Miaka 36 ya Mugabe Zimbabwe na 12 ya Mbowe CHADEMA

Miaka 36 ya Mugabe Zimbabwe na 12 ya Mbowe CHADEMA

Mimi ni mkulima niko huku kijijini Lusewa. Sina pembejeo za kilimo, mazao yangu yamekosa bei ya uhakika sokoni (nanyang'anywa), wanangu hawapati elimu bora kwani kuna mrundikano madarasani na hawasomi katika mazingira rafiki kwa mtoto, huduma za afya ni mbovu kupita maelezo kwani mara niendapo hospitali natakiwa kununua dawa kwenye maduka ya madawa na sizipati toka hospitalini hapo, usafiri wa kawaida huku kwetu ni wa kutumia "maguta" yaani pikipiki zenye matairi matatu, umeme tunakutana nao pindi tuendapo mjini. Sasa ndugu yangu badala ya kuongelea shida tuzipatazo sisi wakulima wa Lusewa na kuishauri serikali ya CCM na Magufuli watupunguzie ukali wa maisha, wewe unamwongelea Mbowe sijui, ambaye sisi huku Lusewa hatufahamu anakoishi na wala kazi anayofanya. Mbowe ni nani kwenye maslahi yetu sisi wavuja jasho? Wakati mwingine, ukishiba acha kuwadhihaki wenye njaa.
 
Mimi ni mkulima niko huku kijijini Lusewa. Sina pembejeo za kilimo, mazao yangu yamekosa bei ya uhakika sokoni (nanyang'anywa), wanangu hawapati elimu bora kwani kuna mrundikano madarasani na hawasomi katika mazingira rafiki kwa mtoto, huduma za afya ni mbovu kupita maelezo kwani mara niendapo hospitali natakiwa kununua dawa kwenye maduka ya madawa na sizipati toka hospitalini hapo, usafiri wa kawaida huku kwetu ni wa kutumia "maguta" yaani pikipiki zenye matairi matatu, umeme tunakutana nao pindi tuendapo mjini. Sasa ndugu yangu badala ya kuongelea shida tuzipatazo sisi wakulima wa Lusewa na kuishauri serikali ya CCM na Magufuli watupunguzie ukali wa maisha, wewe unamwongelea Mbowe sijui, ambaye sisi huku Lusewa hatufahamu anakoishi na wala kazi anayofanya. Mbowe ni nani kwenye maslahi yetu sisi wavuja jasho? Wakati mwingine, ukishiba acha kuwadhihaki wenye njaa.
Wewe sio mkulima wa Lusewa, hakuna mkulima anayeweza kuchukua muda katika kuandika yote uliyoyaandika tena kwa mpangilio uliotumia. Jamii forum inazo mada ngapi zinazoendelea kwa sasa?. Unao uhakika kwamba hakuna mada hata moja inayokuhusu wewe na shida za Lusewa?. Unataka kunipangia nini cha kuongea, wakati gani niongee, hiyo sio demokrasia.
 
mwacheni kaka yetu babu wee mbona ccm ipo tangu enzi na enzi mnaiba kura mnakata albino vidole sie hatusemi nyambafu kabisa nyiie hata znz pia ni yaleyale
nadhani hujamuelewa mtoa mada. yeye kazungumzia mtu hajazungumzia chama kinachokaa madarakani. kazungumzia Mbowe sasa kama ungelinganisha na ccm labda ungelinganisha na labda Nyerere, Mwinyi, Mkapa, au kikwete.umezungumzia ushabiki usiokuwa na tija kwa taifa letu. upumbaf mtupu
 
Back
Top Bottom