Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,926
- 31,169
Wakuu si jambo jema kumtabiria kifo binadamu mwenzako ila wakati mwingine lazima tuwe realistic kidogo.Mbunge wa Arumeru Mashariki Jeremiah Solomon Sumari wakati wowote anaweza kuungana na ndugu,jamaa na marafiki waliotangulia mbele ya haki.Mheshimiwa Sumari pamoja na kuwa na elimu ndogo sana ya form four aliukwaa unaibu waziri wa fedha kwakuwa mtoto wake kamwoa mtoto wa Laigwanani mkuu Afrika Mashariki Elowasa.Taarifa za uhakika toka kwa ndugu wa karibu Mheshimiwa Sumari hali ya afya yake imezidi kudorora sana.Chama cha Magamba tayari kimeshaanza mchakato wa kumpata mtu wa kurithi mikoba yake.Jimbo la Arumeru Mashariki uenda likawa jimbo la kwanza kufanya uchaguzi muda mfupi ujao.