Mh. Dr. Mwakyembe ushauri huu muhimu

Mh. Dr. Mwakyembe ushauri huu muhimu

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,198
Reaction score
7,535
Waziri Mwakiembe kwa mara kadhaa ameonekana akijitahidi kukabiliana na watu wanao ihujumu nchi hii;

Wakati Fulani akifanikiwa kiasi na wakati Fulani akikwama na mara nyingine kupata madhila kama wote tunavyo fahamu.Kauli ambazo amezitoa Waziri Mwakyembe jana wakati akihojiwa katika kipindi cha "Jenerali On Monday" kinachorushwa na Channel Ten ; zina nisukuma kuamini kwamba mzee wetu huyu (Mwakyembe) anahitaji ushauri makini ili kuweza kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi huku akibaki na hadhi yake ya kisiasa na kibinadamu.

Naamini ni sisi tunao weza kumshauri mzee wetu huyu.Katika mahojiano hayo nimejifunza mambo yafuatayo ambapo binafsi yana nitia woga sana.

Moja.Sio tu kwamba mwakyembe anafahamu na kukubali kwamba watu hawana imani na baadhi ya vyombo vya usalama ikiwemo Polisi; bali pia yeye mwenyewe anaonekana kutokuwa na imani na vyombo hivyo. kwa mfano, alipoulizwa kuhusu jinsi watakavyo washughulikia walio kamatwa na madawa ya kulevya JNIA, alisema ashafikisha kesi zote Polisi na kuongeza "Safari hii wakisema tena ushahidi haujakamilika na wakati kuna video mimi sitawaelewa".

Alipoulizwa kama mtu ana taarifa ya madawa ya kulevya apeleke wapi? Alisema "Apeleke kwa vyombo vya serikali,kama haviamini basi azilete kwangu" aliongeza tena "Safari hii wakileta upuuzi upuuzi wao; nitaleta video hapa channel ten watu waione". n.k Kwa ku yaangalia kwa makini majibu hayo ya Waziri Mwakyembe, ni wazi kwamba sio tu kwamba anafahamu kuwa watu hawa amini baadhi ya vyombo vya serikali ikiwemo Polisi (kwa kuwa ha viaminiki) bali pia hatayeye mwenyewe haviamini sawa sawa. Sasa yeye kama waziri kama haamini vyombo hivyo, na maana yake atakuwa kesha jaribu kuongelea hilo ndani ya Baraza la Mawaziri bila mafanikio, na sasa analisema hadharani;

Swali analopaswa kujiuliza ni je! Hata kama atakuwa anapelekewa taarifa yeye kama yeye huku vyombo vya usalama haviaminiki je! Ataweza kutekeleza majukumu yake kama waziri?

Mbili. Inaonekana kuna hali ya viongozi kuogopana wao kwa wao hata kama mmoja wao ni sehemu ya tatizo, wenzake wana muogopa kwa sababu ambazo sio za wazi sana (Pengine kwa kuwa wako ndani ya chungu kimoja). Kwa mfano Waziri mwakyembe amesema kuna kesi zaidi ya 36 ambazo amezifikisha Polisi ndani ya mwaka mmoja lakini hazina mrejesho.

Anasema kuna Begi lilikamatwa ndani yaEmirates siku nyingi zilizopita,lilikuwa lishaingizwa kwenye ndege huku likiwa na unga na tag iliyoonesha jina la mwenye begi lakini mpaka leo mwenye begi hajaonekana na yeye (Mwakyembe ) hajui kama begi hilo lipo bado, na kama lipo liko wapi.Anatoa mifano mingine kibao ya namna hiyo lakini hatimaye anahitimisha kwa kusema "Waziri wa mambo ya ndani anachapa kazi si mchezo. Namwamini sana nchimbi". Kimantiki mtu huhitimisha alichokiongea.

Sasa tukijiuliza ni kwa nini Mwakyembe Analalamika kwamba kati ya kesi zote 36 alizofikishaPolisi (Wizara ya mambo ya ndani) hazijaleta mrejesho halafu anahitimisha kwa kumsifu Waziri wa Wizara hiyo kwa kuchapa kazi? Ni wazi kuna hali ya kuogopana hivyo hata kama mtu anapigania haki ndani ya serikali hii ya CCM, anatakiwa awe anafanya hivyo huku akiipaka mafuta batili kiujanja sana kitu ambachoni hatari.

Tatu. Inaonekana Mwakyembe ana nia njema lakini kuna vitu vinamfanya kukwama na hivyo kujikuta nafsi ikimsuta. Kwa mfano alipoulizwa kuhusu kiwango cha madawa yanayopita KIA, alisema "Kia wanakamatwa sana na ndio maana wanapenda kupitishia dar" alipoulizwa kwamba kwa hiyo udhaifu uko Dar?Anasema " JNIA sio mchezo; anaetaka ajaribu aone".

Sasa ukiangalia kwa makini unakuta kauli hizi zinagongana zenyewe kwa zenyewe na tafsiri ninayo ipata hapa ni kuwa Mwakyembe angependa JNIA kuwe "Drugs free zone lakini anakwamishwa na wenzake" na hataki kukubali wazi kwamba anakwamishwa kwa sababu yeye ni sehemu ya mawaziri.

USHAURIWANGU KWA MWAKYEMBE.

1. Mimi ningekuwa ndio Mwakyembe; Ninge durusu na kujiridhisha kama bado inafaa kuendelea kufanya kazi na Baraza hili la Mawaziri na nikafanya kazi zangu kwa ufanisi, huku nikiitii dhamira yangu na kulinda hadhi yangu kama binadamu, mwanasiasa na mtanzania mzalendo. Kama nikiona sio ; basi ninge jiuzulu uwaziri .

2. Ninge jipima na kujiridhisha kama bado ninafaa kuendelea kuwa mwanaCCM katika mazingira haya! zaidi ya hapo, namtakia Mwakiembe kila la heri japo mmmh! Sijui...................!
 
Ushauri wako kwamba angejiuzuru haufai, nahisi umetumwa!
 
Ushauri wako kwamba angejiuzuru haufai, nahisi umetumwa!
Sijaanza kwa kusema ajiuzulu. Hujanielewa vizuri. Nimesema ajifikirie kama anaweza kuendelea kufanya kazi na watu anaofanya nao sasa. Ukumbuke kwamba kama unafanya kazi na watu ambao unatofautiana nao misimamo, fikra, hisia na malengo kwa kiwango kikubwa; ni vigumu kufanikiwa hata kama una nia njema. Ukumbuke kuwa kwa mfano anakuambia kapeleka kesi zaidi ya 36 polisi zenye ushahidi wa wazi lakini mpaka leo hamna feedback. wewe unadhani ni kwa nini? je katika mazingira ya namna hiyo; si ataendelea kupeleka kesi huku wenzake wanamzunguka?
 

Kimantiki mtu huhitimisha alichokiongea. Sasa tukijiuliza ni kwa nini Mwakyembe Analalamika kwamba kati ya kesi zote 36 alizofikishaPolisi (Wizara ya mambo ya ndani) hazijaleta mrejesho halafu anahitimisha kwa kumsifu Waziri wa Wizara hiyo kwa kuchapa kazi? Ni wazi kuna hali ya kuogopana hivyo hata kama mtu anapigania haki ndani ya serikali hii ya CCM, anatakiwa awe anafanya hivyo huku akiipaka mafuta batili kiujanja sana kitu ambachoni hatari. 3. Inaonekana Mwakyembe ana nia njema lakini kuna vitu vinamfanya kukwama na hivyo kujikuta nafsi ikimsuta. ..........!
betlehem
Ndugu helewa somo hapo kuwa kikwazo ni DPP, Itakuwa yeye kila fahili likija Ushahidi hautoshi.
 
Huyo ndiyo Mwakyembe, bwana misifa na mtu mwongo sana. Unajua mwongo huwa anasahau alichosema muda uliyopita? Ndiyo maana umeona contradictions nyingi katika majibu yake!

Huyo Ndiye Dr Harrison Mwakyembe bwana!!
 
Dunia ni mahala pabaya kuishi si kwa sababu waovu ni wengi ila ni kwa sababu waadilifu wachache waliopo wamekaa kimya, Mwakyembe kama kaamua kutokukaa kimya na akazungumza hali halisi, ushauri wako wa kutoka kwake ndani ya SYTEM ili achape kazi kwa umakini kwa muktadha huu haufai
 
mh. Waziri sio mkweli na hivi vita haviwezi kwasababu.

1: anajaribu kukata matawi na kuacha mizizi, hili liko wazi kuwa wanaokamatwa ni watu wadogo sana ambao kama waziri angekua na dhamira ya dhati wangetumika kama thread ya kukamata wahusika wakubwa, mfano wanaomfahamu Masogange watakubali kwamba hawezi kuwa na mtaji binafsi wa 6b za kuendeshea boashara ya madawa ya kulevya, so lugha rahisi ni kuwa wanatumwa na watu wenye uwezo. Hili jana kwenye kipindi cha jana alikwepa kulijibu baada ya mama mmoja kutoka morogoro kupiga simu na kumwambia waziri atumie hawa waliokamtwa kutaja wanowatuma, katika majibu yake akasema watu wanoawajua wauza unga wampelekee majina kwa sababu tunaishi nao mitaani tunawajua، haya ni majibu rahisi kwa waziri kutoa, lakini pia kwa nn asitumie majina ambayo rais alisema anayo?

2: kuna baadhi ya wanasiasa wengine bado wako kwenye serikali wengine wastaafu wamekua wakisema kuwa nchi itakuja kuongozwa na wauza unga, kwa tafsiri nyepesi tu ni kuwa either kuna 2015 presidential aspirant anafanya hii biashara au anaungwa mkono na watu wanaofanya biashara hii haramu, waziri hajatuambia kama hao wanasiasa wamehojiwa juu ya kauli zao hizo!!

3: mwakiembe ni mtu wa maneno, mtakumbuka wakati wa ripoti ya Richmond akisema kuna mengine hakusema ili kulinda serikali, juzi tena akasema kesho nitawataja wauza unga na picha zao ili wananchi wawajue, siku ilipofika akataja wafanyakazi wa uwanja wa ndege, sasa inawezekana hakujua vita hivyo ni vigumu kiasi gani.

Mwisho naungana wenzangu hapo juu kuwa waziri kama anadhamira ya kupambana na madawa ya kulevya basi yuko peke yeke, na inavyojulikana ili serikali ifanikiwe kwenye mapambano yoyote ile iwe ya umaskini au uharamia lazima ifanye kazi kama system, sasa kama anapambana peke yeke wenzake wanahujumu hata fanikiwa milele.
 
Hatajiuzulu....akisha sema wengi serikalini wananuka
Rushwa na walioko chini yake ATAWASHUGHULIKIA... sijaona point yako....ushauri upi...huna...many words...so akiwa hana imani na vyombo vya usalama AWAACHEEE...?? huna point...
 
Mwakyembe yupo makini sana, Naamini wizara yake ikiunganishwa na Ile ya mambo ya ndani na yeye ndio awe waziri wake. watu wangewekwa uchi sana.

Hongera Mwakyembe unaonyesha kuwa Serikali ikiamua inaweza.!!!
 
Wakati nikifuatilia kipindi cha mahojiano ya TV ya dr Mwakyembe alitokea rafiki na jirani yangu ambaye ni ofisa wa polisi kwanza alimsifu sana mh mwakeymbe kwa uchapaji wake kazi ila akasema kinachomwangusha ni kutoshirikisha mawazo nje yake na hii imekuwa ni tabia ya viongozi wengi wa serikali, kwa mfano anasema ule mfumo wa ulinzi wa airport ni wa kizamani sana sio wa kisasa kama Mh. Mwakyembe alivyodai pia hautoshelezi ulinzi wa uwanja ukilinganisha na ukubwa wa uwanja kwani ulinzi wa uwanja wa ndege sio mizigo tu ni rasilimali zote zilizopo uwanjani mfumo huo si toshelezi.

akanigusia kuwa wao ndani ya jeshi la polisi wameisha andaa mfumo shirikishi wa ulinzi wa kisasa kabisa kwa ajili ya jiji na majiji mengine na taasisi zake kama airport na bandari na taasisi nyingine zinazohitaji ulinzi wa polisi na hivi soon wataanza kuujenga huo mfumo ambao ni shirikishi ambapo vyombo vyote vya ulinzi vya nchi na taasisi husika kwa wakati mmoja vitaweza ku monitor matukio moja kwamoja kila idara kivyake bila kumbugudhi mwenzake na kutoa tahadhari za kitaalam hata kabla tukio baya halijatokea akaendelea kusema bila kuwa na mfumo shirikishi ambao vyombo vya ulinzi vitaweza kupata accesss ya kufuatilia matukio live yanayoendelea tatizo la uhalifu litaendelea kwa sababu bado inapotokea tatizo idara za upelelezi zitaendelea kuomba hisani ya matukio yaliyorekodiwa na taasisi husika ambayo mengi yatakuwa ni yenye kulinda interest zao hata mengine kuyaficha lakini kama mfumo ni shirikishi huitaji kwenda airport au bandari kwani kila kilichotokea kinakuwa kilishaonekana kwenye idara nyingine nyeti za usalama.

aliendelea kunihabarisha kuwa mfumo wao waliokuwa wameuandaa ungeweza kutoa ulinzi wa kisasa katika taasisi zote kama airport bandari na hivyo hujuma zingeisha kabisa hivyo pia ameshauri kama viongozi wa serikali wangekuwa wanabadilishana mawazo na wenzao na sio kila kitu kwenda kivyake nchi hii ingepiga hatua sana kwa mfano amesema kama Dr mwakyembe angewasiliana na jeshi la polisi lingempa mikakati yake ya ulinzi wa kutumia technolojia na wala Mwakyembe asingeweza kutangaza tender ya kufunga vifaa vya ulinzi bandarini tena kwa mkopo aghali wa benki ya dunia badala yake bandari ingeongezea nguvu zake kidogo kwenye mradi huo wa polisi na kuokoa mabilioni ya walipa kodi kuliwa na wajanja bila sababu kwa kuwa mfumo wao ni rahisi na sio gharama kubwa kama unavyoweza kuwa wa bandari hivyo hata kumletea kashfa bila yeye kujua wakati ni mtendaji mahiri na mchapa kazi ambaye kila mtanzania hawezi kubishania hilo.

Hivyo nami ninamshauri Dr mwakyembe kama hizi habari ni kweli kutana na Mkuu wa polisi IGP kwani nasikia ni ndoto zake kuhakikisha ana acha mfumo huu ukifanya kazi kama legacy yake mzungumze mshauriane kuhusu hili na ikibidi muunganishe nguvu tuweze kuwa na mfumo bora wa ulinzi lakini uwe ni affordable nina imani Dr mwakyembe unapita humu au washauri wako hivyo utawasiliana na watu wa polisi kuzungumzia jambo hili kwa faida ya nchi na hata kuokoa pesa zinazotaka kutumika bandari nina imani utakuwa hujachelewa kuanza mazungumzo haya hata leo kwa ajili ya faida ya nchi.
 
Si wanakutana kwenye baraza la mawaziri? huko ndipo wanaweza kujadili vizuri na kupata exparties ya Chimbi--Waziri wa wizara husika.Yeye kumfuata IGP ni kuingilia wizara ya mwenzake.......Protocal ni muhimu pia otherwise mtachanganyana sana kwenye utendaji....
 
Kufanya kazi na mtu/uongozi usiokuwa na imani nao ni busara kujiuzulu(kuachia ngazi) ili uonesha kuwa huna imani na serikal yako na kuonesha m,simamo wako!
 
Wakati mwingine naona fadhali afanye kazi km yy bila kushirikisha wengine. Jamii hii imeoza, ukimshirikisha mtu huyohuyo anakuwa wa kwanza kutoboa siri na kuivujisha maana mtandao wa mafisadi ni mkubwa sana.

Kwani hao wanaojidai eti mfumo shirikishi walikuwa wapi hadi majanga yatokee ndio eti wajidai ooh wao hawajashirikishwa?

Imefika wakati kwa viongozi jasiri km Dr.Mwakyembe kijitoa mhanga kwa manufaa ya Taifa. Najua kuna wanaokasirishwa sana nautendaji wake wako tayari hata kumtoa roho km walivyofanya kwa marehemu Sokoine. Ila kwa hali ilivyo sasa, unaweza mshirkisha mtu akakugeuka kabla hamjatekeleza mliyopanga.

Dr. endeleza wembe huohuo utapata tu wa kukuunga mkono na Mungu akulinde na akubariki kwa kazi nzuri tunayoiona na sio porojo za kisiasa za kujaza matumbo supu ya utumbo asubuhi na kupiga miayo km kiboko. Tunataka vitendo na siyo porojo porojo tu.
 
Si wanakutana kwenye baraza la mawaziri? huko ndipo wanaweza kujadili vizuri na kupata exparties ya Chimbi--Waziri wa wizara husika.Yeye kumfuata IGP ni kuingilia wizara ya mwenzake.......Protocal ni muhimu pia otherwise mtachanganyana sana kwenye utendaji....

Mkuu, kuna watu huwa wanakurupuka sana. Usikute pia aliyempa taarifa hizo ni Polisi FEKI maana siku hizi wamejaa kweli mitaani. zamani tulikuwa tu tunasikia habari za maafisa usalama feki kumbe siku hizi mpaka mapolisi wapo feki, ma JWTZ nao wapo feki, si mnamkumbuka yule jamaa alipiga picha na GODBLESS LEMA?
 
Wakati mwingine naona fadhali afanye kazi km yy bila kushirikisha wengine. Jamii hii imeoza, ukimshirikisha mtu huyohuyo anakuwa wa kwanza kutoboa siri na kuivujisha maana mtandao wa mafisadi ni mkubwa sana.

Kwani hao wanaojidai eti mfumo shirikishi walikuwa wapi hadi majanga yatokee ndio eti wajidai ooh wao hawajashirikishwa?

Imefika wakati kwa viongozi jasiri km Dr.Mwakyembe kijitoa mhanga kwa manufaa ya Taifa. Najua kuna wanaokasirishwa sana nautendaji wake wako tayari hata kumtoa roho km walivyofanya kwa marehemu Sokoine. Ila kwa hali ilivyo sasa, unaweza mshirkisha mtu akakugeuka kabla hamjatekeleza mliyopanga.

Dr. endeleza wembe huohuo utapata tu wa kukuunga mkono na Mungu akulinde na akubariki kwa kazi nzuri tunayoiona na sio porojo za kisiasa za kujaza matumbo supu ya utumbo asubuhi na kupiga miayo km kiboko. Tunataka vitendo na siyo porojo porojo tu.

Mambo ya mfumo shirikishi ni kuleta siasa kwenye vyombo vya dola. ndo maana tangia mfumo shirikishi na polisi jamii vianzishwe, mambo yanaenda hovyo sana. ulinzi shirikishi unafaa kwenye vituo vya daladala tu na si katika maeneo nyeti kama Airport
 
Eti mpango huo ulikwepo!!!! mbona walikuwa hawauweki mpaka waone mwenzao kaaamua kufanya kweli ndio wanaibuka eti na wao walikuwa na mpango huo huo. Ukweli ni kwamba madawa ya kulevya hayajaanza leo, IGP anajua ila ni wale waleeee wa ile stail ya kujifanya kama huoni au unashughulikia lkn taratibu ili jamaa wafanye fasta fasta wakati unataka kutoka madarakani ndio unajifanya kuwa serious. Janja ya nyani hiyo. Mwakyembe amewashtukia mwache aendeleee. KAZA BUTI MWAKYEMBE.
 
Wakati mwingine naona fadhali afanye kazi km yy bila kushirikisha wengine. Jamii hii imeoza, ukimshirikisha mtu huyohuyo anakuwa wa kwanza kutoboa siri na kuivujisha maana mtandao wa mafisadi ni mkubwa sana.

Kwani hao wanaojidai eti mfumo shirikishi walikuwa wapi hadi majanga yatokee ndio eti wajidai ooh wao hawajashirikishwa?

Imefika wakati kwa viongozi jasiri km Dr.Mwakyembe kijitoa mhanga kwa manufaa ya Taifa. Najua kuna wanaokasirishwa sana nautendaji wake wako tayari hata kumtoa roho km walivyofanya kwa marehemu Sokoine. Ila kwa hali ilivyo sasa, unaweza mshirkisha mtu akakugeuka kabla hamjatekeleza mliyopanga.

Dr. endeleza wembe huohuo utapata tu wa kukuunga mkono na Mungu akulinde na akubariki kwa kazi nzuri tunayoiona na sio porojo za kisiasa za kujaza matumbo supu ya utumbo asubuhi na kupiga miayo km kiboko. Tunataka vitendo na siyo porojo porojo tu.

Ulilosema nilakweli ndugu, kwanza huyo waziri wa wizara husika mwenyewe umemsikia akilizungumzia hili? mimi mara ya mwisho nilimsikia pale pungeni akitetea maovu sijamsikia tena baada ya hapo
 
9k=
2Q==
 
Ulilosema nilakweli ndugu, kwanza huyo waziri wa wizara husika mwenyewe umemsikia akilizungumzia hili? mimi mara ya mwisho nilimsikia pale pungeni akitetea maovu sijamsikia tena baada ya hapo

Ni kweli sijamsikia, ndg yangu ulinzi wa pale Airport ulivyo huwezi amini magunia yale ya dawa eti yapite bila big boss kuidhinisha, hako ni kamchezo kachafu kalifanyika na hakika kuna wakubwa akaunti zao zinahemea juu juu kwa mpunga waliolishwa.

Ww fikiria, eti mtu wa kawaida pale airport akipita hata na wembe tu unaonekana na begi linafunguliwa hadi atoe huo wembe, sasa iweje magunia ya unga yapite kilaiiini namna hiyo. mm nahakika hapo kuna chain ya wahusika katk njama hizo, dili km hilo halichezwi na striker mmoja lazima kulikuwa na mlinda mlango mashuhuri, mabeki, mid fielders na strikers kadhaa na hata washangiliaji.
 
Ingekuwa vyema pia kwenda kukagua akaunti za staff wote waliokuwepo siku hiyo km zilijaa mpunga wa ghafla ghafla
 
Back
Top Bottom