Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,508
- 911,249
- Thread starter
- #11,421
Miss Utalii kutembelea ‘media'
na Mwandishi wetu
MSHINDI wa taji la taifa la Miss Utalii Tanzania mwaka huu, Adelqueen Njozi, akiambatana na wale tano bora wanaotarajiwa kufanya ziara ya kujitangaza katika vyombo mbalimbali vya habari.
Kwa mujibu wa Rais wa Miss Utalii Tanzania, Gideon Chipungahelo, Njozi ataambatana na washindi wa pili hadi wa tano, ambao ni Happywitney, Mariam Rabi, Rosemary Kasiga, Immaculate Alphonce na Miss Utalii Tanzania 2010/11 Vipaji, Deissy Mshumbuzi.
Chipungahelo alisema ziara hiyo ya wiki moja itaanza Machi 17 ambayo pia utaambatana na mafunzo.
Alisema ziara hiyo iliyopewa jina la ‘Miss Tourism Tanzania 2010/11 Media Tour', ina malengo ya kuwawezesha warembo hao, kujifunza jinsi vyombo vya habari vinavyofanya kazi ya kuhabarisha na kuelimisha jamii.
Rais huyo aliongeza kuwa hiyo ni moja ya utekelezaji wa mpango mkakati wao wa kushirikiana kwa karibu na sekta hiyo katika kutekeleza majukumu yao ya kutangaza vivutio vya utalii kitaifa na kimataifa.
"Pia ni sambamba na kuhamasisha utalii wa ndani, kuelimisha jamii juu ya utalii na utamaduni, kutangaza mianya ya uwekezaji ya Tanzania, kuhamasisha kampeni ya kuondoa umaskini kupitia utalii, kupiga vita juu ya uvuvi na uwindaji haramu, uharibifu wa mazingira na vita dhidi ya tamaduni kongwe na potofu, zikiwemo za tohara kwa wanawake, mauaji ya vikongwe, albino na uchunaji wa ngozi," alisema.
Aidha, ziara hiyo itatoa fursa kwa warembo hao, kujitambulisha kwa vyombo vya habari na kupanga mikakati ya kushirikiana katika medani nzima ya kutangaza sekta hiyo ya utalii.
Chipungahelo aliongeza kuwa aidha katika ziara hiyo warembo hao watakabidhi vyeti vya shukrani kwa vyombo vya habari ambavyo vimetoa mchango mkubwa katika kufanikisha fainali za mwaka huu na mashindano kwa ujumla.
Fainali za Miss Utalii taifa zilifanyika Machi 5 mwaka huu katika Hoteli ya Kiromo, Bagamoyo, Pwani ambako zaidi ya warembo 30 kutoka mikoa yote na vyuo vikuu waliwania taji hilo, ambalo washindi wake watawakilisha Tanzania katika mashindano ya kimataifa.
Mashindano hayo ni pamoja na ‘International Miss Tourism World', ‘Miss Heritage World', ‘Miss Tourism University World', ‘Miss Globe International', ‘Miss United Nations', ‘Miss University Africa' na mengineyo ya kimataifa.
na Mwandishi wetu
Kwa mujibu wa Rais wa Miss Utalii Tanzania, Gideon Chipungahelo, Njozi ataambatana na washindi wa pili hadi wa tano, ambao ni Happywitney, Mariam Rabi, Rosemary Kasiga, Immaculate Alphonce na Miss Utalii Tanzania 2010/11 Vipaji, Deissy Mshumbuzi.
Chipungahelo alisema ziara hiyo ya wiki moja itaanza Machi 17 ambayo pia utaambatana na mafunzo.
Alisema ziara hiyo iliyopewa jina la ‘Miss Tourism Tanzania 2010/11 Media Tour', ina malengo ya kuwawezesha warembo hao, kujifunza jinsi vyombo vya habari vinavyofanya kazi ya kuhabarisha na kuelimisha jamii.
Rais huyo aliongeza kuwa hiyo ni moja ya utekelezaji wa mpango mkakati wao wa kushirikiana kwa karibu na sekta hiyo katika kutekeleza majukumu yao ya kutangaza vivutio vya utalii kitaifa na kimataifa.
"Pia ni sambamba na kuhamasisha utalii wa ndani, kuelimisha jamii juu ya utalii na utamaduni, kutangaza mianya ya uwekezaji ya Tanzania, kuhamasisha kampeni ya kuondoa umaskini kupitia utalii, kupiga vita juu ya uvuvi na uwindaji haramu, uharibifu wa mazingira na vita dhidi ya tamaduni kongwe na potofu, zikiwemo za tohara kwa wanawake, mauaji ya vikongwe, albino na uchunaji wa ngozi," alisema.
Aidha, ziara hiyo itatoa fursa kwa warembo hao, kujitambulisha kwa vyombo vya habari na kupanga mikakati ya kushirikiana katika medani nzima ya kutangaza sekta hiyo ya utalii.
Chipungahelo aliongeza kuwa aidha katika ziara hiyo warembo hao watakabidhi vyeti vya shukrani kwa vyombo vya habari ambavyo vimetoa mchango mkubwa katika kufanikisha fainali za mwaka huu na mashindano kwa ujumla.
Fainali za Miss Utalii taifa zilifanyika Machi 5 mwaka huu katika Hoteli ya Kiromo, Bagamoyo, Pwani ambako zaidi ya warembo 30 kutoka mikoa yote na vyuo vikuu waliwania taji hilo, ambalo washindi wake watawakilisha Tanzania katika mashindano ya kimataifa.
Mashindano hayo ni pamoja na ‘International Miss Tourism World', ‘Miss Heritage World', ‘Miss Tourism University World', ‘Miss Globe International', ‘Miss United Nations', ‘Miss University Africa' na mengineyo ya kimataifa.