PreGE2025 Mhariri Daily News: Acheni kunyamazisha Uhuru wa Vyombo vya Habari, Waandishi sio Kero ni Daraja. Serikali kutoa taarifa sio ombi ni wajibu

PreGE2025 Mhariri Daily News: Acheni kunyamazisha Uhuru wa Vyombo vya Habari, Waandishi sio Kero ni Daraja. Serikali kutoa taarifa sio ombi ni wajibu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
2,786
Reaction score
7,567
Wakuu,

Baada ya Tuzo za Kalamu ya Samia Mhariri wa Gazeti la Daily News alirusha jiwe angani, akasema, wenye D mbili na hata wale wenye F wameelewa. Maana kilichofanyika pale ni kuzika uhuru wa vyombo habari, kuwazuia vidomo domo kwenye kuchimba na kuwapiga mkwara, tumewapa hela hizi sasa ole wenu mkaendeleze chokochoko, tutawanyoosha.

Nimependa jinsi mwandishi amendika kitaalamu😆😆, ujumbe umefika bila hasira. Serikali taarifa sio ombi ni wajibu wenu. Namna hiyo! Waandishi wa aina hii ndio wanaohitajika, sio mama anatosha, wakati mwenyewe anajua hatoshi:PeepoRunCry::PeepoRunCry::PeepoRunCry:

Hii hapa ni tafsiri yake ya Kiswahili.....

====

Msinyamazishe Uhuru wa Vyombo vya Habari – Waandishi ni Daraja

Serikali ilipowatambua na kuwatuza waandishi wa habari hivi karibuni kwa kazi zao (Tuzo za Kalamu ya Samia), haikuwa tu ishara ya heshima – ilikuwa ni ujumbe, ulio wazi na usiotia shaka. Uandishi wa habari si taaluma ya kalamu na vitambulisho tu; ni nguzo ya nne ya maendeleo na katika Tanzania ya leo, inabeba mzigo mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.

Kwa kuwaheshimu wataalamu wa habari, serikali imetambua kile ambacho wengi husahau: waandishi si wachochezi au wakusanya umbea. Ni wajenzi wa taifa, wakitumia vipaza sauti badala ya nyundo – lakini wanachojenga ni muhimu vilevile; na hiyo ni wananchi wenye taarifa sahihi. Katika demokrasia, hiyo ndiyo msingi wa maendeleo.

Lakini, wakati serikali inawapongeza wanahabari, bado kuna baadhi ya viongozi wa taasisi na wakuu wa wizara wanaendeleza michezo ya kuficha taarifa. Unafiki huu ni lazima ukome.


Pia soma: Tuzo za Kalamu ya Samia zimezika Uhuru wa Vyombo vya Habari, kuna aliyepewa tuzo atakuwa na ubavu wa kumkosoa Rais?

Kuna nini kinachofichwa, watumishi wa umma wenye tabia kama hizi? Hamkuajiriwa kulinda korido za wizara kama majoka ya kufikirika yanayohifadhi taarifa. Mmeaminiwa kushika nafasi za umma kwa ajili ya kuhudumia wananchi, siyo kuziba milango ya habari. Mnapowazuia waandishi kupata taarifa muhimu, hamwakatishi tamaa tu waandishi – mnawanyima Watanzania haki yao ya kujua.

Tuambiane ukweli: kodi ya wananchi ndiyo inayoendesha ofisi zenu, mafuta ya magari yenu, na pengine hata kiyoyozi kizuri mnachokifurahia katika minara yenu ya mamlaka. Hivyo basi, mwandishi anapouliza mradi unaendeleaje, bajeti imetumikaje, au maendeleo yakoje – hiyo si kuwaingilia kwenye majukumu yenu, bali ni uwajibikaji.

Hii si kuhusu majigambo au kujiona. Ni kuhusu watu wa Tanzania. Tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu, mawasiliano yanazidi kuwa muhimu – si hiari tena, ni lazima. Wananchi wanahitaji kuelewa sera, kuchambua ahadi, na kujua viongozi wao waliowachagua wanafanya nini hasa. Na ni nani anayeunganisha habari hizo kutoka meza za serikali hadi redio za vijijini? Ni waandishi wa habari.

Pia soma:
Bila waandishi kuuliza maswali magumu na kutoa majibu kwa umma, demokrasia inakuwa mchezo wa kubahatisha. Uchaguzi unakuwa mashindano ya umaarufu badala ya mwelekeo wa sera. Na wananchi? Wanabaki gizani – wakiwa wamechanganyikiwa, wamepotoshwa, au hata kudanganywa.

Nafasi ya vyombo vya habari msimu huu si chaguo, ni muhimu. Lakini ili waweze kuitumikia vema, uwazi ni lazima uwe wa pande zote. Haitoshi kwa Rais au wizara kubwa kufanya mkutano na waandishi mara kwa mara. Kila taasisi, kila idara, kila wizara lazima ichukulie mawasiliano kama jukumu la kiraia.

Hivyo basi, kwa wakuu wa taasisi wanaowachukulia waandishi kama kero: Acheni kujikweza. Hamombiwi mfichue siri au kutoa ripoti za kipelelezi – mnaombwa kueleza mnachokifanya kwenye rasilimali za umma. Hilo si neema au upendeleo – ni kazi yenu.

Na kwa waandishi huko nje: Endeleeni kusukuma. Endeleeni kuchimba. Endeleeni kuuliza. Kwa sababu mnaposema ukweli, hampati tu vichwa vya habari – mnaandika historia.

Tuache kuchukulia Uandishi wa Habari si kama Usumbufu – bali kama kioo chetu, kipaza sauti chetu, na hasa kwa sasa – njia yetu ya uhai kwenye Demokrasia.

===

Don't muzzle press freedom, journalists are bridge

When the government recently recognized and awarded journalists for their work, it was not just a gesture, it was a message, loud and clear. Journalism is not just a profession of pens and press passes. It is the fourth pillar of development and in today's Tanzania, it is holding up more weight than ever.

By honoring media professionals, the government has acknowledged what many forget: Journalists are not noisy troublemakers or gossip collectors. They are nation builders, wielding microphones instead of hammers, but constructing something just as vital and that is an informed citizenry, and in a democracy, that is the very foundation of progress.

Again, while the government is applauding the media, some institutional heads and ministry bosses are still playing hide-and-seek with information. This hypocrisy must end.

What is with the secrecy, dear public servants with such behaviours? You were not appointed to guard ministry corridors like mythical dragons hoarding data. You were entrusted with public positions to serve, not to stonewall. When you block journalists from accessing vital information, you are not just frustrating reporters, you are denying Tanzanians their right to know.

Let us be honest: Taxpayers fund your offices, fuel your cars and probably pay for that nice AC you enjoy in your ivory towers. So, when journalists ask about how projects are going, budgets are being spent, or what progress is being made, that is not intrusion, that is accountability.

This is not about ego or entitlement. It is about the people of Tanzania. As the country inches toward the general elections, communication becomes more than important, it becomes essential. Citizens need to understand policies, assess promises and hear what their elected leaders are actually doing. And guess who connects that information from government desks to village radios? Journalists.

Without reporters asking the hard questions and sharing the answers Democracy becomes a guessing game. Elections become popularity contests not policy decisions. And citizens? They remain in the dark, confused, misinformed, or even misled.

The media's role in this season is not optional, it is crucial. But for them to play that role, transparency must be a two-way street. It is not enough for The President or top ministries to host a press conference now and then. Every institution, every department, every ministry must embrace communication as a civic duty.

So, to the Heads of Institutions who still treat journalists like pests: It is time to get over yourself. You are not being asked to leak secrets or deliver Exposés, you are being asked to explain what you are doing with public resources. That's not a favor; it is your job.

And to the journalists out there: Keep pushing. Keep digging. Keep asking. Because when you speak truth, you don't just make headlines, you make history.

Let's stop treating journalism like an inconvenience. It is our mirror, our megaphone and especially now our lifeline to democracy.

Editor, Daily News
 

Attachments

  • mhariri.jpg
    mhariri.jpg
    222.8 KB · Views: 12
  • mhariri1.jpg
    mhariri1.jpg
    241.2 KB · Views: 15
TEF
DEODATUS BALILE
Pascal Mayala
Manyerere JACTON
TUjadili zana ya UHURU WA MWANDISHI
 
Nawasubiri ndugu waandishi Pascal Mayalla Robert Heriel Mtibeli na wengine tupate maoni yenu juu ya hili. Mkuu Tlaatlaah and the gang mpoo? 🌚🌚
Yes,
ni sahihi kabisa serikali kutoa taarifa kwa umma sio ombi ni wajibu,

ndio maana kila kona na kila pembe ya nchi hii kuna picha na mabango mbalimbali ya Rais yakiwa yamesheheni taarifa muhimu sana za kina za utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa mwaka 2020-2025, iliyojaa taarifa muhimu za kukamilika na kuendelea kukamilika kwa miradi mbalimbali ya Maendeleo kote nchini. Na hiyo ni njia mojawapo ya kutoa taarifa kwa umma ikiwa huyo muungwana hajieliwi.

Na zaidi sana,
hivi sasa, upo utaratibu wa serikali kupitia katibu mkuu wizara ya habari na kurugenzi ya mawasiliano Ikulu kuandaa siku maalumu kwa mawaziri, wakuu wa taasisi, mamlaka na idara za serikali kutoa taarifa muafaka za mafanikio, changamoto na way forward za sekta zao katika kuwahudumia wananchi na waTanzania wote. Na yote hayo yanafanyika kwa uwazi mbele ya waandishi wa habari.
Na mara zote inakua live, labda kama huyo muungwana ni mtu wa kususa mambo.

Lakini pia,
taarifa nyingi zaidi za serikali hutolewa kupitia vikao vya bunge la Tanazania ambalo nalo hua live.

Na uwajibikaji huo wa serikali kutoa taarifa kwa umma, uliwahi kumkera mwanasiasa moja mropokaji anaesota korokoroni hivi sasa, kwamba taarifa za utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM pembezoni mwa barabara ya namanga kuelekea Kenya zina mkera sana, akimaanisha hapendi waTanzania wapate taarifa wala wapate Maendeleo.

Kazi na utu, tusonge mbele bila upotoshaji my lady 🐒
 
Hili ni daily news la Tanzania? Kama ndivyo basi kuna kitu hakiko sawa ndani ya system au ni mnyukano wa makundi ndani ya "CCM.

Vinginevyo, tunashuhudia mavadiliko makubwa kabisa katika chombo hiki ambacho nategemea kama msimamo wa chombo uko hivi, ni dhahiri tutashuhudia Chauma ikipewa nafasi sawa na CCM.
 
Back
Top Bottom