Mheshimiwa Rais, ikikupendeza uwashauri vijana waachane na madesa, wasome vitabu!

Mikopo Chefuchefu

JF-Expert Member
May 15, 2017
3,373
6,756
Mheshimiwa Rais, ikikupendeza uwashauri vijana waachane na madesa, wasome vitabu!

Sijawahi ona wanafunzi wavivu wa kusoma vitabu kama wanafunzi wa vyuo vikuu.
Wao kazi yao kubwa ni kusoma madesa (zile notes zinazotolewa na wakufunzi), kupiga group discussion basi. Kazi ndio inakuwa imeishia hapo.

Mwalimu akija kutoa mitihani definitely atabase kwenye yale madesa yake hivyo kuwawezesha wanafunzi wengi kufaulu vizuri tu. Lakini kiuhalisia hili huwafanya wanafunzi wengi wa vyuo vikuu kuwa weupee vichwani.

Yani ukikutana nao hata kwenye interveiw, wanapita tu kwa kuwa kampuni inahitaji watumishi, na wengi wako ivyo hivyo.
Hili hufanya taifa liwe na wataalam wengi vilaza ambao hawawezi kufikiria nje ya box.

Mimi nilipokuwa nasoma chuo, sikufanikiwa kupata GPA kubwa, lakini niliweka bidii ya kuitumia vizuri library ya chuo na hii imenisaidia sana kuweza kuwa deep kwenye fani yangu kiasi kwamba nikiomba kazi, huwa siulizwagi vyeti na huu ni mwaka wa nane sijawahi kurudi kuchukua cheti ili niweze kupata ajira.

Yani kuna graduates wengine unakutana nao unashindwa kuamini kama kweli mtu alimaliza chuo kikuu, angalau mpaka alete cheti. Wengi ni weupe sana.

Library mpya ikitumika vizuri, angalau itawawezesha wanafunzi wengi kuwa na content kwenye vichwa vyao.

ujinga.jpg
 
Hivi yeye "Phd ya maganda ya korosho" aliipataje?
Dah! Mheshimiwa alikomaaa. Alikuwa hata msosi anagonga pale kwenye kafteria ya wanafunzi ya DARUSO. Alikuwa sio mtu wa kuremba. Tena alivyokuwa anakuja chuo kupiga msuli, alikuwa haji kama waziri. Nasikia alikuwa anachukua Benzi lake, anajiendesha mwenyewe huyoo mpaka chuo, anapiga msuli then anaenda zake kama mtu wa kawaida tu.
Yani ungekutana naye wakati ule, wala hata usingejua kama ni government senior minister!
 
Nilimsikia tajiri Wa hotel moja kule Mtwara akilalamika M/kazi ana elimu ya Chuo kikuu hajui taratibu za kuandika barua za kiofisi nilishangaa sana nawe umenikumbusha halafu tunalalamika Wakenya kushika soko la ajira nchini
 
"Elimu haijashuka, mbona kuna panya wanafundishwa kutegua mabomu kule SUA"- Dr JP Magufuli

Hiyo hapo ni moja ya kauli yake kuhusu hali ya elimu hapa nchini. Sasa sijui unavyozungumzia kutumia madesa sidhani kama Raisi wetu mtakatifu na mwenye akili sana kuliko watanzania wote atakuelewa kabisa.
Lakini kubwa zaidi nadhani suala la kutumia madesa huko chuoni ni utamaduni mbovu ambao ulianzishwa na wanazuoni wa kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam.


Kubwa la kulifahamu ni hili hapa,
Wasomi wa Tanzania hawana utamaduni wa kupenda kuandika na kufanya tafiti mpaka pale wanapoona wana maslahi ya kipesa au vyeo. Kama wanazuoni hawaandiki machapisho mengi unategemea wanafunzi watakuwa ni watu wa kujisomea ??? Ukienda kwenye maktaba za vyuo vikuu, asilimia 80% ya vitabu vinavyotumia kufundishia ni vile ambavyo vimetoka nje ya nchi.


Wazawa hawaandiki kabisaa, na kama wakiandika basi tegemea haya yafuatayo:
1. Ni makala kwenye majarida ya kitaaluma (Journals)
2. Au kitabu kipo chini ya kiwango kwa kukosa utafiti na rejea za kutosha.


Nchini Kenya na Nigeria, ukiingia kwenye maktaba zao utakuta vitabu vilivyoandikwa na wakenya ni kama asilimia 50%. Makala kwenye majarida ya kitaaluma ndiyo usiseme, sasa watu kama hawa hata wanafunzi wao lazima wawe ni watu makini. Lakini leo mwalimu awe anatoa videsa tu na kwa mwaka amejitahidi sana ni amechapisha mara tano hivi, utagemea wanafunzi wake watakuwa ni wasoma vitabu ?

Profesa aliyekaa kazini miaka 10 unakuta ana kitabu kimoja tu....
Kazi kwelikweliiiii.
 
nikiwa chuo kikuu kimoja hapa nchini (kila mtu hapa jf ana elimu ya chuo kikuu hahaha!, ila mimi nilikomea semester ya 3, nikamuiga baba wa Microsoft) tulikuwa tunanakili assignment ya mtu mmoja darasa zima na zisahihishwa na wote tunapata maksi nzuri! Alafu mkufunzi anatufundisha mbinu za kufanikiwa kwenye mitihani eti: "usiache kujibu swali kwenye mtihani hata kama hujui jibu wewe andika chochote hata kama ni story tu maana ukiacha nafasi wazi mimi nitashindwa kukuwekea maksi..." sijawahi kujuta kuacha chuo!
 
Mwezi uliopita,nilishuhudia jamaa mmoja ana GPA ya 4.2 akiaibika kwenye interview,yaani jamaa alikuwa mweupe kama sufi,kila swali hajui ata yale common kwenye field yake.Tulijiuliza sana iyo GPA alipataje
🙆🏽‍♂️🙆🏽‍♂️
 
Mheshimiwa Rais, ikikupendeza uwashauri vijana waachane na madesa, wasome vitabu!

Sijawahi ona wanafunzi wavivu wa kusoma vitabu kama wanafunzi wa vyuo vikuu.
Wao kazi yao kubwa ni kusoma madesa (zile notes zinazotolewa na wakufunzi), kupiga group discussion basi. Kazi ndio inakuwa imeishia hapo.

Mwalimu akija kutoa mitihani definitely atabase kwenye yale madesa yake hivyo kuwawezesha wanafunzi wengi kufaulu vizuri tu. Lakini kiuhalisia hili huwafanya wanafunzi wengi wa vyuo vikuu kuwa weupee vichwani.

Yani ukikutana nao hata kwenye interveiw, wanapita tu kwa kuwa kampuni inahitaji watumishi, na wengi wako ivyo hivyo.
Hili hufanya taifa liwe na wataalam wengi vilaza ambao hawawezi kufikiria nje ya box.

Mimi nilipokuwa nasoma chuo, sikufanikiwa kupata GPA kubwa, lakini niliweka bidii ya kuitumia vizuri library ya chuo na hii imenisaidia sana kuweza kuwa deep kwenye fani yangu kiasi kwamba nikiomba kazi, huwa siulizwagi vyeti na huu ni mwaka wa nane sijawahi kurudi kuchukua cheti ili niweze kupata ajira.

Yani kuna graduates wengine unakutana nao unashindwa kuamini kama kweli mtu alimaliza chuo kikuu, angalau mpaka alete cheti. Wengi ni weupe sana.

Library mpya ikitumika vizuri, angalau itawawezesha wanafunzi wengi kuwa na content kwenye vichwa vyao.

View attachment 946916
Sasa Magufuli mwenyewe umewahi kumsikia amesoma kitabu ama gazeti gani? The Economist wanampiga za chini ya mkanda kila mwezi lkn maskini wa Mungu hata haelewi kilichoandikwa, wala hajui kama anaandikwa...na tunamzungumzia mtu mkubwa nchi hii!
 
Wangekuwepo watu 10000 kama wewe nchini tungekuwa na uwezo wa kutengeneza viwanda mama, chuma tusingeagiza nje tena.
Takataka za mchina tungesahau.
Elimu, elimu, elimu.
 
Mkuu kutokana na uzoefu wangu nitakudokeza kama ifuatavyo kwa kifupi tuu;
1. Utashi wa kusoma unaanza pale mtoto anapojifunza kusoma na kuendelea katika maisha yake yote( tunaiita hii literal development of a child)
2. Utashi wa mtoto husika husukuma kupenda kusoma vitabu kutokana na mazoea, elimu, makuzi na mazingira!
3. Nafasi ya shule katika kukuza ari na motisha ya mwanafunzi kujifunza na kujiamini katika kujifunza
4. Upatikanaji wa nyenzo za kujisomea na kujengwa kwa desturi ya kujisomea
5. Mtazamo wa kitaasisi kuhusu namna ya kumjenga mwanafunzi aweze kusoma na kujisomea na kutumia maarifa- elimu husika( hapa ndipo shida ya madesa na kutotumia vitabu ilipo)
Hivyo mkuu chimbuko sio hku juu mzizi wa fitna upo tangu mtoto anapokua na hadi kufikia hyo ngazi ya chuo kikuu.
Nawasilisha!
 
Ukipata nafasi, zipitie (review) hizo papers na vitabu vyao critically and fairly.
The Washington Post: 9th December 1984
"For all its problems, this is a remarkably stable country, with dignified,
intelligent people, a high degree of religious and ethnic tolerance and many of the attributes of nationhood"

Utakuja kunielewa vizuri kipindi kizazi cha Mzee Nyerere na Mwinyi kitakapokuwa kimeondoka na nchi imeabikia na watu kama Humphrey Polepole na Le Mutuz. Hapa ndiyo tutajua kwamba tulitoa elimu bora kwa watoto wetu au lah.....

Kuhusu kupitia machapisho, ya Kenya na Naijeria. Nimeyasoma vizuri na kugundua kwamba kwenye swala zima la elimu hatuwezi kujilinganisha nao kabisa. Lengo la taaluma siyo kutoa chapisho linalokubalika asilimia 100%, bali chapisho ambalo litazaa mijadala ya kitaaluma, kualika ukosoaji, kufundisha jamii na kuwafanya wasomi wafanye tafiti zaidi.

Mantiki ya Chuo Kikuu ni kufanya tafiti (Research) na siyo kufaulisha watoto kwa alama kubwa. Kama wasomi wa nchi hawana utamaduni wa kupenda kuchapisha mpaka pale wanaptaka cheo au pesa basi nchi hiyo lazima ina matatizo makubwa mno.
 
Back
Top Bottom