DR Mambo Jambo
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 8,580
- 17,683
Habari za Mida hii Ndugu Zangu Naomba kuanza kwa kuwatakia Sikukuu njema ya Kuzaliwa kwa Yesu kwa wale wote wafuasi wa imani ya Kikristo na hope mnaenjoy sana Happy noela
Kabla ya yote ningependa kurejea Luka 1:1-3 Kama inavyosema;
..."Kwa kuwa watu wengi wametia mikono kutunga kwa taratibu habari za mambo yale yaliyotimizwa katikati yetu,kama walivyotuhadithia wale waliokuwa mashahidi wenye kuyaona, na watumishi wa lile neno tokea mwanzo,nimeona vema mimi nami, kwa kuwa nimejitafutia usahihi wa mambo hayo yote tangu mwanzo, kukuandikia kwa taratibu,.........,"
Miaka 2000 iliyopita katika Mji wa bathelehem ya Uyahudi Alizaliwa Mtoto Aliyepewa Jina la Yeshua/Yehoshua ama yesu au Issa unaweza kumuita utakavyoweza kuita kwa lugha yako ilimradi imani ibaki kuwa alizaliwa Mtoto Ambaye ni Mtu muhimu sana katika historia ya ukombozi wa Wakristo duniani,
Na maandiko yote Yameandika kuhusu yesu kuzaliwa kwake,Miujiza yake mafundisho yake kuishi kwake ,Kusulubiwa kwake na kufufuka kwake na hata kupaa kwake kwenda mbinguni.
Maandiko yote ya biblia yaliyopo yanaanza kuzungumzia yesu kuanzia alipokuwa anazaliwa mpaka akiwa na umri wa miaka 12 (Soma luka 2 yote,pia soma mathayo 2)
Lakini baada ya miaka hiyo 12 Biblia ikawa kimya mpaka tena pale ambapo yesu anatimiza miaka 30 ya maisha yake ndo tunaona yesu anaanza kutajwa tena,kipindi anabatizwa na yohana Mbatizaji..(luka 3:23,Marco 1;9 ,Mathayo 3 kuanzia aya ya 14 na kuendelea)
Lakini miaka yake yote kuanzia umri wa miaka 13 mpaka 29 hakuna sehemu yoyote ya biblia inayotaja maisha yake alikuwa wapi? Alifanya nini? Aliishi wapi? na ilikuwaje?
basi nitajaribu kupitia baadhi ya theory na nakala za vitabu ili tuende sawa katika kujibu haya
HOJA KWA UFUPI
Maisha ya yesu kipindi Akiwa hai hakuna aliyekuwa anayanakili ama kuandika maisha yake kwakuwa Maisha yake na injili hii imekuja kuandikwa Miaka 70 mpaka 140 baada ya kifo chake.
Japo inasemekana historia ya yesu ilikuwa inaelezwa kuwa Masimulizi kumhusu yesu yalikuwa yakifahamika kwa watu wengi Sana kwa muda mchache.
kulingana na Injili ya yohana Yesu alifanya kazi kwa muda wa mwaka mmoja tu na kulingana na injili za ki"synoptikia" (synoptic gospels) Yaani Luka matayo na marko alifanya kazi kwa muda wa miaka 2 mpaka mitatu kabla ya kifo chake...
Japo kuliandikwa Vitabu vingi sana zaidi ya 100 kuhusu maisha ya Yesu lakini vitabu 4 tu vya injili ndiyo vilivyokubaliwa kuingia katika biblia rasmi iliyoamriwa kutumika...
Mengi tunayoyajua kuhusu yesu Tunayatoa katika vitabu vinne tu vya injili yaani marko,mathayo luka na yohana,japo vitabu vingine ambavyo havikuingizwa kwenye biblia bado vipo na vingi viko maktaba vimehifadhiwa kwa na unaweza ukaviita APOKRIFA GOSPELS na vina mambo mengi sana ambayo huwezi kuyakuta kwenye biblia na mara nyingi huwa hayaruhusiwi kuzungumzwa kwa uwazi na mengine utayakuta kwenye biblia..
Kwanini hawakutaka kuviingiiza kwa kisingizio cha KUVUVIWA ama canonical views ?.....
Baadhi ya Vitabu Hivyo vingine huzungumzia Maisha ya yesu akiwa na umri wa miaka 13 mpaka 29 kama kitabu cha The Gospel of Mary, Injili ya mtoto yesu na vinginevyo....
UCHAMBUZI
Dr.Elizabeth McNamer,Proffesor of theology and religious history wa rocky Mountain college Huko Billings Montana,
ambaye kwa Miaka 14 Amekuwa Mkurugenzi mkuu wa Bethsaida Biblical Archaeological Excavations in Israel ( Machimbo ya Kiakiolojia ya kiblia huko Israel) Pia ni proffesor maarufu kwa ufundishaji wake wa Maandiko huko Asia Na anaposcast yake kuhus Historia ya Biblia.Katika moja ya mahojiano yake aliwahi kunukuliwa akisema
"Ililichukua kanisa miaka isiyopungua 500 kujadili mambo mbalimbali kuhusu Yesu, na kipi kiwemo kwenye biblia na kipi kisiwemo na kipi kiandikwe na kiandikwe vipi na kipi kiachwe kabisa na kisizungumzwe tena Na wengi hawajui kuwa kuandikwa kwa biblia ya sasa kulichukua miaka mingi sana ,Huku pia kanisa likijadili Yesu anatakiwa kuonekana vipi mbele za jamii..."
Hiyo ni wakati akijibu moja ya maswali kuhusu kitabu chake cha Jesus and First-Century Christianity in Jerusalem by Elizabeth McNamer,
Kutokana na kutokuonekana kwa historia ya Yesu Katika miaka 18, hii ni kuanzia miaka 13 mpaka miaka 29 kwenye biblia kumezua mijadala mingi sana katika Jukwaa la wana theolojia na wasomi wa dini wabobezi wa kikristo mpaka ikafika hatua Wakaunda theory zao ama hypothetical Views zao na Wote wakaipa majina miaka hii kama.. The lost years of Jesus Christ "Miaka iliyopotea ya Hostori ya Yesu kristo" na wengine waliita "The unaccounted years of Jesus Christ" Pia huitwa the silent years au the missing years ...
MILA NA DESTULI ZA KIYAHUDI KUHUSU MIAKA ILIYOPOTEA YA YESU NA CHANZO CHA NADHARIA
Hapa tutaangalia mila na desturi za kiyahudi kuhusu miaka hiyo inayosemekana kutokupatikana historia ya yesu Kama wewe ni mfatiliaji wa mila na desturi za kiyahudi na kiAramaiki utakuwa si mgeni wa maneno kama Bar-Mitzvah au Bat-Mitzvah..
Hizi ni mila kama mila za kwetu africa au kwetu huko uziguani,Au huko kwetu uzaramoni au umasaini na kwingineko...
Kwakuwa yesu alikuwa ni mmoja wa Wayahudi katika kabila la kiAramaic hivo alifata Tamaduni zote..
"Bar Mitzvah" maana yake halisi ni "mwana (wa kiume) mwenye amri." "Bar" ni "mwana wa kiume" katika Kiaramu, ambayo ilikuwa ni lugha ya watu wa Kiyahudi.
"Mitzvah" ni "amri" katika Kiebrania na Kiaramu.
"Bat" ni binti katika Kiebrania na Kiaramu. (Matamshi ya Ashkenazic ni "bas").
Kitaalamu,Maneno hayo humaanisha mtoto anayekua, na ni sahihi kabisa kwa mila za kiyahudi kumuita mtu kama "kuwa bar (au bat) mitzvah.
"Hata hivyo, neno hili linatumika zaidi ku sherehe za ukuaji zenyewe, na kuna uwezekano mkubwa wa kusikia kwamba mtu "ana bar mitzvah" au "alialikwa kwenye bar mitzvah."
Sasa sherehe hizi zikuwaje na zilimaanisha nini
Mtoto wa kiyahudi zamani hizo mpaka leo kwa kufata sheria za Musa (zilizopo kwenye talmud) Anapofikisha umri wa miaka 13 (kwa mtoto wa kiume) na miak 12 (kwa mtoto wa kike) huhesabika kama amekuwa na hufanyiwa sherehe hiyo ya Mitzvah ili ayavae majukumu yake mapya na ieleweke kwamba mtoto akishafanyiwa sherehe hii hawi tena chini ya uangalizi wa wazazi hiyo umaanisha kwamba hawi chini ya amri ya wazazi na ndo maana ikaitwa Bar/Bat mitzvah..
Na ni mujibu baba kufurahi na kumpa maneno mazuri ya wosia mtoto huyo kwani Baba amejitoa katika responsibikity za mtoto huyo kwahyo dhambi zake na maamuzi huwa yapo chini ya mtoto (hapo mwanzo kabla ya miaka 13 mtoto huwa chini ya kifungo cha miaka na wazazi wake hivyo dhambi na malezi yote huwa chini ya wazazi wake) sherehe hizi hufanyika siku ya sabato....
Na mtoto huwa na ruksa ya kwenda mahali popote atakapo..
(Rejea ya Tamaduni hii ipo katika kitabu cha Talmud na inafanywa na wayahudi mpaka leo)..
Mila hizi zinahusianaje sasa na upotevu wa maisha ya yesu kuanzia miaka 13-29?
Inasemekana kwamba baada ya yesu kuwa tayari amekuwa Bar-Mitzvah akiamua kwenda sehemu mbalimbali kutafuta Elimu huku akiiacha Yerusalem na kurafuta elimu sehemu mbalimbali za nchi zote duniani na Hatimae kurudi Akiwa na miaka 30
(Ambayo pia ni miaka ya Kuhubiri na utume kwa mujibu wa Talmud)
Katika miaka ya 1800-1900 kuliibuka nadharia "Hypothetical views" nyingi sana kuhusu the lost years of jesus christ,Japo wanatheolojia wengi wa kisasa yaani morden theologists wanasema kuwa Yesu aliishi Nazareth na alikuwa akifanya kazi na baba ake kama fundi selemala Japo hili linakosa ushahidi zaidi wa moja kwa moja wa kimaandiko kwenye biblia zaidi ya ushahidi wa mathayo 13:55 na Marko 6:3 japo ukiangalia vizur utagundua ni andiko moja lenye sentensi moja na lenye maana tofauti huku kwwnye mathayo limetajwa tofauti na kwenye marko limetajwa tofauti labda ni katika zile njama Dr Elizabeth McNamer alizokuwa akitueleza..sasa twende kwwnye nadharia hizo kuhusu miaka iliyopotea .....
1.EARLY THORIES (about early as possible as 70-1600 Ad)
Nadharia za awali Kuwa kuna uthibitisho gani unaounga mkono imani kwamba Yesu alisafiri maelfu ya maili kutoka Yudea hadi nchi nyingine?
Vyanzo vya kwanza kabisa vinatoka katika maandiko ya Injili ya Mathayo, Marko, Luka na Yohana. Bethlehemu ni mahali ambapo inaaminika kuwa Kristo alizaliwa, lakini Injili zinasema familia yake iliondoka mara baada ya hapo na kukaa katika mji wa Nazareti, kutimiza yale ambayo manabii katika Biblia walitabiri; kwamba Yesu ataitwa Mnazareti. Nazareti lilikuwa eneo tulivu, la kilimo na la uvuvi ambapo jamii iliishi maisha yasiyofaa, ikidokeza kwamba hadhi ya Yesu ilikuwa ‘Blue collar’ huku yeye na baba yake seremala
Yusufu wakipata riziki zao duni kama mafundi. Huku kukiwa na matarajio machache ya kazi, nadharia moja ni kwamba huenda Yesu alitafuta kazi fulani umbali wa maili tatu katika mji wenye shughuli nyingi wa Sepphoris katika eneo la kati la Galilaya katika Israeli ya leo, mji uliojulikana wakati huo kwa michoro yake maridadi sana iliyotengenezwa na Waruma. Kukiwa na fursa nyingi za kujenga nyumba na kuta,
Huenda mji huu ukawa ndio hatua ya kwanza kuelekea mahali panapoaminika kuwa mahali pa kuanzia kwa jitihada ya Yesu ya kupata nuru ya kiroho. Ikiwa kama vile wasomi fulani Wakristo wanavyoamini kwamba Yesu alitumia muda mwingi wa miaka hii ya kati akifanya kazi ya seremala katika Galilaya, kuna marejezo machache kuhusu hilo katika Biblia. Pengo la miaka kumi na minane katika maandiko limetokeza nadharia kadhaa za kushangaza, lakini hadi sasa hakuna iliyothibitishwa na ushahidi wa kutegemewa.
2.WALKABOUT (MATEMBEZI)
Nadharia nyingine ni kuhusu Yesu na miaka yake iliyopotea ni kwamba alienda ‘kutembea’ kutoka nyumbani kwao Nazareti. Ikiwa tukio hili linatokea Yesu alikuwa mvulana wa miaka 12, kwa hiyo kijana kama huyo anaonekana alikuwa na uwezo upi wa kihisia-moyo na ujuzi gani ili kuchukua safari kubwa na inayoweza kuwa hatari? Sawa endelea
Yaelekea zaidi alipokuwa akiishi Sepphoris, Kijana Yesu anaweza kuwa alipata ujuzi wake wa mapema wa ulimwengu kupitia lugha ya Kiaramu na kujifunza kusoma. Andiko moja linalodokeza hilo linapatikana katika Injili ya Luka, inayosema kwamba Yesu aliingia katika sinagogi na kusoma kitabu cha kukunjwa cha manabii. Wakati huu akiwa kijana, angepitia moja kwa moja unyanyasaji wa kijamii na kiuchumi wa wakulima wa Kiyahudi wa Kipalestina wa wakati wake, ambao alikuwa sehemu yao. Huenda ujuzi huo ndio uliomtia moyo Yesu kutafuta majibu katika ulimwengu wa nje na huenda ukawa na uvutano juu ya uamuzi wenye utata wa kuacha familia yake.
Wasomi wa elimu ya Historia ya kidini wanaamini kwamba
Yosefu baba wa Yesu alikufa alipokuwa na umri wa miaka 12 hivi na kwamba tukio hilo lenye kuhuzunisha ndio lilikuwa kichocheo kwake, akiwa bado mvulana mdogo, kuanza jitihada ya kibinafsi ya kupata nuru ya kiroho. 'Matembezi' haya yaliyodumu kwa takriban miongo miwili yanaweza kuwa yalianza muda mfupi baada ya kuwa na umri wa miaka 13. Ni katika umri huu hatari ambapo madai ya ‘mengi ya miaka 18 uya upotevu wa historia ya yesu’ huanza na nadharia nyingi za mahali ambapo Yesu alitumia miaka yake ya malezi kukua na kuwa mtu mzima ziko wazi kwa tafsiri nyingi.
Haidhuru Kijana yesu alikuwa na jukumu gani kwa mama yake na jamaa zake huko Nazareti,
ulikuwa uamuzi wenye kutatanisha kuwaacha watu wake wa karibu katika umri mdogo kama huo, alipokuwa akianza safari ya ajabu na hatari kwa miguu. Hata hivyo, baadhi ya Wakristo wanaamini kuwa miaka iliyokosekana haina matokeo madogo na ufunuo wowote kuihusu hauwezi kuleta mabadililko yoyote...
3.VATICAN'S SECRETS (Siri za Vatikani)
Kumekuwa na uvumi kwa miaka mingi kwamba Vatican ina ushiikilia ukweli huu kuhusu maisha ya Yesu na miaka kumi na minane iliyopotea,kwa madai kuwa Habari hizo zinaweza kubadilisha sana imani ya dini ya kikristo ya leo,
Hata hivyo hakuna kilichofichuliwa kuhusu kuwepo kwa hati hizo na kile ambacho Yesu alikuwa akifanya na mahali alipokuwa kuanzia umri wa miaka 13 hadi 30. Baadhi ya watafiti wanaamini kwamba alitumia miaka hii isiyo andikwa kusafiri kwenda Uingereza akiwa na 'Yosefu wa Arimathaya', huku wengine wanaamini alisafiri hadi India na Uajemi. Mwishoni mwa karne ya 19 msafiri Mrusi Aitwaye Nicolas Notovitch alidai kwamba aligundua maandishi ya kweli katika nyumba ya watawa huko India ambayo yalithibitisha kwamba Yesu alisafiri na kufundisha huko na kwingineko Mashariki.
ZIKO THEORY NYINGI SANA NITAENDELEA KUZINDIKA KADRI NIPATAVYO UWEZO
CLARIFICATION
To declare interest "Part of the story was done on wasafi Tv the "storybook"
Kabla ya yote ningependa kurejea Luka 1:1-3 Kama inavyosema;
..."Kwa kuwa watu wengi wametia mikono kutunga kwa taratibu habari za mambo yale yaliyotimizwa katikati yetu,kama walivyotuhadithia wale waliokuwa mashahidi wenye kuyaona, na watumishi wa lile neno tokea mwanzo,nimeona vema mimi nami, kwa kuwa nimejitafutia usahihi wa mambo hayo yote tangu mwanzo, kukuandikia kwa taratibu,.........,"
Miaka 2000 iliyopita katika Mji wa bathelehem ya Uyahudi Alizaliwa Mtoto Aliyepewa Jina la Yeshua/Yehoshua ama yesu au Issa unaweza kumuita utakavyoweza kuita kwa lugha yako ilimradi imani ibaki kuwa alizaliwa Mtoto Ambaye ni Mtu muhimu sana katika historia ya ukombozi wa Wakristo duniani,
Na maandiko yote Yameandika kuhusu yesu kuzaliwa kwake,Miujiza yake mafundisho yake kuishi kwake ,Kusulubiwa kwake na kufufuka kwake na hata kupaa kwake kwenda mbinguni.
Maandiko yote ya biblia yaliyopo yanaanza kuzungumzia yesu kuanzia alipokuwa anazaliwa mpaka akiwa na umri wa miaka 12 (Soma luka 2 yote,pia soma mathayo 2)
Lakini baada ya miaka hiyo 12 Biblia ikawa kimya mpaka tena pale ambapo yesu anatimiza miaka 30 ya maisha yake ndo tunaona yesu anaanza kutajwa tena,kipindi anabatizwa na yohana Mbatizaji..(luka 3:23,Marco 1;9 ,Mathayo 3 kuanzia aya ya 14 na kuendelea)
Lakini miaka yake yote kuanzia umri wa miaka 13 mpaka 29 hakuna sehemu yoyote ya biblia inayotaja maisha yake alikuwa wapi? Alifanya nini? Aliishi wapi? na ilikuwaje?
basi nitajaribu kupitia baadhi ya theory na nakala za vitabu ili tuende sawa katika kujibu haya
HOJA KWA UFUPI
Maisha ya yesu kipindi Akiwa hai hakuna aliyekuwa anayanakili ama kuandika maisha yake kwakuwa Maisha yake na injili hii imekuja kuandikwa Miaka 70 mpaka 140 baada ya kifo chake.
Japo inasemekana historia ya yesu ilikuwa inaelezwa kuwa Masimulizi kumhusu yesu yalikuwa yakifahamika kwa watu wengi Sana kwa muda mchache.
kulingana na Injili ya yohana Yesu alifanya kazi kwa muda wa mwaka mmoja tu na kulingana na injili za ki"synoptikia" (synoptic gospels) Yaani Luka matayo na marko alifanya kazi kwa muda wa miaka 2 mpaka mitatu kabla ya kifo chake...
Japo kuliandikwa Vitabu vingi sana zaidi ya 100 kuhusu maisha ya Yesu lakini vitabu 4 tu vya injili ndiyo vilivyokubaliwa kuingia katika biblia rasmi iliyoamriwa kutumika...
Mengi tunayoyajua kuhusu yesu Tunayatoa katika vitabu vinne tu vya injili yaani marko,mathayo luka na yohana,japo vitabu vingine ambavyo havikuingizwa kwenye biblia bado vipo na vingi viko maktaba vimehifadhiwa kwa na unaweza ukaviita APOKRIFA GOSPELS na vina mambo mengi sana ambayo huwezi kuyakuta kwenye biblia na mara nyingi huwa hayaruhusiwi kuzungumzwa kwa uwazi na mengine utayakuta kwenye biblia..
Kwanini hawakutaka kuviingiiza kwa kisingizio cha KUVUVIWA ama canonical views ?.....
Baadhi ya Vitabu Hivyo vingine huzungumzia Maisha ya yesu akiwa na umri wa miaka 13 mpaka 29 kama kitabu cha The Gospel of Mary, Injili ya mtoto yesu na vinginevyo....
UCHAMBUZI
Dr.Elizabeth McNamer,Proffesor of theology and religious history wa rocky Mountain college Huko Billings Montana,
ambaye kwa Miaka 14 Amekuwa Mkurugenzi mkuu wa Bethsaida Biblical Archaeological Excavations in Israel ( Machimbo ya Kiakiolojia ya kiblia huko Israel) Pia ni proffesor maarufu kwa ufundishaji wake wa Maandiko huko Asia Na anaposcast yake kuhus Historia ya Biblia.Katika moja ya mahojiano yake aliwahi kunukuliwa akisema
"Ililichukua kanisa miaka isiyopungua 500 kujadili mambo mbalimbali kuhusu Yesu, na kipi kiwemo kwenye biblia na kipi kisiwemo na kipi kiandikwe na kiandikwe vipi na kipi kiachwe kabisa na kisizungumzwe tena Na wengi hawajui kuwa kuandikwa kwa biblia ya sasa kulichukua miaka mingi sana ,Huku pia kanisa likijadili Yesu anatakiwa kuonekana vipi mbele za jamii..."
Hiyo ni wakati akijibu moja ya maswali kuhusu kitabu chake cha Jesus and First-Century Christianity in Jerusalem by Elizabeth McNamer,
Kutokana na kutokuonekana kwa historia ya Yesu Katika miaka 18, hii ni kuanzia miaka 13 mpaka miaka 29 kwenye biblia kumezua mijadala mingi sana katika Jukwaa la wana theolojia na wasomi wa dini wabobezi wa kikristo mpaka ikafika hatua Wakaunda theory zao ama hypothetical Views zao na Wote wakaipa majina miaka hii kama.. The lost years of Jesus Christ "Miaka iliyopotea ya Hostori ya Yesu kristo" na wengine waliita "The unaccounted years of Jesus Christ" Pia huitwa the silent years au the missing years ...
MILA NA DESTULI ZA KIYAHUDI KUHUSU MIAKA ILIYOPOTEA YA YESU NA CHANZO CHA NADHARIA
Hapa tutaangalia mila na desturi za kiyahudi kuhusu miaka hiyo inayosemekana kutokupatikana historia ya yesu Kama wewe ni mfatiliaji wa mila na desturi za kiyahudi na kiAramaiki utakuwa si mgeni wa maneno kama Bar-Mitzvah au Bat-Mitzvah..
Hizi ni mila kama mila za kwetu africa au kwetu huko uziguani,Au huko kwetu uzaramoni au umasaini na kwingineko...
Kwakuwa yesu alikuwa ni mmoja wa Wayahudi katika kabila la kiAramaic hivo alifata Tamaduni zote..
"Bar Mitzvah" maana yake halisi ni "mwana (wa kiume) mwenye amri." "Bar" ni "mwana wa kiume" katika Kiaramu, ambayo ilikuwa ni lugha ya watu wa Kiyahudi.
"Mitzvah" ni "amri" katika Kiebrania na Kiaramu.
"Bat" ni binti katika Kiebrania na Kiaramu. (Matamshi ya Ashkenazic ni "bas").
Kitaalamu,Maneno hayo humaanisha mtoto anayekua, na ni sahihi kabisa kwa mila za kiyahudi kumuita mtu kama "kuwa bar (au bat) mitzvah.
"Hata hivyo, neno hili linatumika zaidi ku sherehe za ukuaji zenyewe, na kuna uwezekano mkubwa wa kusikia kwamba mtu "ana bar mitzvah" au "alialikwa kwenye bar mitzvah."
Sasa sherehe hizi zikuwaje na zilimaanisha nini
Mtoto wa kiyahudi zamani hizo mpaka leo kwa kufata sheria za Musa (zilizopo kwenye talmud) Anapofikisha umri wa miaka 13 (kwa mtoto wa kiume) na miak 12 (kwa mtoto wa kike) huhesabika kama amekuwa na hufanyiwa sherehe hiyo ya Mitzvah ili ayavae majukumu yake mapya na ieleweke kwamba mtoto akishafanyiwa sherehe hii hawi tena chini ya uangalizi wa wazazi hiyo umaanisha kwamba hawi chini ya amri ya wazazi na ndo maana ikaitwa Bar/Bat mitzvah..
Na ni mujibu baba kufurahi na kumpa maneno mazuri ya wosia mtoto huyo kwani Baba amejitoa katika responsibikity za mtoto huyo kwahyo dhambi zake na maamuzi huwa yapo chini ya mtoto (hapo mwanzo kabla ya miaka 13 mtoto huwa chini ya kifungo cha miaka na wazazi wake hivyo dhambi na malezi yote huwa chini ya wazazi wake) sherehe hizi hufanyika siku ya sabato....
Na mtoto huwa na ruksa ya kwenda mahali popote atakapo..
(Rejea ya Tamaduni hii ipo katika kitabu cha Talmud na inafanywa na wayahudi mpaka leo)..
Mila hizi zinahusianaje sasa na upotevu wa maisha ya yesu kuanzia miaka 13-29?
Inasemekana kwamba baada ya yesu kuwa tayari amekuwa Bar-Mitzvah akiamua kwenda sehemu mbalimbali kutafuta Elimu huku akiiacha Yerusalem na kurafuta elimu sehemu mbalimbali za nchi zote duniani na Hatimae kurudi Akiwa na miaka 30
(Ambayo pia ni miaka ya Kuhubiri na utume kwa mujibu wa Talmud)
Katika miaka ya 1800-1900 kuliibuka nadharia "Hypothetical views" nyingi sana kuhusu the lost years of jesus christ,Japo wanatheolojia wengi wa kisasa yaani morden theologists wanasema kuwa Yesu aliishi Nazareth na alikuwa akifanya kazi na baba ake kama fundi selemala Japo hili linakosa ushahidi zaidi wa moja kwa moja wa kimaandiko kwenye biblia zaidi ya ushahidi wa mathayo 13:55 na Marko 6:3 japo ukiangalia vizur utagundua ni andiko moja lenye sentensi moja na lenye maana tofauti huku kwwnye mathayo limetajwa tofauti na kwenye marko limetajwa tofauti labda ni katika zile njama Dr Elizabeth McNamer alizokuwa akitueleza..sasa twende kwwnye nadharia hizo kuhusu miaka iliyopotea .....
1.EARLY THORIES (about early as possible as 70-1600 Ad)
Nadharia za awali Kuwa kuna uthibitisho gani unaounga mkono imani kwamba Yesu alisafiri maelfu ya maili kutoka Yudea hadi nchi nyingine?
Vyanzo vya kwanza kabisa vinatoka katika maandiko ya Injili ya Mathayo, Marko, Luka na Yohana. Bethlehemu ni mahali ambapo inaaminika kuwa Kristo alizaliwa, lakini Injili zinasema familia yake iliondoka mara baada ya hapo na kukaa katika mji wa Nazareti, kutimiza yale ambayo manabii katika Biblia walitabiri; kwamba Yesu ataitwa Mnazareti. Nazareti lilikuwa eneo tulivu, la kilimo na la uvuvi ambapo jamii iliishi maisha yasiyofaa, ikidokeza kwamba hadhi ya Yesu ilikuwa ‘Blue collar’ huku yeye na baba yake seremala
Yusufu wakipata riziki zao duni kama mafundi. Huku kukiwa na matarajio machache ya kazi, nadharia moja ni kwamba huenda Yesu alitafuta kazi fulani umbali wa maili tatu katika mji wenye shughuli nyingi wa Sepphoris katika eneo la kati la Galilaya katika Israeli ya leo, mji uliojulikana wakati huo kwa michoro yake maridadi sana iliyotengenezwa na Waruma. Kukiwa na fursa nyingi za kujenga nyumba na kuta,
Huenda mji huu ukawa ndio hatua ya kwanza kuelekea mahali panapoaminika kuwa mahali pa kuanzia kwa jitihada ya Yesu ya kupata nuru ya kiroho. Ikiwa kama vile wasomi fulani Wakristo wanavyoamini kwamba Yesu alitumia muda mwingi wa miaka hii ya kati akifanya kazi ya seremala katika Galilaya, kuna marejezo machache kuhusu hilo katika Biblia. Pengo la miaka kumi na minane katika maandiko limetokeza nadharia kadhaa za kushangaza, lakini hadi sasa hakuna iliyothibitishwa na ushahidi wa kutegemewa.
2.WALKABOUT (MATEMBEZI)
Nadharia nyingine ni kuhusu Yesu na miaka yake iliyopotea ni kwamba alienda ‘kutembea’ kutoka nyumbani kwao Nazareti. Ikiwa tukio hili linatokea Yesu alikuwa mvulana wa miaka 12, kwa hiyo kijana kama huyo anaonekana alikuwa na uwezo upi wa kihisia-moyo na ujuzi gani ili kuchukua safari kubwa na inayoweza kuwa hatari? Sawa endelea
Yaelekea zaidi alipokuwa akiishi Sepphoris, Kijana Yesu anaweza kuwa alipata ujuzi wake wa mapema wa ulimwengu kupitia lugha ya Kiaramu na kujifunza kusoma. Andiko moja linalodokeza hilo linapatikana katika Injili ya Luka, inayosema kwamba Yesu aliingia katika sinagogi na kusoma kitabu cha kukunjwa cha manabii. Wakati huu akiwa kijana, angepitia moja kwa moja unyanyasaji wa kijamii na kiuchumi wa wakulima wa Kiyahudi wa Kipalestina wa wakati wake, ambao alikuwa sehemu yao. Huenda ujuzi huo ndio uliomtia moyo Yesu kutafuta majibu katika ulimwengu wa nje na huenda ukawa na uvutano juu ya uamuzi wenye utata wa kuacha familia yake.
Wasomi wa elimu ya Historia ya kidini wanaamini kwamba
Yosefu baba wa Yesu alikufa alipokuwa na umri wa miaka 12 hivi na kwamba tukio hilo lenye kuhuzunisha ndio lilikuwa kichocheo kwake, akiwa bado mvulana mdogo, kuanza jitihada ya kibinafsi ya kupata nuru ya kiroho. 'Matembezi' haya yaliyodumu kwa takriban miongo miwili yanaweza kuwa yalianza muda mfupi baada ya kuwa na umri wa miaka 13. Ni katika umri huu hatari ambapo madai ya ‘mengi ya miaka 18 uya upotevu wa historia ya yesu’ huanza na nadharia nyingi za mahali ambapo Yesu alitumia miaka yake ya malezi kukua na kuwa mtu mzima ziko wazi kwa tafsiri nyingi.
Haidhuru Kijana yesu alikuwa na jukumu gani kwa mama yake na jamaa zake huko Nazareti,
ulikuwa uamuzi wenye kutatanisha kuwaacha watu wake wa karibu katika umri mdogo kama huo, alipokuwa akianza safari ya ajabu na hatari kwa miguu. Hata hivyo, baadhi ya Wakristo wanaamini kuwa miaka iliyokosekana haina matokeo madogo na ufunuo wowote kuihusu hauwezi kuleta mabadililko yoyote...
3.VATICAN'S SECRETS (Siri za Vatikani)
Kumekuwa na uvumi kwa miaka mingi kwamba Vatican ina ushiikilia ukweli huu kuhusu maisha ya Yesu na miaka kumi na minane iliyopotea,kwa madai kuwa Habari hizo zinaweza kubadilisha sana imani ya dini ya kikristo ya leo,
Hata hivyo hakuna kilichofichuliwa kuhusu kuwepo kwa hati hizo na kile ambacho Yesu alikuwa akifanya na mahali alipokuwa kuanzia umri wa miaka 13 hadi 30. Baadhi ya watafiti wanaamini kwamba alitumia miaka hii isiyo andikwa kusafiri kwenda Uingereza akiwa na 'Yosefu wa Arimathaya', huku wengine wanaamini alisafiri hadi India na Uajemi. Mwishoni mwa karne ya 19 msafiri Mrusi Aitwaye Nicolas Notovitch alidai kwamba aligundua maandishi ya kweli katika nyumba ya watawa huko India ambayo yalithibitisha kwamba Yesu alisafiri na kufundisha huko na kwingineko Mashariki.
ZIKO THEORY NYINGI SANA NITAENDELEA KUZINDIKA KADRI NIPATAVYO UWEZO
CLARIFICATION
To declare interest "Part of the story was done on wasafi Tv the "storybook"