Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,504
- 911,249
- Thread starter
- #13,061
Waandishi wa michezo wapewa changamoto
Imeandikwa na Mwandishi Maalumu, Seoul; Tarehe: 24th March 2011 @ 23:40 Imesomwa na watu: 26; Jumla ya maoni: 0
WAANDISHI wa habari za michezo duniani wametakiwa kujipanga kukabiliana na changamoto zitokanazo na maendeleo ya teknolojia ya habari kama blogu na kuenea kwa mitandao ya Intanet ili kuhakikisha misingi asili ya taaluma haikiukwi.
Rai hiyo imetolewa na Profesa Paul Pedersen wakati akiwasilisha mada ya uandishi wa kisasa katika kongamano la 74 la kimataifa la Vyama vya Waandishi wa Habari za Michezo Duniani (AIPS) linaloendelea hapa Seoul, Korea Kusini.
Alisema ni ukweli usiopingika kuwa kuibuka kwa teknolojia hizo kumesababisha kuzorota kwa uandishi wa kiasili (traditional media) kutokana na urahisi wa upatikanaji wake usiozingatia misingi ya taaluma na kujali walaji.
"Blogu zimesababisha habari kufika kwa jamii kwa uhuru mkubwa bila chujio tena bure jambo linalosababisha kampuni nyingi za habari kufilisika kutokana na mauzo ya habari hasa kupitia magazeti, kushuka kila kukicha," alisema.
Profesa Pedersen alisema ni vigumu kuzuia maendeleo ya habari kisasa lakini cha muhimu kwa wanataaluma ni kuendelea kusisitiza misingi ya taaluma ili uandishi wa michezo usiathirike kama zilivyo nyingine hivi sasa duniani.
Badala yake alisema ni vyema utandawazi na mabadiliko ya fani ya ueneaji wa habari, ukatumiwa na waandishi kwa ajili ya kutangaza michezo na wanamichezo duniani.
Awali, akiwasilisha mada katika kongamano hilo, Rais wa Chama cha Michezo ya Kubahatisha Michezoni, Risto Nieminen, alisema waandishi wa michezo ni wasimamizi wakubwa wa haki katika matokeo michezoni na kuwataka kutotumika kwa namna yoyote kupanga matokeo kwa lengo la kunufaisha kundi fulani la watu.
Alisema katika baadhi ya nchi zilizoendelea, waandishi wamekuwa wakitumiwa kwa kupanga matokeo au kutofichua mianya ya upangaji matokeo kwa misingi ya rushwa na kushauri kila mdau wa habari za michezo kujikosoa mwenyewe ili kuleta mabadiliko duniani.
"Ipo mifano katika baadhi ya nchi lakini cha muhimu ni kwetu sisi kuwa wapingaji zaidi... najua hili litakupunguzia marafiki wengi lakini litakuongezea heshima kubwa," alisema.
Kongamano hilo linalotarajiwa kumalizika Machi 25 mwaka juu, limeratibiwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Duniani (AIPS) kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa
Habari za Michezo Korea Kusini.
Imeandikwa na Mwandishi Maalumu, Seoul; Tarehe: 24th March 2011 @ 23:40 Imesomwa na watu: 26; Jumla ya maoni: 0
WAANDISHI wa habari za michezo duniani wametakiwa kujipanga kukabiliana na changamoto zitokanazo na maendeleo ya teknolojia ya habari kama blogu na kuenea kwa mitandao ya Intanet ili kuhakikisha misingi asili ya taaluma haikiukwi.
Rai hiyo imetolewa na Profesa Paul Pedersen wakati akiwasilisha mada ya uandishi wa kisasa katika kongamano la 74 la kimataifa la Vyama vya Waandishi wa Habari za Michezo Duniani (AIPS) linaloendelea hapa Seoul, Korea Kusini.
Alisema ni ukweli usiopingika kuwa kuibuka kwa teknolojia hizo kumesababisha kuzorota kwa uandishi wa kiasili (traditional media) kutokana na urahisi wa upatikanaji wake usiozingatia misingi ya taaluma na kujali walaji.
"Blogu zimesababisha habari kufika kwa jamii kwa uhuru mkubwa bila chujio tena bure jambo linalosababisha kampuni nyingi za habari kufilisika kutokana na mauzo ya habari hasa kupitia magazeti, kushuka kila kukicha," alisema.
Profesa Pedersen alisema ni vigumu kuzuia maendeleo ya habari kisasa lakini cha muhimu kwa wanataaluma ni kuendelea kusisitiza misingi ya taaluma ili uandishi wa michezo usiathirike kama zilivyo nyingine hivi sasa duniani.
Badala yake alisema ni vyema utandawazi na mabadiliko ya fani ya ueneaji wa habari, ukatumiwa na waandishi kwa ajili ya kutangaza michezo na wanamichezo duniani.
Awali, akiwasilisha mada katika kongamano hilo, Rais wa Chama cha Michezo ya Kubahatisha Michezoni, Risto Nieminen, alisema waandishi wa michezo ni wasimamizi wakubwa wa haki katika matokeo michezoni na kuwataka kutotumika kwa namna yoyote kupanga matokeo kwa lengo la kunufaisha kundi fulani la watu.
Alisema katika baadhi ya nchi zilizoendelea, waandishi wamekuwa wakitumiwa kwa kupanga matokeo au kutofichua mianya ya upangaji matokeo kwa misingi ya rushwa na kushauri kila mdau wa habari za michezo kujikosoa mwenyewe ili kuleta mabadiliko duniani.
"Ipo mifano katika baadhi ya nchi lakini cha muhimu ni kwetu sisi kuwa wapingaji zaidi... najua hili litakupunguzia marafiki wengi lakini litakuongezea heshima kubwa," alisema.
Kongamano hilo linalotarajiwa kumalizika Machi 25 mwaka juu, limeratibiwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Duniani (AIPS) kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa
Habari za Michezo Korea Kusini.