Uchaguzi 2020 Miaka mitano ya Rais Magufuli ni somo tosha la Uraia kwa vitendo. Inatosha, tuseme Hapana

RockCarnegie

JF-Expert Member
Jan 17, 2019
963
1,927
Habari wana JF

Ukijifunza kwa nadharia tu, mara nyingi watu walio wengi huwa ni vigumu kupata ufahamu mpaka wafanye vitendo (practical).

Mwaka 2015 vyama upinzani viliwaeleza namna wananchi watakavyooshwa na Serikali chini ya Rais Magufuli lakini hawakuamini! Miaka mitano baadaye kila mtu anaweza kuelewa kuwa kukosea kuchagua kiongozi wa nchi, gharama inayolipwa na kila mtu ni kubwa haijalishi wewe ni kada mtiifu ama ni mpinzani!

1. Wafanyabiashara wanalia biashara zao zimekufa lakini wanasahau kuwa hawakutimiza wajibu wao ili kulipatia taifa kiongozi bora.

2. Wakulima wa korosho, pamba, mbaazi, choroko, ndegu, ufuta nk wanalia mazao yao yanakosa wanunuzi, lakini wanasahau kuwa walifanya kosa la kiufundi mwaka 2015 kuchagua rais na chama kisicho na uwezo wa kuwatafutia masoko ya mazao yao.

3. Wananchi waliokumbwa majanga ya matetemeko na mafuriko mnaweza kusimulia vizuri baada ya kufikisha vilio vyenu kwa mfariji mkuu wa taifa. Aliwaambia yeye hakuleta tetemeko, na waliosombwa na mafuriko aliwaambia acha mabonde 'yawabondoe'.

4. Jana mkulu awatangazia ambao hawakufanikiwa kupata mavuno mazuri ya mazao ya chakula 'watwangwe'! Ni somo la uraia kwa vitendo!

5. Wanahabari habari mnazo, ukijifanya mjuaji hutaki kusifu na kuabudu, uhujumu uchumi na uchochezi unakuhusu! Wote wimbo ni mmoja tu, nao ni Heko mtukufu kwa kuletea ndege, SGR, Stiglers na mabarabara ya juu kwa juu!

6. Wafanyakazi mpo! Miaka mitano jamaa kapiga pasi ndefu, hata mia haijaongezwa kwenye mishahara!

7. Wafugaji na wavuvi nao wanayakusimulia, umasikini ulioasisiwa na Magufuli na chama chake si wa kuisha leo ama kesho!

8. Wamachinga nao hawajabaki salama. Siku hizi wanapanga bidhaa mpaka katikati ya barabara, lakini wateja hamna! Uchumi umebaki wa kuhemea ubwabwa tu!

9. Wahitimu wa vyuo nao hawajaachwa salama kwenye somo hili la uraia kwa vitendo! Hakuna ajira na viwanda vinafungwa kila siku!

10. Bunge na Mahakama nao ni kuimba "asifiwe chaguo la Mungu". Wananchi hakuna pa kukimbilia kwani mhimili uliojichimbia unafanya kazi kwa maagizo na si kwa sheria na katiba!

Jiwe linataka miaka mingine mitano, sipati picha maisha ya watu yatakuwaje, kwani kwa ni heri punda afe ila mzigo ufike! Tayari mahabusu wametangaziwa kiama cha kazi ngumu kabla ya kutiwa hatiani, na kila mtu ni mahabusu mtarajiwa!

Uchaguzi mkuu wa October ni upenyo wa kuikataa CCM na mgombea wake Rais Magufuli ambaye kwa miaka mitano amedhihirisha kuwa kwake vitu ni bora kuliko utu!

Pamoja na kuwa Tume ya uchaguzi, polisi na usalama ni mbeleko za chuma zinazo mhakikishia Jiwe kuapishwa kuwa rais kwa miaka mingine mitano, Mungu huwa yuko upande wa wenye haki, Mwananchi timiza wajibu wako, kataa mateso na umasikini unaoletwa kwa makusudi na CCM chini ya Jiwe.
 
Huyu ni Rais wa Miundombinu! Kwa hilo, anastahili pongezi zote. Ila ukija kwenye hayo makundi, mfano Wafanyakazi! Hana faida yoyote ile kwa kweli.
Miundo mbinu yake ni SGR na Rufiji Gorge.

Asipofanikiwa kwa hiyo basi tena.
 
Huyu ni Rais wa Miundombinu! Kwa hilo, anastahili pongezi zote. Ila ukija kwenye hayo makundi, mfano Wafanyakazi! Hana faida yoyote ile kwa kweli.
Rais wa miundo mbinu barabara ya kutoka Ruaha mpaka Ifakara alitoa ahadi ya kuiweka lami lakini hadi sasa miaka zaidi ya mitatu imepita na hakueleweki.
 
Naomba kuuliza swali.
Hivi ni sababu gani ya msingi iliyopelekea serikali kutokuongeza mishahara?

Ni kwa sababu ya uhakiki, kununua ndege, kujenga stiglers gorge, kujenga flyovers, nk. Hizi ndiyo sababu zao siku zote.

Tunaishukuru sana Corona kwa kutuepusha na zile hotuba za mei mosi za kukopi na kupesti kwa miaka 5 mfululizo.
Enzi za JK kila mwaka kuna incriment, baada ya miaka 3 unapandishwa daraja, baada ya miaka 3 anaongeza mshahara!

Kwa sasa ukibahatika tu kupandishwa daraja tena baada ya miaka 5 na kuendelea, unatamani kufanya sherehe! maana huamini. No annual salary incriment! hakuna ajira mpya! Wafanyakazi wanaishi kwa vitisho na bila matumaini yoyote yale.
 
Rais wa miundo mbinu barabara ya kutoka Ruaha mpaka Ifakara alitoa ahadi ya kuiweka lami lakini hadi sasa miaka zaidi ya mitatu imepita na hakueleweki.

Yule Mkandarasi huenda ana uhusiano na kigogo mkubwa serikalini! Haiwezekani ni zaidi ya miaka 3 sasa, bado yuko busy tu kusembua barabara na kujenga vikaravati!

Au labda wanasubiria uchaguzi ukaribie ndipo waongeze bidii ili waje wawadanganye Wana Ifakara muirudishe tena Ccm madarakani, ingawa mpaka sasa uwezekano wa kurudisha hayo majimbo mawili kutoka Chadema ni mkubwa sana.
 
Naomba kuuliza swali.
Hivi ni sababu gani ya msingi iliyopelekea serikali kutokuongeza mishahara?

Simply ni kuwa Jiwe kwa miaka mitano, Jiwe amejidhihirisha kuwa ni mtu asiyejua ama kwa makusudi hathamini kuwa watu ni rasilimali kubwa inayohitaji kupata ustawi ili ilete tija zaidi. Fikra zake anaona watu ni kama punda tu, akishafikisha mzigo basi hana faida tena akajitafutie!
 
Unapoona mtu anaishabikia CCM au amevaa mtisheti wa CCM unamtazaaamaaa unamuonea tu huruma Cha ajabu wengi wanaovaa matisheti kofia au mavilemba ya CCM ni wazee au majitu yenye sura mbayambaya hivi.
 
Hayumbishwi,anafanya maamuzi magumu,
hanasifa ya kujilimbikizia mali na ubadhilifu,analinda na kuzitumia rasilimali za nchi kwa manufaa ya nchi.sifa zake na nyingi sana ila kwa hizi chache zinatosha.

Kuyumbishwa na nani!?. Unauhakika hajilimbikizii au unaongea kishabiki! Mbona tuhuma za upotevu wa pesa ni nyingi na zinappotelea ikulu ambako CAG amezuiliwa kukagua!
Rasilimali gani amelinda, mbona makinikia wazungu wanabeba!

Sifa munazo mpa Magufuli ni sifa bandia za gizani! Peupe ni mchafu afadhali ya dodoki!
 
Back
Top Bottom