Bantulile, tunaungana kuwafanyia thathmini pana viongozi wetu katika wingi na ukubwa wa mazuri na mabaya yao.
Kiongozi mtumia rushwa na fisadi, ameshajiengua wala hana nafasi ya kupimwa tena kwa uhudhriaji wake misibani, kutoa michango kwa makundi au propaganda. Kosa la ufisadi na rushwa linafunika wema na uzuri wowote wa kiongozi.
Kiongozi anayesaliti katiba, anasaliti uma. Hata angejaribu kujitabasamisha namna gani huyo hafai kuongoza umma kwa sababu hatasimamia maslahi ya umma.
Ninakubaliana na wewe kabisa kwamba kiongozi ni mdau wa masuala yote yanahusu jamii anayoiongoza na anapaswa kuyashughulikia. Tatizo linakuja namna gani anashughulikia? Kujaribu kuvuruga amani ya nchi kinyume na misingi ya katiba na utaifa eti unashughulikia tatizo la kundi moja? Unashughulikia tatizo la kundi moja kwa gharama ya uhai wa taifa? Hapo ndipo sifa ya Pinda ilipoondoka na mahakama yake ya kadhi.
Hivi leo wafanyabiashara wanagoma kulipa kodi, halafu kiongozi anaanza kushirikiana nao kuboresha mgomo ili kodi walipe wafanyakazi peke yao. Ni sahihi? Kwamba kwa kuwa hawataki basi atafute lugha ya kuwashawishi wafanyakazi wakubali klipa kodi peke yao kuwaridhisha wafanya biashara waiogoma? Hapana ndugu. Huo si uongozi.
Migogor yote inatatuliwa kwa kurejea kwenye constitution. Hivi kulikuwa na haja gani Pinga kulazimisha hasi muswada wa kuvuanja sheria za nchi na kuvuruga amani? Hajui kama katiba inasemaje? Huyu Pinda na wenziye wa ccm (wanafiki wachache), wangekuwa wakweli, na wana uchungu na taifa, walishindwa nini kuwapa elimu ya uraia na katiba hao waliotka dini yao iwe ya seriakli? Kilichowafanya hadi waingize kwenye ilani ni nini kama si unafiki, na woga wa kuitetea katiba ya Jamhuri?
Hapo ndipo Pinda na ccm fisadi, wamethibitisha hawawezi ama kwa hiyari ama kwa mfumo wa chama chao, ama kwa kundi dogo lenye nia ovu na taifa, kuitetea na kuisimamia katiba na hivyo hatuhitaji tena kuwapima kwa vitu vingine ingawa hata hivo yak mengi sana waliyopwaya.
Kwa ufupi, Mahakama ya kaedhi alivyoishughulikiapinda, hafai kuwa kiongozi wa umma.
Lowasa kwa wizi, rushwa , ufisadi na uwongo uwongo wake wa kuhadaa, hafai kuwa kiongozi wa umma na hatuna sababu ya kuwaupima kwa namna nyingine kwa sababu makosa yana constitute major constitutional offences na actually wanastahili kushitakiwa.
Hatuhitaji watu wenye usafi wa kutafutiza kwenye nafasi zoe za uongozi.
Hope umenielewa kiongozi.
Tatizo la baadhi ya watanzania hupima urais kwa kigezo kimoja tena kigezo dhaifu kama mahakama ya kadhi. Hata waisilam sio wote wanashadadia mahakama ya Kadhi sembuse wakristo au hata wapagani? Suala sio kusema Pinda anaipenda hoja ya Mahakama ya Kadhi hoja ni namna gani ameishughulikia? Hata kama haijakubalika yeye binafsi kama kiongozi amelishughulikiaje.Hawezi kuacha kulishughulikia kwa sababu tu yeye sio Mwisilamu, la hasha! Yeye siyo kiongozi wa kidini ni kiongozi wa kisiasa. Kiongozi hufanyi jambo lile unalolipenda tu hata usilolipenda lakini kuna wananchi ambao wewe ni kiongozi wao wana jambo wanalolipenda wewe unawasaidiaje kufikia malengo yao. Uraisi ni mambo mengi yanayoshikana kwa pamoja (complex) Kumkataa mtu kwa sababu ya jambo moja tu Mahakama ya Kadhi na huwezi kumkubali mtu kwa sababu ya Mahakama ya Kadhi tu, tumwangalie mtu in his totallity. Kama vile watu kumjudge mtu kwa jinsi anavyotoa rushwa kwenye vikundi vya dini au kijamii. Hapana uraisi ni mchanganyiko wa sifa nyingi zikijumuishwa kwa pamoja.