Nina uhakika kinachoendelea dhidi ya Katoliki si mzaha wala burudani, bali ni dharau, dhihaka na kejeli ya wazi dhidi ya Katoliki na Imani ya Kikristo kwa ujumla. Hii ni hatua hatari sana kwa Taifa.
Mzaha wa aina hii hauwezi hata kufikiriwa kufanywa na vijana wa Kikristo dhidi ya taasisi za dini ya Kiislamu.
Hebu jaribu kufikiria, hata kwa sekunde moja, vijana wa Kikristo wajifanye Waislamu halafu waandamane hadi BAKWATA. Je, hali ingekuwaje? Jibu lake liko wazi, mambo yangechukua mwelekeo mwingine kabisa.
Leo watu wanaandamana hadi Ubalozi wa Vatican bila kizuizi chochote, huku vyombo vya dola vikitazama kana kwamba hakuna tatizo. Halafu bado mtu anataka kutuambia kwamba hili sio kazi ya dola wala uzembe wa makusudi?
Huu ni ukimya unaohatarisha Taifa. Serikali, kwa kuruhusu hali hii, mnafungua mlango mpana wa uharibifu wa amani na mshikamano wa kitaifa. Mnasahau jambo moja muhimu sana, ndani ya vyombo vya dola kuna Polisi, Usalama wa Taifa, na Jeshi na ndani yake kuna Wakristo wengi, wakiwemo Wakatoliki.
Kuendelea kudharau imani yao hadharani ni kuchezea hisia za hao . Hili ni jambo la hatari kubwa. Mkiendelea hivi, mtakuwa mnaandaa mazingira ya mgongano wa kijamii na kidini ambao matokeo yake yatakuwa mabaya mno kwa Taifa.
Onyo hili si la kejeli wala si la vitisho, ni mwito wa akili na busara. Acheni mara moja. Acheni kabisa. Rudisheni upumbavu huu nyuma kabla haujageuka janga la kitaifa.
Mzaha wa aina hii hauwezi hata kufikiriwa kufanywa na vijana wa Kikristo dhidi ya taasisi za dini ya Kiislamu.
Hebu jaribu kufikiria, hata kwa sekunde moja, vijana wa Kikristo wajifanye Waislamu halafu waandamane hadi BAKWATA. Je, hali ingekuwaje? Jibu lake liko wazi, mambo yangechukua mwelekeo mwingine kabisa.
Leo watu wanaandamana hadi Ubalozi wa Vatican bila kizuizi chochote, huku vyombo vya dola vikitazama kana kwamba hakuna tatizo. Halafu bado mtu anataka kutuambia kwamba hili sio kazi ya dola wala uzembe wa makusudi?
Huu ni ukimya unaohatarisha Taifa. Serikali, kwa kuruhusu hali hii, mnafungua mlango mpana wa uharibifu wa amani na mshikamano wa kitaifa. Mnasahau jambo moja muhimu sana, ndani ya vyombo vya dola kuna Polisi, Usalama wa Taifa, na Jeshi na ndani yake kuna Wakristo wengi, wakiwemo Wakatoliki.
Kuendelea kudharau imani yao hadharani ni kuchezea hisia za hao . Hili ni jambo la hatari kubwa. Mkiendelea hivi, mtakuwa mnaandaa mazingira ya mgongano wa kijamii na kidini ambao matokeo yake yatakuwa mabaya mno kwa Taifa.
Onyo hili si la kejeli wala si la vitisho, ni mwito wa akili na busara. Acheni mara moja. Acheni kabisa. Rudisheni upumbavu huu nyuma kabla haujageuka janga la kitaifa.