Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,378
- 39,315
Imeripotiwa hivi karibuni kuwa Rais Kikwete ametaka wale wote wanaofuja fedha za serikali wafikishwe polisi badala ya Taasisi ya Rushwa au kuitwa kwenye vikao vya nidhamu. Maneno hayo yamesifiwa na vyombo vya habari vya bongo na baadhi ya watu ambao upeo wao wa kufikiri umetiwa kiwingu na kutangaa kwa Mhe. Kikwete. Hata hivyo, siyo wote ambao ni vipofu!!
Mhe. Rais,
a. Ulipokuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, je kuna fedha zozote ambazo zilipotea "kiana"? Je kuna mtu yeyote chini ya iliyokuwa wizara yako ambaye alituhumiwa kufuja fedha za umma? Kama yupo, je huyo mtu amefikishwa polisi?
b. Katika nafasi yako ya sasa kama Rais wa JMT, je kuna mtu yeyote ambaye chini ya ofisi ya Rais ametuhumiwa kufuja fedha, na bado yupo kwenye nafasi yake hiyo? Je uko tayari kumsimamisha mtu huyo na kumfikisha polisi ili uchunguzi ufanywe?
c. Je kati ya mawaziri na viongozi kadhaa uliowateua tangu uchukue madaraka kuna yeyote ambaye chini ya uongozi wake kiasi cha fedha kimepotea bila maelezo ya kutosha? Je uko tayari kumsimamisha mtu/watu hao kutoka nafasi hizo ili polisi wafanye uchunguzi na ikibidi afikishwe mahakamani?
Mkono mtupu haulambwi!! na maneno matupu hayavunji mfupa!!!!! Onyesha mfano badala ya kutuzuga!!!! Kama hauko tayari kuonyesha mfano usitegemee wengine wafuate!!!!
Thanks you!!!
Mhe. Rais,
a. Ulipokuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, je kuna fedha zozote ambazo zilipotea "kiana"? Je kuna mtu yeyote chini ya iliyokuwa wizara yako ambaye alituhumiwa kufuja fedha za umma? Kama yupo, je huyo mtu amefikishwa polisi?
b. Katika nafasi yako ya sasa kama Rais wa JMT, je kuna mtu yeyote ambaye chini ya ofisi ya Rais ametuhumiwa kufuja fedha, na bado yupo kwenye nafasi yake hiyo? Je uko tayari kumsimamisha mtu huyo na kumfikisha polisi ili uchunguzi ufanywe?
c. Je kati ya mawaziri na viongozi kadhaa uliowateua tangu uchukue madaraka kuna yeyote ambaye chini ya uongozi wake kiasi cha fedha kimepotea bila maelezo ya kutosha? Je uko tayari kumsimamisha mtu/watu hao kutoka nafasi hizo ili polisi wafanye uchunguzi na ikibidi afikishwe mahakamani?
Mkono mtupu haulambwi!! na maneno matupu hayavunji mfupa!!!!! Onyesha mfano badala ya kutuzuga!!!! Kama hauko tayari kuonyesha mfano usitegemee wengine wafuate!!!!
Thanks you!!!