apolycaripto
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 644
- 225
Hakika mtu huyu amepania kuona kama anaweza kuwarubuni kwanza wanaCCM wenzake na hatimaye Watanzania ili awe Rais wa Nchi hii.Ninachukizwa sana na harakati zake za kutafuta uhalali wa kurudi ndani ya serikali akiwa Rais.
Uko wapi usafi wa Lowassa, ikumbukwe kuwa hakuwahi kuelezea siri ya utajiri wake mbali na ule unaodaiwa kama wa kurithi kutoka kwa Mzee wake.Hivi kweli Lowassa anataka kutuhakikishia kuwa ni muadilifu na hajawahi kutuibia watanzania?.Umiliki wa majumba na mashamba pote hapa nchini amepata kihalali pasipo rushwa ama kutumia madaraka aliyokuwa nayo?
Lowassa anapishana kabisa na falsafa ya Mwl. Nyerere kuwa anayekimbilia Ikulu "muogopeni kama ukoma".Mtu huyu alikuwa ametulia sana pamoja na purukushani za magazeti (Mwanahalisi & Tanzania Daima) dhidi yake.Kapita mgongo wa nyuma na sasa amekamata vyombo vya habari kama njia ya kujisafisha kwani sasa ndiye "role model" kuliko hata Rais wa Nchi,Pinda ama Mawaziri Wakuu Wastaafu (ambao hawakujiuzuru).
Tunatambua kuwa Mh. Lowassa alikuwa na miadi na Kikwete kuwa baada yake U-rais utaangukia kwake.Haya ni mawazo na ulevi wa madaraka na kusahau demokrasia ya Wananchi kumchagua nani kuwa kiongozi wao.Hivi Lowassa anadhani wananchi wako nae ama ni WanaCCM (Makada wa Mikoa na Wilaya) wenye manufaa binafsi nae (kifedha na vyeo).Bila shaka anaemuunga mkono Lowassa nitakuwa na mashaka nae kwani huwezi kuwa mchapa kazi huku mwizi.Kazi ili iwe nzuri nimuhimu kuambatana na uadilifu na si "ujanja ujanja".
Tazama bila aibu anajaribu kutoa utetezi kuwa "Mh. Mwenyekiti nilipokuletea jina la Rostam Aziz kama mtu wa kutusaidia kumpata Mwekezaji (Dowans/Richmond) ulikubali bila kusita".Hapa analaumiwa aliyemleta mwizi (Rostam) ama aliyemkubali mwizi?.Ni dhahiri Lowassa hakuwa mbali na Rostam katika "deal na ndio maana alimpendekeza Rostam kwa Kikwete na sio Mengi wala Said.
Leo hii Lowassa karudi kwenye ulingo wa siasa za kitaifa kwa gia ya "ajira kwa vijana ni bomu linalongoja kulipuka"!Itambulike kuwa kati ya shughuli anazozifanya Mkewe zimechangia kupunguza ajira za watu maofisini na kwinginepo.Mke wa Lowassa Bi. Regina ana kampuni ya usafi ambayo imekwapua ajira za watu maofisini kwa kigezo cha ku-outsource na hivyo kufanya vijana wengi ambao wangeweza kuwa ma-office attendants kutokupata ajira hizo, hivyo kubaki kuranda randa mitaani.Ni dhahiri kampuni hii ilikuwa kwa kasi na kupata tenda nyingi Serikalini kipindi ambacho Lowassa alikuwa Waziri MKuu.
Ni nani asiyejua alifanya nini pindi akiwa Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, sehemu kubwa ya ardhi nzuri na majumba ya serikali yaligeuka vitega uchumi kwake.Leo Lowassa anatuaminisha nini?.Aihitaji utafiti mkubwa kujua Lowassa ni gamba na wala ulegelege wa Kikwete si sababu ya Lowassa kuwa SAFI.Watanzania hawakumuhitaji Lowassa kuwa Rais wala Waziri Mkuu hata kabla ya Kikwete.Uteuzi wa Lowassa kuwa Waziri Mkuu ulitokana na uswahiba kati yao wawili (hawakukutana barabarani) na si uchapa kazi,wengi hatukuupenda uteuzi huo japo tulijua lazima iwe hivyo.Vile vile wengi tulishangilia sana pindi alipotamka kujiuzuru, sasa leo umaarufu wake wa kupigiwa ama kujipigia chapuo kuwa Rais wa Nchi hii unatoka wapi? kwa TB JOSHUA (SCOAN).
Lowassa ni Saratani na kimsingi anaombwa kuwaacha watanzania wafikiri nani wa kuwa Rais wao pindi muda muafaka utakapojiri na si vinginevyo.Kutafuta kujiuza kupitia vyombo vya habari tena kwa kutumia pesa ni kujaribu kutuudhi watanzania na isije ikawa ndiye chanzo cha uvunjifu wa amani katika nchi pindi tutakapochoka nae.Wapambe ama wafuasi wake wakubwa ni wenye njaa na tamaa ya madaraka na pilika zao zote si bure bali "quid pro quo".Ni dhahiri nchi yetu yenye watu zaidi ya milioni 45 haiwezi kumkosa kiongozi bora na muadilifu kuwa Rais eti ikamng'ang'ania Lowassa kuwa Rais.Mifano ya Kenya na Afrika Kusini kwetu haina nafasi kabisa kwani tunatofautiana katika mila na desturi pamoja na mafundisho (maadili).
Nimeandika suala hili kutokana na kuona misururu ya magari na wapambe wengi kila siku hapa nyumbani kwake Mahando (Masaki) utadhani msiba au sherehe ya kifahari.Haiwezekani magari kujaza pande zote mbili za barabara pasipo sababu hasa baada ya kudai "amelipua bomu NEC Dodoma".Bila shaka amekwisha anza kampeni na wapambe wake ama wanafiki wanaomsaidia kucheza na akili za Watanzania.Nasema wanajidanganya kwani zama hizi si zile za chama kimoja.Lowassa atambue kuwa CCM wakimpitisha kwa (hongo na ombwe) Watanzania tuna pengi pa kuchagua na si yeye na chama chake.Maadam alijiuzuru (resigned) (sio kustaafu (retired)) lakini anapata heshima ya retired Prime Minister ashukuru Mungu kwani akituchafua ajue hata hiyo "illegal benefit " anayopata itageuka shubiri.
Uko wapi usafi wa Lowassa, ikumbukwe kuwa hakuwahi kuelezea siri ya utajiri wake mbali na ule unaodaiwa kama wa kurithi kutoka kwa Mzee wake.Hivi kweli Lowassa anataka kutuhakikishia kuwa ni muadilifu na hajawahi kutuibia watanzania?.Umiliki wa majumba na mashamba pote hapa nchini amepata kihalali pasipo rushwa ama kutumia madaraka aliyokuwa nayo?
Lowassa anapishana kabisa na falsafa ya Mwl. Nyerere kuwa anayekimbilia Ikulu "muogopeni kama ukoma".Mtu huyu alikuwa ametulia sana pamoja na purukushani za magazeti (Mwanahalisi & Tanzania Daima) dhidi yake.Kapita mgongo wa nyuma na sasa amekamata vyombo vya habari kama njia ya kujisafisha kwani sasa ndiye "role model" kuliko hata Rais wa Nchi,Pinda ama Mawaziri Wakuu Wastaafu (ambao hawakujiuzuru).
Tunatambua kuwa Mh. Lowassa alikuwa na miadi na Kikwete kuwa baada yake U-rais utaangukia kwake.Haya ni mawazo na ulevi wa madaraka na kusahau demokrasia ya Wananchi kumchagua nani kuwa kiongozi wao.Hivi Lowassa anadhani wananchi wako nae ama ni WanaCCM (Makada wa Mikoa na Wilaya) wenye manufaa binafsi nae (kifedha na vyeo).Bila shaka anaemuunga mkono Lowassa nitakuwa na mashaka nae kwani huwezi kuwa mchapa kazi huku mwizi.Kazi ili iwe nzuri nimuhimu kuambatana na uadilifu na si "ujanja ujanja".
Tazama bila aibu anajaribu kutoa utetezi kuwa "Mh. Mwenyekiti nilipokuletea jina la Rostam Aziz kama mtu wa kutusaidia kumpata Mwekezaji (Dowans/Richmond) ulikubali bila kusita".Hapa analaumiwa aliyemleta mwizi (Rostam) ama aliyemkubali mwizi?.Ni dhahiri Lowassa hakuwa mbali na Rostam katika "deal na ndio maana alimpendekeza Rostam kwa Kikwete na sio Mengi wala Said.
Leo hii Lowassa karudi kwenye ulingo wa siasa za kitaifa kwa gia ya "ajira kwa vijana ni bomu linalongoja kulipuka"!Itambulike kuwa kati ya shughuli anazozifanya Mkewe zimechangia kupunguza ajira za watu maofisini na kwinginepo.Mke wa Lowassa Bi. Regina ana kampuni ya usafi ambayo imekwapua ajira za watu maofisini kwa kigezo cha ku-outsource na hivyo kufanya vijana wengi ambao wangeweza kuwa ma-office attendants kutokupata ajira hizo, hivyo kubaki kuranda randa mitaani.Ni dhahiri kampuni hii ilikuwa kwa kasi na kupata tenda nyingi Serikalini kipindi ambacho Lowassa alikuwa Waziri MKuu.
Ni nani asiyejua alifanya nini pindi akiwa Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, sehemu kubwa ya ardhi nzuri na majumba ya serikali yaligeuka vitega uchumi kwake.Leo Lowassa anatuaminisha nini?.Aihitaji utafiti mkubwa kujua Lowassa ni gamba na wala ulegelege wa Kikwete si sababu ya Lowassa kuwa SAFI.Watanzania hawakumuhitaji Lowassa kuwa Rais wala Waziri Mkuu hata kabla ya Kikwete.Uteuzi wa Lowassa kuwa Waziri Mkuu ulitokana na uswahiba kati yao wawili (hawakukutana barabarani) na si uchapa kazi,wengi hatukuupenda uteuzi huo japo tulijua lazima iwe hivyo.Vile vile wengi tulishangilia sana pindi alipotamka kujiuzuru, sasa leo umaarufu wake wa kupigiwa ama kujipigia chapuo kuwa Rais wa Nchi hii unatoka wapi? kwa TB JOSHUA (SCOAN).
Lowassa ni Saratani na kimsingi anaombwa kuwaacha watanzania wafikiri nani wa kuwa Rais wao pindi muda muafaka utakapojiri na si vinginevyo.Kutafuta kujiuza kupitia vyombo vya habari tena kwa kutumia pesa ni kujaribu kutuudhi watanzania na isije ikawa ndiye chanzo cha uvunjifu wa amani katika nchi pindi tutakapochoka nae.Wapambe ama wafuasi wake wakubwa ni wenye njaa na tamaa ya madaraka na pilika zao zote si bure bali "quid pro quo".Ni dhahiri nchi yetu yenye watu zaidi ya milioni 45 haiwezi kumkosa kiongozi bora na muadilifu kuwa Rais eti ikamng'ang'ania Lowassa kuwa Rais.Mifano ya Kenya na Afrika Kusini kwetu haina nafasi kabisa kwani tunatofautiana katika mila na desturi pamoja na mafundisho (maadili).
Nimeandika suala hili kutokana na kuona misururu ya magari na wapambe wengi kila siku hapa nyumbani kwake Mahando (Masaki) utadhani msiba au sherehe ya kifahari.Haiwezekani magari kujaza pande zote mbili za barabara pasipo sababu hasa baada ya kudai "amelipua bomu NEC Dodoma".Bila shaka amekwisha anza kampeni na wapambe wake ama wanafiki wanaomsaidia kucheza na akili za Watanzania.Nasema wanajidanganya kwani zama hizi si zile za chama kimoja.Lowassa atambue kuwa CCM wakimpitisha kwa (hongo na ombwe) Watanzania tuna pengi pa kuchagua na si yeye na chama chake.Maadam alijiuzuru (resigned) (sio kustaafu (retired)) lakini anapata heshima ya retired Prime Minister ashukuru Mungu kwani akituchafua ajue hata hiyo "illegal benefit " anayopata itageuka shubiri.