Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Kaburu: Ni mshikamano tu, tunaitoa Mazembe Send to a friend Wednesday, 30 March 2011 20:48

Sweetbert Lukonge
MAKAMU Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Godfrey Kaburu amewataka mashabiki wa klabu hiyo kushikamana na 'kuisapoti' timu yao katika mechi ya marudiano na TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo itakayofanyika Jumapili ijayo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jana juu ya maandalizi ya mchezo huo, Kaburu alisema kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha wanaibuka na ushindi katika mechi hiyo lakini umoja na mshikamano kati ya watu wote wenye mapenzi na Simba ndiyo utakaowasaidia kufanikisha hilo.

"Cha msingi kwetu sasa siyo rekodi ni kuhakikisha tunatimiza lengo la kusonga mbele katika michuano hii mikubwa Afrika kwa ngazi ya klabu kwa kuitandika Mazembe, hilo linawezekana kabisa kama kila mmoja wetu atatoa ushirikiano wa kweli.

"TP Mazembe ni timu nzuri lakini hiyo siyo sababu ya kutuzuiya tusishinde kwani katika mechi ya Lubumbashi licha ya kupoteza mechi hiyo vijana wetu walionyesha kuwa wano uwezo wa kushinda," alisema Kaburu.

Alisema mechi ya juzi ya Ligi Kuu ya dhidi ya Kagere Sugar ambayo ilimalizika kwa suluhu isiwavunje moyo mashabiki na kushindwa kuisapoti timu yao kwani hayo ni matokeo na wanachopaswa kufanya kwa sasa ni kuiunga mkono Juamapili.

Kaburu alisema: "Lengo la kila mpenzi na shabiki wa Simba ni kutaka kuiona timu hiyo inafanya vizuri kwenye mechi zake zote hivyo sare hiyo ya Kagera haiwezi kutuathiri."
 
Abbiati bemoans Leonardo switch


RivalsDM



PRINT RSS

9

Updated Mar 30, 2011 12:16 PM ET
AC Milan keeper Christian Abbiati has expressed his disappointment over Leonardo's decision to coach Inter Milan ahead of this weekend's derby.


The Brazilian will be in the Nerazzurri dug-out for the top-of-the-table clash, a season on from when he was in the opposite camp as AC's manager.
After leaving the current leaders at the end of last season, he made a surprise return to the game as Inter's boss at Christmas, and has sparked a revival of their title challenge.
"The fact that when he left he made us understand that he wouldn't be coaching the following year left me perplexed," Abbiati told Sky Italia.
"I think his passage to Inter has disappointed many Milan fans. Some of my team-mates were also hurt by the decision."
 
...Phiri awapiga mkwara wachezaji Send to a friend Wednesday, 30 March 2011 20:47

Doris Maliyaga na Clara Alphonce
KOCHA mkuu wa Simba, Patrick Phiri ametangaza hatari kikosini mwake akiwataka nyota wake kubadilika na kuwa makini ili kushinda mechi mbili walizobakiwa nazo kwenye Ligi, na kuweka wazi ndizo zitakamilisha mahesabu ya pointi wanazozihitaji kutetea ubingwa wao.

Phiri ambaye aliyerejea Jumapili kutoka Zambia alikokwenda baada ya mechi ya TP Mazembe kutokana na matatizo ya kifamilia na kukiacha kikosi chake kinachokabiliwa na mechi ngumu ya kimataifa itakayochezwa Jumapili dhidi ya TP Mazembe kikinolewa na Abdalah Kibaden ‘King'.

Baada ya TP Mazembe Simba inayoongoza Ligi Kuu kwa pointi 45, itakutana na JKT Ruvu Aprili 6 na kumaliza na Majimaji Aprili 10.Akizungumza na Mwananchi, Phiri alisema kuwa, hali imekuwa ya kiushindani zaidi na hasa timu wanazokutana nazo.

''Ligi imekuwa ngumu kila mechi ni ngumu kilichopo sasa ni kazi kuhakikisha tunashindana ili kushinda mechi hizo mbili zilizobaki,''alisema Phiri aliyedai muda waliobakiwa nao kukutana na Mazembe watahakikisha wanautumia vema ili wawafunge.

''Tunatakiwa kubadilika na kuwa siriazi ili kukamilisha malengo yetu ya kutetea ubingwa tuliyojiwekea,''aliongeza Phiri. Hata hivyo, Phiri alisema kuwa wachezaji wake hawakuitilia maanani mechi hiyo kutokana na TFF kuwa sogezea mbele mchezo huo kitu kilichowafanya wasitilie maanani mchezo huo na kuwazia zaidi mechi yao ya jumapili dhidi ya TP Mazembe ya Congo.

Alisema kitu kingine ambacho kilifanya washindwe kushinda mchezo huo wachezaji wake waliidharau Kagera na kuona kuwa ni mechi nyepesi wakati Kagera ni kati ya timu nzuri siku zote na imekuwa ikitoa upinzani mkubwa kila wanapokutana nao.

Alisema kwa akili yake anaielekeza katika mchezo wa TP Mazembe ya Congo Jumapili na michezo ya ligi iliyobaki ilikuakikisha hapotezi mchezo hata mmoja tena.

Alisema ligi kwa sasa ni ngumu sana kwani anakutana tena na JKT Ruvu ambao ni wazuri na ana maliza na Majimaji ya Songea ambao wanapigania kutokushuka daraja.
 
Uholanzi, Hispania zafanya kweli tena Ulaya Send to a friend Wednesday, 30 March 2011 20:46

LONDON, England
UHOLANZI imejiweka katika mazingira mazuri ya kufuzu fainali za Euro baada ya kuizabua Hungary 5-3 wakati Hispania iliendeleza ushindi wa Kundi I kwa kuichapa Lithuania mabao 3-1.

Hungary ilifunga mabao mawili ya harakaharaka na kuifanya timu hiyo kuwa mbele kwa mabao 2-1.

Alikuwa Wesley Sniejder aliyefunga mawili kabla ya mkongwe, Ruud van Nistelrooy kufunga lingine, lakini mchezaji wa Hungary, Zoltan Gera alifanya matokeo kuwa 3-3 ndani ya dakika 15 katika mechi hiyo ya Kundi E.

Dirk Kuyt alifunga mabao mengine mawili zikiwa zimesalia dakika 12 na kuifanya Uholanzi kufikisha pointi 18 kutokana na mechi sita, ikiwa ni pointi tisa zaidi ya Hungary na kujiweka katika nafasi nzuri ya kucheza fainali hizo mwakani.

Sweden iko nafasi sawa na Hungary baada ya kuipiga Moldova 2-1. Hispania ilishinda mechi yake ya tano mfululizo huku kiungo wake, Xavi Hernandez, akifunga bao la utangulizi.

Lithuania ilisawazisha dakika ya 57 kwa jitihata zilizosababisha Juanma Mata kujifunga. Mechi za juzi, 10 kati ya hizo ni kuwani kufuzu Euro 2012, wakati mechi zilizosalia zilikuwa za kirafiki.

Australia ilifunga mabao mawili ndani ya dakika nne na kuilaza Ujerumani mabao 2-1, huku England ikiruhusu bao dakika za lala salama na kulazimishwa sare ya 1-1 na Ghana kwenye Uwanja wa Wembley katika mechi ya kimataifa ya kirafiki.

Uruguay iliyoingia nusu fainali ya Kombe la Dunia mwaka jana, ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Ireland, huku Italia ikiifunga 2-0 Ukraine na Ufaransa ikitoka suluhu na Croatia.

Uhoplanzi, ambayo ilipata bao la kuongoza dakika ya 13 kupitia kwa Robin van Persie, iko katika mazingira ya kufuzu huku kocha, Bert van Marwijk akisema kuwa ngome imewaangusha kwa kasi fulani kuruhusu mabao.

"Inatakiwa kuwa wastahimilivu na kucheza kwa nguvu," alisema kocha wa Uholanzi, Bert van Marwijk. " mchezo ulianza vizuri, tukafunga mabao lakini mambo yakabadilika. Tulipoteza mipira kirahisi."

Uholanzi iliyoitandika Hungary 4-0 wiki iliyopita, ilishindwa kujipanga na kupoteza mipira mingi hata kutoa nafasi kwa wapinzani wao kutawala.

Hispania inayocheza pasi fupifupi za haraka, ilidai kushindwa kufanya kweli kwenye Uwanja wa Kaunas wakisema haukuwa na viwango.

"Lakini haya ni matokeo muhimu, japokuwa uwanja ulikuwa mbaya," Xavi alisema baada ya kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi wa 11 mfululizo kwa mechi zote. "Tumefikia malengo, na kuanzia hapa tunaweza kusonga mbele … timu imecheza vizuri."

Shuti la Xavi lilimgonga Andrius Skerla na kuingia wavuni na kuifanya Hispania kuongoza kwa bao la dakika ya 19 na walitengeneza nafasi nyingi kupitia kwa Fernando Llorente.

Kipa Zydrunas Karcemarskas aliokoa mpira wa hatari wa Llorente mwanzoni mwa kipindi cha pili kabla ya Marius Stankevicius alipiga shuti katikati ya msitu wa wachezaji na kusawazisha bao.

Hispania ikiwa na kiungo wake, Xavi alimchanganya beki wa Lithuania, Tomas Razanauskas na kumfanya ajifunge katika dakika ya 70. Kw amatokeo hayo, Hispania sasa ina pointi 15 ikiwa ni pointi sita zaidi ya Jamhuri ya Czech iliyoifunga Liechtenstein 2-0.

Nayo Ubelgiji iliifunga Azerbaijan 4-1 na kushika nafasi ya pili katika Kundi A ikiwa ni pointi moja zaidi ya Uturuki, iliyoifunga Austria 2-0. Katika Kundi C, Serbia ilitoka sare ya 1-1 na Estonia huku Slovenia ikitoka suluhu na Ireland ya Kaskazini.

Adrian Mutu alifunga mara mbili na kuiwezesha Romania kuifunga Luxembourg 3-1 katika mechi ya Kundi D, wakati Israel ilishinda 1-0 dhidi ya Georgia katika mechi za Kundi F.

Mshambuliaji wa Bayern Munich, Mario Gomez aliipatia timu yake bao la kuongoza katika mechi hiyo iliyopigwa Moenchengladbach lakini David Carney akasawazisha dakika ya 61 na David Wilkshire akaifungia penalti ya bao la ushindi Socceroos.

Australia ilipoteza mechi tatu mfululizo, na kuruhusu mabao matatu katika kila mechi.

"Hatukutarajia matokeo haya," alisema Holger Osieck, Kocha wa Australia. "Nawaheshimu Ujerumani, sikuangalia nani yuko uwanjani, wana wachezaji wazuri. Tulipanga kucheza vizuri na kujihami, lakini hatukutarajia matokeo haya."

Nayo Ufaransa ilikatizwa ushindi wa sita mfululizo baada ya Karim Benzema kupoteza nafasi ya wazi huku Adil Rami akiigongesha posti dhidi ya Croatia mechi iliyopigwa Stade de France.

Giuseppe Rossi na Alessandro Matri waliifungia Italia mabao mawili na kuifanya timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 huku ikicheza dakika 16 wakiwa 10 baada ya Davide Astori aliyeingia kipindi cha pili kulambwa kadi nyekundu.

Kiungo wa FC Porto, Ruben Micael alifunga mabao mawili na kuiwezesha Ureno kushinda 2-0 dhidi ya Finland mjini Aveiro, lakini Russia ililazimishwa sare ya 1-1 na Qatar.

Katika mechi nyingine, Denmark ilishinda mabao 2-1 dhidi ya Slovakia huku Ugiriki ikitoka suluhu na Poland.
 
Mashabiki Mali waishangilia Walibya Send to a friend Wednesday, 30 March 2011 20:45

BAMAKO, Mali
MAELFU ya mashabiki wa soka wa Mali, juzi waliishangiliwa Libya kwa nguvu ilipokuwa ikicheza na Comoro katika mechi ya kuwania kufuzu Fainali za Afrika 2012.

Mechi hiyo ilifanyika kwenye mji wa Bamako nchini Mali kutokana na uwepo wa usalama mdogo nchini Libya.

Zaidi ya mashabiki 20,000 wa Mali walikuwa na mabango yenye picha za kiongozi wa Libya huku wakiwa na mabango yanayopinga hatua za mataifa ya magharibi kuivamia Libya. Katika mchezo huo, Libya ilishinda mabao 3-0.

"Mashabiki wa Mali walitupa nguvu sana," alisema nahodha wa Libya, Tariq Ibrahim al-Tayib alipozungumza na BBC baada ya mchezo huo.Mwandishi wa habari anayeishi kwenye mji wa Bamako, Martin Vogl alisema serikali ya Mali na Libya zina uhusiano wa karibu na kiongozi wake, Muammar Gaddafi kwani wamekuwa wakiisaidia nchi hiyo katika nyanja mbalimbali.

Baada ya mchezo huo kumalizika, mashabiki walikuwa wakipiga kelele: "Gaddafi! Gaddafi," alisema.

Tayib alisema kuwa wachezaji wengi wameshindwa kujiunga na timu hiyo kwa kuwa wako Benghazi, mji wenye mgogoro mkubwa kati ya waasi na wanajeshi wa serikali ya Gaddafi.Hata hivyo alisema, hakuna mgawanyiko wa kisiasa kwenye suala la timu.
"Timu yote ni ya Muammar Gaddafi," alisema.

"Tunawapa ushindi huu wananchi wote wa Libya ambao wameangamia kwa njia moja ama nyingine," aliiambia Associated Press.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom