Miaka 15 ya kifo cha Horace Kolimba

Miaka 15 ya kifo cha Horace Kolimba

Una ushahidi ? Watu wengine mnaitafutia serikali lawama ,wangapi wamesema makubwa ndani ya bunge na hadi hii leo wapo ,yaani ukiwa bungeni huwezi kufikiwa na kifo au na maradhi ya ghafla na kupoteza uhai ???

Vp ndugu nani kaisema serikali?
 
manda1.jpg
 
Nani aeleze kwa kina sababu za Kolimba kutofautina na Mwl? Na ilikuwaje afe ghafla baada ya kuhojiwa?! Kilicho mfanya akahojiwe bila shaka hakikuwapendeza walio muita wakamhoji?! Mwenye kujua mengi hebu afanye udadavuzi ili na sisi vijana wa leo akiili zetu zikakavue.
 
Hivi serikali hii ya CCM imeshaua watu wangapi? anayejua tafadhali atujuze
 
Hao hawana Ujasiri wa kuongea kama Kolimba,sioni kama CCM ya Sasa inamtu Jasiri
 
Nawe una matatizo wewe ni mungu nadra maana yake nini mwanaadamu anaweza kuugua lolota akafariki.kama ccm iliweza kuwaondoa akina seif sharf hamad na wenzake hivi kolimba angekuwa tishio gani after all he was not popular nor poweful in his party
 
Horace Kolimba alianza kuropoka, kumbe ccm walivyochunguza wakabaini alikuwa anawasiliana na Oscar Kambona miaka mitatu iliyopita. Na kwa nafasi ya Kolimba ndani ya ccm ilikuwa nzito sana, na siasa za ushawishi wa Oscar Kambona zilikuwa za mapigo ya hali ya juu, japo mzee Kambona alikuwa ashazeeka na hana nguvu. Kambona naye alikufa mwaka huo huo 1997, baadaye nyerere akafuatia 1999.
 
RIP
Kijana wako DEO FILIKUNJOMBE
m Ludewa mwenzio
Amekesha leo kuendeleza kazi yako
 
Horace Kolimba alianza kuropoka, kumbe ccm walivyochunguza wakabaini alikuwa anawasiliana na Oscar Kambona miaka mitatu iliyopita. Na kwa nafasi ya Kolimba ndani ya ccm ilikuwa nzito sana, na siasa za ushawishi wa Oscar Kambona zilikuwa za mapigo ya hali ya juu, japo mzee Kambona alikuwa ashazeeka na hana nguvu. Kambona naye alikufa mwaka huo huo 1997, baadaye nyerere akafuatia 1999.


Zinc,

Kama Koimba alianza kuwasiliana na Kambona miaka minne nyuma, basi kwa kuwa alikufa mwaka 1997 basi mawasiliano na Kambona ilikuwa mwaka 1994.

Je, hiyo 1994 kulitokea nini kikubwa hapa nchini? Mwaka huo ndipo hoja ya Kolimba ilipopigwa chini ya kutaka serikali tatu baada ya Nyerere kuandika kitabu chake cha UONGOZI WETU NA HATIMA YA TANZANIA.

December mwaka ho Kolimba akalazimishwa ku-resign kama Secretary-General wa CCM.

Sasa najaribu kuangalia ushawishi wa Kambona ulikuwa vipi wakati mwaka uliofuata alirudi nchini tena akawa mwanachama wa TADEA.

Cc:

Matoi
 
RIP Chacha Wangwe..mbona huyu alipingana na mwenyekiti wenu waziwazi na alikufa ghafla so watu waseme mlihusika!?
 
Kauli yake bado ni valid "CCM haina dira wala mwelekeo" RIP Kolimba
 
Ndivyo ilivyo, kamkosoe shetani hadharani uone atakufanya nini! ukishazoea kula nyama za watu huwezi kuacha utaendelea kula tu!
 
Mwezi wa kumbukumbu za vifo vya wengi
  • Mwl Nyerere
  • Kolimba
  • Filikunjombe
  • Mtikila
  • !
 
Back
Top Bottom