Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,505
- 911,249
- Thread starter
- #10,481
Nahodha Barca ajipoza Send to a friend Tuesday, 08 March 2011 19:53
BARCELONA, Hispania
BEKI wa kati ya Barcelona, Carles Puyol amejipoza maumivu ya kuikosa mechi dhidi ya Arsenal jana usiku kwa kupokea euro 100,000 ambazo alikabidhiwa kabla ya mechi ya jana.
Puyol ambaye ni majeruhi alikabidhiwa hundi ya kiasi hicho cha fedha ambazo ameahidi kuzitoa kwa Chama cha Kimataifa cha Msalaba Mwekundu (ICRC).
Kulingana na Uefa, Shirikisho la Soka Ulaya, beki huyo alipigiwa kura 230,000 na kutajwa kuwa nahodha wa timu ya mwaka ya watumiaji wa mtandao wa shirikisho hilo, UEFA.com .
Mshauri wa Rais wa Uefa, Michel Platini, William Gaillard ndiye alikabidhi hundi hiyo kwa Puyol kabla ya mchezo huo kwenye Uwanja wa Camp Nou.
Msaada huo kwa mara ya nne umekabidhiwa kwa ICRC kutoka kwa nahodha wa timu hiyo ya watumiaji wa UEFA.com, alieleza Gaillard. Fedha hizo zitatumiwa kusaidia waathirika wa mabomu ya kutegwa nchini Afghanistan.
UEFA ilianza ushirikiano wake na Msalaba Mwekundu mwaka 1997, mkazi ukiwekwa zaidi kwenye ICRC kupambana na mabomu ya kutegwa.
Mbali ya waathirika kusaidiwa, pia fedha hizo zimekuwa zikitumika katika elimu ya ufundi na ununuzi wa vifaa mbalimbali vya kuwasaidia kujimudu kimaisha kama miguu na mikono ya bandia.
Hadi sasa, ICRC imefanikiwa kuwasaidia watu zaidi ya 90,000 wa mabomu hayo na wengine wasiojiweza tangu kuanzishwa kwa mpangi huo mwaka 1988.
Puyol, 32, alsema: "Ni heshima kubwa kwangu kuchaguliwa nahodha wa UEFA.com . Ninatambua kwamba nimetukuzwa si kwa kucheza soka pekee, bali kuwa na afya na miguuu miwili iliyo kamili. Nina furaha kuchangia katika mpango huu wa kuwasaidia watu wasiojiweza, ni matumaini yangu kwamba wataboreshewa maisha."
Timu hiyo ya mwaka 2010 ya UEFA.com ni pamoja na : Iker Casillas (Real Madrid ); Maicon ( Inter), Gerard Pique ( Barcelona), Carles Puyol ( Barcelona), Ashley Cole (Chelsea); Cristiano Ronaldo (Real Madrid ), Xavi Hern·ndez ( Barcelona), Wesley Sneijder ( Inter ), Andres Iniesta ( Barcelona); Lionel Messi ( Barcelona), David Villa ( Barcelona). Kocha : JosÈ Mourinho (Real Madrid ).
BARCELONA, Hispania
BEKI wa kati ya Barcelona, Carles Puyol amejipoza maumivu ya kuikosa mechi dhidi ya Arsenal jana usiku kwa kupokea euro 100,000 ambazo alikabidhiwa kabla ya mechi ya jana.
Puyol ambaye ni majeruhi alikabidhiwa hundi ya kiasi hicho cha fedha ambazo ameahidi kuzitoa kwa Chama cha Kimataifa cha Msalaba Mwekundu (ICRC).
Kulingana na Uefa, Shirikisho la Soka Ulaya, beki huyo alipigiwa kura 230,000 na kutajwa kuwa nahodha wa timu ya mwaka ya watumiaji wa mtandao wa shirikisho hilo, UEFA.com .
Mshauri wa Rais wa Uefa, Michel Platini, William Gaillard ndiye alikabidhi hundi hiyo kwa Puyol kabla ya mchezo huo kwenye Uwanja wa Camp Nou.
Msaada huo kwa mara ya nne umekabidhiwa kwa ICRC kutoka kwa nahodha wa timu hiyo ya watumiaji wa UEFA.com, alieleza Gaillard. Fedha hizo zitatumiwa kusaidia waathirika wa mabomu ya kutegwa nchini Afghanistan.
UEFA ilianza ushirikiano wake na Msalaba Mwekundu mwaka 1997, mkazi ukiwekwa zaidi kwenye ICRC kupambana na mabomu ya kutegwa.
Mbali ya waathirika kusaidiwa, pia fedha hizo zimekuwa zikitumika katika elimu ya ufundi na ununuzi wa vifaa mbalimbali vya kuwasaidia kujimudu kimaisha kama miguu na mikono ya bandia.
Hadi sasa, ICRC imefanikiwa kuwasaidia watu zaidi ya 90,000 wa mabomu hayo na wengine wasiojiweza tangu kuanzishwa kwa mpangi huo mwaka 1988.
Puyol, 32, alsema: "Ni heshima kubwa kwangu kuchaguliwa nahodha wa UEFA.com . Ninatambua kwamba nimetukuzwa si kwa kucheza soka pekee, bali kuwa na afya na miguuu miwili iliyo kamili. Nina furaha kuchangia katika mpango huu wa kuwasaidia watu wasiojiweza, ni matumaini yangu kwamba wataboreshewa maisha."
Timu hiyo ya mwaka 2010 ya UEFA.com ni pamoja na : Iker Casillas (Real Madrid ); Maicon ( Inter), Gerard Pique ( Barcelona), Carles Puyol ( Barcelona), Ashley Cole (Chelsea); Cristiano Ronaldo (Real Madrid ), Xavi Hern·ndez ( Barcelona), Wesley Sneijder ( Inter ), Andres Iniesta ( Barcelona); Lionel Messi ( Barcelona), David Villa ( Barcelona). Kocha : JosÈ Mourinho (Real Madrid ).