Miaka 4 hata 10 bado haitoshi kuiweka TANESCO sawa

Miaka 4 hata 10 bado haitoshi kuiweka TANESCO sawa

ubarinolutu

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2012
Posts
2,711
Reaction score
5,641
Nimemsikia Waziri Makamba akisema apewe miaka minne Kama Kalemani na Kero zote za TANESCO atakuwa kazimaliza. Kiuhalisia Miaka minne haitoshi kuiweka TANESCO Sawa, na matatizo naona ndo naona yanaweza kuwa makubwa zaidi kutokana na mambo mbalimbali Kama yafuatayo

1. Miundombinu isiyofuata viwango inazidi kujengwa na kusambaa hasa inayojengwa na Tanesco na REA, hivyo kuongeza tatizo la kukatika umeme na tatizo hapa ni siasa hivyo . Hakuna kitengo Cha kusimamia ubora katika wizara

2. Hili shirika bado linaendelea kuwa na mideni isiyoshuka, na sijui wizara Ina mpango gani wa kulipa deni Hilo linalosemekana ni trilioni 1

3. Ubora wa vifaa unaotumika katika miundombinu ya umeme ni ya chini, hivyo umeme utaendelea kukatika tu maana tayari ndo miundombinu iliyopo na hatuna pesa za kuibadilisha.

4. Stigler's gorge ndani ya miaka minne itakuwa haijakamilika, fikiria rusumo Ina MW 81 miaka 5 imepita bado haujaisha ndo ije 2115, grand Ethiopian haijaisha na miaka 11 imepita. Kipindi stigler's inakamilika tutakuwa tumeshateseka sana na mgao.

5. Tatizo co Makamba Wala Kalemane, Tanesco ilishaharibika siku nyingi , almost miaka 30 iliyopita, matatizo uliyoyakusanya kwa miaka 30 huwezi kuyatatua kwa miaka 4.

6. Uzalishaji uliopo bado mdogo kulingana na mahitaji yaliyopo hivyo mfano ukizima mtambo wa kidatu Kuna mgao.

7. Matatizo ya kukatika umeme kwenye usambazaji ni makubwa kuliko kwenye uzalishaji hivyo umeme utaendelea kukatika tu na sijui utaacha lini.

Ongezea sababu nyingine kuonesha miaka minne haitoshi, na tayari imebakia miaka mitatu na miezi kazaa
 
Mbna Kwa Maghufuli kulikuwa hakuna matatizo , before him things were worse than today ,unatakiwa uwe Fala tu kuzikubali hzo cheap excuse
 
Kama majibu ya kwanini umeme unakatika katika ndio kama haya kila mtu anaweza kuwa Waziri wa Nishati maana unajibu lolote tu unalojisikia na hakuna wa kukuwajibisha.
 
Back
Top Bottom