Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,482
- 40,495
Kuna rafiki yangu mmoja yupo kwenye ndoa huu ni mwaka wa 19, wameishi pamoja na mkewe kwa muda mrefu, na hii imechangiwa pia kwa kufanya kazi mkoa ambapo wote wanaishi pamoja.
Amejitahidi kujiwekeza anavyoweza ila mwaka juzi alipata uhamisho wa kikazi wa kwenda mkoa wa mbali.
Kufika huko mkoani akaanza maisha mapya ya ubachela, mbaya zaidi hakuwa na mchepuko. Ikawa anajitahidi kila wakati kumtumia mkewe nauli ili aende akamalize haja zake.
Basi jamaa ikabidi apambane anavyoweza ili aweze kurudi nyumbani akaishi na mkewe kwa kujiajiri, akafanikiwa kununua Hiace.Amejitahidi kujiwekeza anavyoweza ila mwaka juzi alipata uhamisho wa kikazi wa kwenda mkoa wa mbali.
Kufika huko mkoani akaanza maisha mapya ya ubachela, mbaya zaidi hakuwa na mchepuko. Ikawa anajitahidi kila wakati kumtumia mkewe nauli ili aende akamalize haja zake.
Kutokana na nguvu ya kumpenda mkewe pamoja na kuhisi labda wakulungwa wanamfaidi, akaamua kuacha kazi, na kurudi kwa mkewe.
Mbaya zaidi, gari yake bado hajaikamilisha kwenye usajili, imepaki nyumbani tu, na amekuwa ni baba wa nyumbani. Mpaka mkewe ameanza kumdharau, kwa sababu hakuna mapato yanayoingia.
Na mapenzi yameanza kuchuja
Chakujifunza: nguvu ya mwanaume ni pesa, huko alipo kama angekuwa na mchepuko pesa ingekuwepo na heshima ingekuwepo.