Aen Urner
JF-Expert Member
- Aug 31, 2016
- 358
- 351
Salaam, Ninaishi Dasalam. Umri wangu ni miaka 26, kitaaluma mimi ni mhandisi wa mitambo (mechanical engineer) ila sijawahi fanya kazi kama engineer, nimesajiliwa na bodi ya wahandisi na nimepewa kibali cha kufanya SEAP, lakini mpaka sasa shughuli zinazonifanya nisurvive ni kufundisha (teaching) japo kwa sasa sina kituo. Nimekuja kwenu kuomba kushikwa mkono kwenye moja kati ya haya au yote: (1) Connection kwenye kupata sehemu yoyote ya kufundisha; Nina uwezo wa kufundisha masomo matatu kwa ufasaha Physics, Chemistry na Mathematics kwa level zote, uzoefu upo wa kutosha. (2) connection kwenye kupata Taasisi/kampuni ya kufanya SEAP au kujishikiza ili niweze kuendeleza taaluma yangu ya uhandisi. Natanguliza shukurani zangu!