Miaka 60 ya uhuru umeme bado wa shida Tanzania

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Apr 12, 2018
2,510
4,224
Inasikitisha sana kuona jinsi shirika hili linavyoendeshwa.Miaka 60 ya uhuru lakini bado umeme ni wa shida hapa nchini.

Mbaya zaidi hakuna anayewajibika au kuwajibishwa. Waziri mhusika ndiyo kwanza anatumia chopper kukagua vyanzo vya maji na kusema Tanzania nzima hakuna Crane ya kuweza kubeba tani 80 na kutangaza mgao wa siku zaidi ya 10 akiahidi kumaliza kero za umeme jambo ambalo tumeshuhudia kuwa ni uongo, Lakini cha kushangaza bado yupo ofisini.

Umeme umekuwa ukikatika hovyo kwa kisingizio cha dharura. Hivi TANESCO wanaelewa maana ya neno 'dharura'?

Walau miaka michache iliyopita hapakuwa na makatizo Makali ya umeme kiasi hiki. Ina maana vyanzo vya umeme hapo nyuma vilikuwa tofauti na sasa?

Tuliaminishwa mgao mkubwa uliopita siku za karibuni utakuwa mwisho Lakini inasikitisha kuona kila mara umeme bado unakatika kwa sababu zisizoisha.

Sijui lini Tutafika.
 
Viongozi wetu wa siasa ndio changamoto kubwa baada ya hao Kuna watumishi wa umma baadhi Yao Kama sio wengi wao ni majipu. Mwisho kabisa Katina yetu haiwawajibishi Hawa watu accordingly. Hivyo nilivyokutajia vikiwa katika mstari Tutasonga mbele
 
Inasikitisha sana kuona jinsi shirika hili linavyoendeshwa.Miaka 60 ya uhuru lakini bado umeme ni wa shida hapa nchini.

Mbaya zaidi hakuna anayewajibika au kuwajibishwa. Waziri mhusika ndiyo kwanza anatumia chopper kukagua vyanzo vya maji na kusema Tanzania nzima hakuna Crane ya kuweza kubeba tani 80 na kutangaza mgao wa siku zaidi ya 10 akiahidi kumaliza kero za umeme jambo ambalo tumeshuhudia kuwa ni uongo, Lakini cha kushangaza bado yupo ofisini.

Umeme umekuwa ukikatika hovyo kwa kisingizio cha dharura.Hivi TANESCO wanaelewa maana ya neno 'dharura'?

Walau miaka michache iliyopita hapakuwa na makatizo Makali ya umeme kiasi hiki. Ina maana vyanzo vya umeme hapo nyuma vilikuwa tofauti na sasa?

Tuliaminishwa mgao mkubwa uliopita siku za karibuni utakuwa mwisho Lakini inasikitisha kuona kila mara umeme bado unakatika kwa sababu zisizoisha.

Sijui lini Tutafika.
Ni wakati wa mabadiliko sasa
 
Hapa nilipo umekatika Jana saa mbili usiku mpaka muda huu haujawaka,r.i.p Magufuli
 
Miaka 60 umeme wa kukatika katika, papo hapo kuna nchi zingine duniani zinasherehekea miaka 100 bila ya kukatika kwa umeme.

Wakati mwingine unaweza kukataa kabisa TZ tunasingiziwa kuitwa mojawapo ya nchi yenye rasilimali za kutosha duniani
 
Back
Top Bottom