Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,502
- 911,254
- Thread starter
- #14,221
TP Mazembe kutua Dar Ijumaa
• Kuwaona Uwanja wa Taifa sh 5,000
na Mwandishi wetu
WAKATI wapinzani wa Simba katika Ligi ya Mabingwa barani Afrika, TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), wakitarajiwa kuwasili nchini kesho kutwa, viingilio vya mchezo baina ya timu hizo vimetajwa huku kiingilio cha chini kikiwa kimepangwa kuwa sh 5,000.
Simba inatarajiwa kukipiga na Mazembe Jumapili kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuanzia saa 9:30 jioni, ikiwa ni mechi ya marudiano baada ya ule wa awali uliopigwa Lubumbashi na Wekundu wa Msimbazi kulala kwa mabao 3-1.
Ofisa habari wa Simba, Clifford Ndimbo alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa, maandalizi kwa ajili ya mechi hiyo yanakwenda vizuri, ambako wachezaji wako katika hali nzuri na ari kubwa ya kushinda mechi hiyo.
Alisema, waamuzi wa mchezo huo kutoka Shelisheli na Kamisaa kutoka Kenya watawasili Jumamosi, huku tiketi zitaanza kuuzwa Ijumaa katika migahawa ya Steers, vituo vya mafuta vya Big Bon, Benjamin Mkapa Tower, BP Mwembechai na Uwanja wa Taifa.
Alivitaja viingilio katika mechi hiyo kuwa ni sh 40,000 kwa VIP A, sh 20,000 VIP B, 10,000 VIP C, huku watakaokaa viti vya rangi ya chungwa watalipa sh 8,000 na wale watakaokaa viti vya kijani na bluu watalipa sh 5,000.
• Kuwaona Uwanja wa Taifa sh 5,000
na Mwandishi wetu
Simba inatarajiwa kukipiga na Mazembe Jumapili kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuanzia saa 9:30 jioni, ikiwa ni mechi ya marudiano baada ya ule wa awali uliopigwa Lubumbashi na Wekundu wa Msimbazi kulala kwa mabao 3-1.
Ofisa habari wa Simba, Clifford Ndimbo alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa, maandalizi kwa ajili ya mechi hiyo yanakwenda vizuri, ambako wachezaji wako katika hali nzuri na ari kubwa ya kushinda mechi hiyo.
Alisema, waamuzi wa mchezo huo kutoka Shelisheli na Kamisaa kutoka Kenya watawasili Jumamosi, huku tiketi zitaanza kuuzwa Ijumaa katika migahawa ya Steers, vituo vya mafuta vya Big Bon, Benjamin Mkapa Tower, BP Mwembechai na Uwanja wa Taifa.
Alivitaja viingilio katika mechi hiyo kuwa ni sh 40,000 kwa VIP A, sh 20,000 VIP B, 10,000 VIP C, huku watakaokaa viti vya rangi ya chungwa watalipa sh 8,000 na wale watakaokaa viti vya kijani na bluu watalipa sh 5,000.
PRINT