Africa for you. Can I help Sam.

Mimi: Nothing of importance really, I am blogging now in teh JamiiForums, formerly, Jambo, which was witch or warchhunted by the rulers and downundered! But here, we are all over again-the blog is a great pressure valve in the world I wish all African leaders can know that.

Olivia: So, what is it you ...

Mimi: Yes, dear, ....wanted to know what is the secret behind Jamaica's success in the Beijing Olympics?

Olivia: Secret, not really, just mere attention to basic life, work and play facts. I call them basic five Ts or something of a sort:
-TRADITION
-TRUST
-TRAINING
-TREATMENT
-TIMETABLE

You have to base sports and other talents on the traditions of your people. Find those and develop them into sports talents that can be harnessed for sports and even employment.
If you have people who chase cows and goats around teach them to run. If you have people who use spears teach them javelin and if you have those who like wrestling develop them into wrestlers and those by sea or lake sides teach them swimming and canoeing.

[We shall continue with this great talk from an able-administrator fromJamie, see you another time....]
 
Hullo Mnyika,

Mimi sidhani kama kuna pointi yoyote kuwa na SERA YA VIJANA itakayoishia kwenye makalabrasha na makabineti baada ya wana (w)izara kutafuna kiasi kikubwa cha fedha ya ufadhili.

Bwanae, kwangu mimi la muhimu ni kuwa na SERA YA MICHEZO KAMA AJIRA NA KUJIAJIRI.

Sera hii nina hakika chini ya watu kama wewe na kupata ufadhili mdogo wa nje na ndani sisi wenyewe tunaweza kuiandaa. Tusingoje walanchi kwa kazi hiyo. Sisi walia tuanze mbele kwa mbele au sio bwana?

Katika mazungumzo na Babsy, huyu ndiye waziri wa Michezo Jamaica kwa sasa kaniambia kwamba sera yake [iliyoleta mafanikio ya ajabu Beijing] imeegeshwa kwenye masuala ya T-7. T hizo ni:
-TRADITION. Tunaweza kujenga mengi kuanzia kwenye kile tulichokipokea [mapokeo] ya mila, desturi na tamaduni kama vile Wamasai wanaorusha mikuki kucheza Javelin, jamaa wa Pwani kuogelea na canoeing; Wakurya-Kick-boxing, Wasukuma -wrestiling and so on.

TRUST. Lazima wanaokuwa viongozi wa michezo na nchi wajenge kuaminiwa na kuaminiana kati yao na ngazi mbalimbali za wanamichezo na viongozi wao. Kama viongozi wanaonekana ni wababaishaji, wabakaji, wapakaziaji na waonevu basi hatutaenda mbali. Lazima wanamichezo wawaone viongozi kama ni baba na mama zao na sio vinginevyo.

TRAINING: Kinachotuua zaidi ni mafunzo. Yule mwandishi maarufu ambaye sasa ametoweka kwenye magazeti. Bw. Sammy Makilla alishawahi kuandika mada ambazo peke yake zikifanyiwa kazi nasi basi Jamaica au Kenya hazitaona ndani kwetu.Lakini nani alizisoma labda Majira izitafute na izirudie upya. Moja ninalokumbuka ni mifano aliyoiona Ujerumani ambako alikwenda na Baba mwanzilishi wa CHADEMA, Mzee Edwin Mtei nayo yalikuwa ni pamoja na 'LAUFPARKS' na vifaa vya kufanyiwa mazoezi vilivyotengenezwa kwa teknolojia nyepesi ya mbao na vyuma. Twendeni Ujerumani na hasa kule Baden Wurtenburg tukajifunze eti.

TREATMETNT- Lazima tuwatendee na kuwafanyia mazuri wanaspoti wetu sio tunapewa fedha halafu tunakwenda kuwaweka kwenye mabaa na gesti hausi na sehemu za ajabu na kuwalisha kile ambacho sisi wenyewe hatuwezi kula. Lazima tuwaenzi ili watuenzi kwa maneno mengine!

TIMETABLE-Lazima tuwe na timetable ya mwaka mzima kila mwaka ya pale tunapoanza michezo kwa kata, tarafa,wilaya, mkoa hadi Taifa na kisha kimataifa. Vinginevyo, tunachokionesha kwa wanaojua huko nje ni kuwa Watanzania wote hatuna tabia ya kupanga bali ya kupangua tu!

TEAMWORK-Lazima tujenge timu zinazoshikamana wakati wote bila kuwa na upendeleo wala uonevu wa aina yoyote katika kuwaangalia na kuwatimizia washiriki mahitaji yao ya msingi.

TARGETS OR AIMS OR OBJECTIVES OR DESIRED ACHIEVEMENTS.. Hatuwezi kushiriki wala kushinda michezo yote. Tuchague kwa makini michezo michache (sio chini ya 8) kulingana na tamaduni na uzoefu wa watu wetu ambayo tuna uhakika tukiifanyia kazi katika miaka 3 ijayo basi 2012 Tanzania itawika kwenye London Olympics 2012!
 
Back
Top Bottom